Lowassa na Kiingereza chake!

In simple terms, it is fair to conclude that the guy has nothing between his ears!
 
Wewe na huyo mnayelumbana, the difference is the same! Lakini mzee naona umeumia sana kuona watu wanakosoa Mungu wako, alkini ukweli unabaki kwamba huyu bwana anahitaji kujinoa kwa lugha na hoja kama anataka kuwa rais wa nchi hii.
 

Ok!kwa hiyo anafanana fanana kitabia na kimatendo na huyu jamaa sio?!!!kama ni hivyo nadhani mungu akimjalia kushika nafasi ya juu kabisa ya uongozi hapa nchini,jamii forum ijiandae kufungasha virago kuhamia eritrea!
 
Last edited by a moderator:

Ndio mana nikasema huko nyuma hukuwa hivyo;mbona umeshasomeka kamanda,sema tu mimi sio mteja mzuri wa mifereji ya maji taka!ndio mana nakupotezea kiaina!sema tu mshkaji unaonekana king'ang'a lakini hutonipata,this is for sure!
 

Kwani lowassa na mwakyembe wamewahi kukosana!?walikosania kitu gani hasa wewe unavyodhani?
 

Kwa kuongezea tu midahalo anayoizungumzia mdau ni kama hii!nawataka muutazame mdahalo huu halafu mpime ni kiongozi gani hapa kwetu anaweza kupita kama tutakua na midahalo ya dizaini hii ambayo jamaa wa ccm huwa wanakatazwa kushiriki na makamba!

Na huu ni mdahalo wa ndani tu,yani Republican kwa republican!

Mitt Romney & Rick Perry Get Physical In Heated GOP Nevada Debate - YouTube
 
kingereza sio ishu hicho anachoongea kinatosha na ndicho cha wabongo au katiba inasema kuwa rais huwe unapiga slain za kibritish, afu huo urais utampa wewe au? be great thinker

Heee basi kumbe jamii forum ni jukwaa la wasomi wasiojua kusoma kiswahili!!!kuna mahali nimesema mtu asipewe urais kwa kuwa haongei kiingereza?ingetosha tu kupima kiingereza chake na kusema kinafaa kama umeridhika nacho,full stop!
 
Wewe na huyo mnayelumbana, the difference is the same! Lakini mzee naona umeumia sana kuona watu wanakosoa Mungu wako, alkini ukweli unabaki kwamba huyu bwana anahitaji kujinoa kwa lugha na hoja kama anataka kuwa rais wa nchi hii.

Tena ana muda wa kutosha tu kufanya hivyo,sema hawa wapambe wake wanaompenda kupita kiasi na kumsifia kwa kila jambo ndio watamtia ujinga aendelee kuamini kwamba uwezo alionao kwenye angle hizo unatosha!kama anaingia humu mzee wangu yule ningemuomba atusikilize sisi zaidi aachane na hawa wapambe wake wanamdanganya!
 
Je hu jin ntao,au wale masheikh viongozi wa dubai,walihitaji kuwa na kiingereza kizuri au idea za maendeleo kwanza!?

Huyu ndugu yetu wa bagamoyo anajitahidi,achilia mbali umahiri wa lugha zote tatu anazozijua,ana interpersonal skills na public speaking skills za kufa mtu.,,je ametufikisha wapi!??
 

we ina maana husomi au?hii ya wachina kutojua kiingereza si kuna mdau kaielezea kwa kirefu sana page iliyopita tu,acha uvivu kijana rudi page 3 kasome vizuri usikurupuke tu!
 
Prisoner 46664,

Tafadhali sana JK kiingereza hajui vilevile, nitaupload link moja kesho uone alivyoharibu kwenye jukwaa la kukabiliana na anguko la uchumi duniani lililofanyika Arusha cha kushangaza alikuwa anaongelea mambo ya uchumi na ana shahada ya uchumi lakini alionekana hawezi kuchambua mambo katika knowledge ya kiuchumi pia kiingereza kilikuwa kibovu bila kueleweka.

Unajua lugha ina ubovu wa aina tatu wa kwanza ni ubovu wa fasihi yaani grammar lakini unaeleweka kama Idd Amini wa Uganda pamoja na kuwa alikuwa anakosea katika fasihi lakini alikuwa anaeleweka sana anachoongea huitaji kumtazama machoni ujue anaongea nini, ubovu wa pili ni ile hali ya kutokuwa na uwezo wa kuunganisha maneno pia kujua hili litumike wapi.

Pia kutokuwa na vocabulary za kutosha ili kuiongea lugha pia katika huo ubovu wa pili ni kutumia tafsri ya moja kwa moja kutoka katika lugha mama.

Na ubovu wa tatu ni kuwa lugha unaifahamu, unavocabulary za kutosha lakini katika kutamka hueleweki vizuri hilo huwa sio tatizo sana maana unaweza kuandika ukafahamika au ukasoma tahariri au vitabu vya maarifa ukaelewa lakini ubovu wa pili huwa mbaya sana maana watu wa namna ile hata kuandika paper hawaezi kwasababu wana maneno machache katika lugha. kwa maana nyingine walikuwa weupe darasani

Mtu kama Idd Amin akiongea utajua elimu yake haikuwa kubwa tokana na grammar yake lakini alikuwa anaongea vizuri sana hata kutamka alikuwa anatamka vizuri sana kuliko hata Julius Nyerere au Kenyatta wa Kenya. Ndio maana tunasema katika lugha ufundi wa kuitamka lugha ni kipaji lakini kujua kuongea kawaida kwa kutumia fasihi ni usomi ndio maana nchi zinazotumia kiingereza na Marekani pamoja na kwamba wanaongea kiigereza hata kule China, au Japan au Urabuni msomi atatofautishwa na mtu wa kawaida katika ile lugha kutokana na grammar yake.

Hata hapa kwetu anavyoongea Mkapa, Sitta, kikwete, pinda katika kiswahili wanaongea kisomi sio kama watu wengi wa kawaida watakavyokiongea kiswahili pale Tandale, Mwanjelwa Mbeya, Babati, Lindi, Mtwara au usukumani Shinyanga.

Tusichanganye wazaramo na watu wa pwani kuongea kiswaili cha kipwani tukazania ni fasihi uliwasikiliza kwa makini hawatumii fasihi wanaharibu badala ya kuoga wataseka kukoga, badala ya kuosha vyombo watasema kukosha vyombo maana kuna lugha ya darasani ya ya mtaani
 
Last edited by a moderator:
Viongozi wa Tanzania waliokuwa wazuri wa lugha ni pamoja na Mkapa, Nyerere, Abdul Jumbe, Dk Bilal, Salima Ahmed Salim, Warioba, Samuel Sitta, Mwandosya, Mwakyembe, Seif Hamad, Dk Omar Juma, Msuya, Malecela na wengine pia wabovu wa kiingereza ni Kikwete, Sumaye, Lowassa, Ngeleja, na wengine
 
Siwezi Kumlaumu kwa kutamka vibaya manano ya Kiingereza coz hata mm pia nayatamka Vibaya kwa kuwa si Lugha mama kwangu, But kama kiongozi wa nchi unatakiwa kueleweka unapoongea Lugha ya kimataifa!
 
Siyo kwamba tu intonation yake ni mbofumbofu, lakini pia it makes you wonder what exactly he's talking about anapokuja na kauli kama "to improve poverty". Kusema kweli, the guy's a joke, and I have no idea wtf motivates him to make a moronic video appearance of the kind provided above.
 

tumpe muda ila asiwazikilize hawa wapambe wake wanaopigia makofi kila atakachosema ama kufanya hata kama anakosea;wanamuua mpenzi wao kwa kumpenda kupita kiasi na kumlamba miguu,atusikilize sisi tunaomchallenge atafanikiwa sana!
 
Unategemea nini kama wapambe wenyewe ni Hamisi Mgeja, Deo Sanga (Jah People), Guninita, Nchimbi na wengineo? Mzee aume jongoo kwa meno na ajinoe maana hii tuliyiona humu ni aibu. Natamani angemsikia Pinda akiwa anapiga lugha, tena bila kusoma popote wala kukaririshwa!
 
tumpe muda ila asiwazikilize hawa wapambe wake wanaopigia makofi kila atakachosema ama kufanya hata kama anakosea;wanamuua mpenzi wao kwa kumpenda kupita kiasi na kumlamba miguu,atusikilize sisi tunaomchallenge atafanikiwa sana!
Ingawaje nakubaliana na yeye kwamba vitendo vyake vya ufisadi vina-improve poverty ya watanzania na inta-improve zaidi akiingia madarakani!
 

Umesema kweli - kuwa kaongea vizuri na hasa jambo lenyewe la elimu hao wanaokebehi kwani yeye ni mwingereza hadi aongee kama CAMERON
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…