Lowassa, marafiki zako hawakuchangii tena?

Lowassa, marafiki zako hawakuchangii tena?

Kwani lazima achangie kila mwaka yeye,tumemuachia Nape achangie nae
 
uroho na tamaa ya kwenda kuinajisi ikulu wa ufisadi ndo vilikua vinamhangaisha
 
Unatoa kiasi ili upate maradufu zaidi, nikama uwekezaji yaani sasa utawekeza kitu gani wkt hakuna mavuno badae hata mimi napiga kimya
 
Mtoa mada hivi milioni unajua ina sifuri ngapi baada ya namba tano..!!? Huenda tunaongea na mtu ambae hajui hata kuiandika achilia mbali kuishika..!! Acheni dharau kwa watu wanaojitolea kusaidia wengine. Kuna watu wanasema amepeleka pampas,pampas za milioni 5 hapo morogoro si angekusanya mtaa mzima!! Hakuna mfanyabiashara mwenye pampas za milioni 5 morogoro. Me nna duka la pampas tupu tandika,lkn mtaji haufiki milioni 5 na duka limejaa..!!! Mtu hujawahi kushika hata laki 3 unadharau milioni 5???
Punguza ushabibi. Nani anajua unauza pampas wewe.

Lowassa na mke wake walikuwa wanatoa si chini ya millioni hamsini kuanzia 2011 hadi 2015. Ndo maana watu hawaridhiki na kamsaada kake kwa sasa.

Ni kama anawakejeli tu.
 
Nani kakuambia Lowassa hatoi michango makanisani? Nenda Dayosisi ya Kaskazini kati ukaulize michango aliyoitoa hivi karibuni.

ACHA KUPAYUKA KAMA HUJUI YANAYOENDELEA.
 
Nani kakuambia Lowassa hatoi michango makanisani? Nenda Dayosisi ya Kaskazini kati ukaulize michango aliyoitoa hivi karibuni.

ACHA KUPAYUKA KAMA HUJUI YANAYOENDELEA.

na wewe acha upopoma; mbona hapo kabla alikuwa akisikika kote makanisani na misikitini iweje leo afuatwe huko tu?
 
na wewe acha upopoma; mbona hapo kabla alikuwa akisikika kote makanisani na misikitini iweje leo afuatwe huko tu?
Hilo la kujitangaza au kutojitangaza mimi silijui labda ukamuulize yeye na ndugu zake. Nilichopinga ni kusema kwamba hatoi tena misaada,jitahidi kusoma na kuelewa.
 
Huyu mzee huwa anafanyaga mambo zake kimyakimya nyie mnazozana lakini kick zake akitokea huwa za moto sana . Viongozi wa nchi wapo tuwape ushirikiano mwacheni Edo afanye yake kkwanza.
 
Kuna ahadi za msikiti hajakamilisha
 
Leo katika taarifa ya habari ya ITV imeoneshwa M/Kiti wa BAWACHA-Taifa Halima Mdee akiwa na Mama Regina Lowassa wametoa shilingi milioni 5 katika Hospitali ya Morogoro.

Hio pesa ni ndogo sana kwa watu ambao wakati wa kuelekea kwenye uchaguzi walikuwa wakitoa mamilioni ya pesa. Mke wa Lowassa kufunga safari kutoka Monduli hadi Morogoro kwenda kutoa shilingi milioni 5 ni kuonesha mamilioni aliokuwa akiyamwaga Lowassa yameisha?.
Alitakiwa atoe shilingi ngapi kwani?
 
Kati ya mwaka 2011 hadi 2015 kulikuwa na changizo katika taifa lote, miskitini na makanisani. Katika kila Harambe ilikuwa lazima utasikia Mgeni wa heshima ni Lowassa. Akifika anasema nimechangiwa na marafiki zangu, mwisho anaweka milioni kadha.

Hali hii ilimfanya Lowassa aonekane kama "mtu wa watu". Akavuma nchi zima. Akateka mikoani na wilayani.

Mwaka huu, sijasikia tena akienda kuchangia tena.

Tunajifunza nini juu ya harakati zake?
Ina maana makanisa na miskiti haiitaji tena michango yake?
Nini tofauti ya watoa misaada wa nje na wa ndani?
Tunajifunza kuwa ni lazima tujue kutofautisha kati ya maziwa na tui la nazi,kovu na ndui,alama ya msalaba na kujumlisha,alama ya X na kuzidisha.
HAPA NI KAZI TU.
 
Nani kakuambia Lowassa hatoi michango makanisani? Nenda Dayosisi ya Kaskazini kati ukaulize michango aliyoitoa hivi karibuni.

ACHA KUPAYUKA KAMA HUJUI YANAYOENDELEA.

Zamani hatukuhitaji kwenda Dayosisi ya kaskazini kuuliza, Mwangwi wa harambee zake hata waliofukiwa mgodini kule Geita uliwafikia. Media zote ilikuwa ndio Breaking news. Alijaza Booking zote za Makanisani,Misikitini,Saccos na mpaka kwenye Vicoba akina Sumaye na Sitta wakabaki na graduation za Nursery schools ndo Jukwaa la kuongelea. Acha bana Lowassa alikuwa Lowassa kweli. Ukimgusa Lowassa utashambuliwa kuliko ukimgusa Rais wa wakati huo.
Hamis Mgeja ndie Rafiki wa kweli wa Lowassa tangu 1995 hajamsaliti na yupo nae, ilipobidi kuchagua kati ya CCM au Kikwete na Lowassa akachagua Lowassa akaacha mpaka uenyekiti wake wa Shinyanga lakin wengine walipenda Rushwa zake sio yeye.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom