Mimi sina cha kujifunza kwani kama ni kuwafahamu wanasiasa basi nina u-profesa (sio kama wa Kikwete lakini). Mwanasiasa wa kiafrika anaji-behave kulingana na mazingira aliyopo na upepo unavyovuma. Akiona upepo unaovuma ni ''safari za nje kwa wingi'' basi atatetea kuwa zina tija na kusifia kabisa. Akiona upepo unaovuma ni ''kukataza safari za nje'' basi atasifu na kusema kusafiri nje ni uzezeta. Hivyo kwa Lowassa wala sishangai kwani hakuona umuhimu wa tume huru ya uchaguzi wala wizi wa kura alipokuwa CCM lakini mara baada ya kutoka macho yakafumbuka.