Lowassa, marafiki zako hawakuchangii tena?

Lowassa, marafiki zako hawakuchangii tena?

eddy

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2007
Posts
17,080
Reaction score
12,300
Baada ya huyu bwana mkubwa kutupa manyanga kwenye uwaziri mkuu alionekana akitoa misaada huku na kule kama miss Tanzania tulipata wasiwasi na kiwango kikubwa cha fedha zilizokuwa zikitolewa ukilinganisha kwa maisha yake yote amekuwa mtumishi wa umma ndo tukaambiwa ana marafiki vibopa ndo wanaomweka mjini.

Cha kushangaza baada ya uchaguzi hatoi tena hiyo mihela ndo maana marafiki zake wamechukizwa na yeye kugombea urais au wameona maslahi waliyoyategemea kutoka kwake hayapo tena, au?

Wakati akidai kuna marafiki nyuma yake hakuwahi kuwataja hata siku moja lakini kuna minong'ono kuwa kati ya washirika wake ni majizi wapiga dili na watu wamjini, mfano kuna tetesi kuwa mtu wake wa karibu anahusishwa na upigaji hela katika hazina yetu wakati akiwa kigogo katika benki moja ya kizungu hivyo kuonyesha wazi kuwa huyu mtu alikuwa na nia ovu na taifa letu.
 
Unataka akusaidie nini? muombe ndio utajua
 
Mwenzako kesha jipanga ana miradi na ma business, siasa ilikuwa nyiongeza katika maisha. na ndoto zake zilikuwa sahihi. lakini mchezo wa rafu nyng za JK na CCM yake. lakini hana mashaka na JPM anavyo tusua kwake. tusua baba.
 
Leo katika taarifa ya habari ya ITV imeoneshwa M/Kiti wa BAWACHA-Taifa Halima Mdee akiwa na Mama Regina Lowassa wametoa shilingi milioni 5 katika Hospitali ya Morogoro.

Hio pesa ni ndogo sana kwa watu ambao wakati wa kuelekea kwenye uchaguzi walikuwa wakitoa mamilioni ya pesa.

Mke wa Lowassa kufunga safari kutoka Monduli hadi Morogoro kwenda kutoa shilingi milioni 5 ni kuonesha mamilioni aliokuwa akiyamwaga Lowassa yameisha?.
 
Bora ziishe zawizi
Pia zilileta shida mtaani
Hatulali NA Hawa Wanywa Viroba
 
Leo katika taarifa ya habari ya ITV imeoneshwa M/Kiti wa BAWACHA-Taifa Halima Mdee akiwa na Mama Regina Lowassa wametoa shilingi milioni 5 katika Hospitali ya Morogoro.

Hio pesa ni ndogo sana kwa watu ambao wakati wa kuelekea kwenye uchaguzi walikuwa wakitoa mamilioni ya pesa. Mke wa Lowassa kufunga safari kutoka Monduli hadi Morogoro kwenda kutoa shilingi milioni 5 ni kuonesha mamilioni aliokuwa akiyamwaga Lowassa yameisha?.
hata mie nimestuka sana genge lote lile tena likiwa na mama lowasa kubebelea pampasi za mil tano kweli?
 
Hajatoa milioni tano, ametoa msaada Wa vifaa vyenye thamani ya m5. Sasa si unajua utapeli Wa Ku over value, inawezekana pumpus za laki tano zikawa valued to milioni tano
 
nyie kina na nihihii mmetoa bei gani tujuze kazi umbeya tu unawaweka mjini hapa jitu zima eti milioni tano ndogo wewe unayo
 
Mtoa mada hivi milioni unajua ina sifuri ngapi baada ya namba tano..!!? Huenda tunaongea na mtu ambae hajui hata kuiandika achilia mbali kuishika..!! Acheni dharau kwa watu wanaojitolea kusaidia wengine. Kuna watu wanasema amepeleka pampas,pampas za milioni 5 hapo morogoro si angekusanya mtaa mzima!! Hakuna mfanyabiashara mwenye pampas za milioni 5 morogoro. Me nna duka la pampas tupu tandika,lkn mtaji haufiki milioni 5 na duka limejaa..!!! Mtu hujawahi kushika hata laki 3 unadharau milioni 5???
 
Lowassa bado anawaumiza vichwa hawa magamba akifanya jambo moja lina watikisa wote. Huyu mzee bado ni asset ya kuwaangusha hawa magamba. Hayupo madarakani lakini wiki haiishii bila kuona thread inayomhusu
sio wiki ni.kila baada ya siku 2
lumumba akukaliki wala akulaliki na mpaka sasa wameshaanza kutimuama kisa lowassa
 
Kati ya mwaka 2011 hadi 2015 kulikuwa na changizo katika taifa lote, miskitini na makanisani. Katika kila Harambe ilikuwa lazima utasikia Mgeni wa heshima ni Lowassa. Akifika anasema nimechangiwa na marafiki zangu, mwisho anaweka milioni kadha.

Hali hii ilimfanya Lowassa aonekane kama "mtu wa watu". Akavuma nchi zima. Akateka mikoani na wilayani.

Mwaka huu, sijasikia tena akienda kuchangia tena.

Tunajifunza nini juu ya harakati zake?
Ina maana makanisa na miskiti haiitaji tena michango yake?
Nini tofauti ya watoa misaada wa nje na wa ndani?
 
Kati ya mwaka 2011 hadi 2015 kulikuwa na changizo katika taifa lote, miskitini na makanisani. Katika kila Harambe ilikuwa lazima utasikia Mgeni wa heshima ni Lowassa. Akifika anasema nimechangiwa na marafiki zangu, mwisho anaweka milioni kadha.

Hali hii ilimfanya Lowassa aonekane kama "mtu wa watu". Akavuma nchi zima. Akateka mikoani na wilayani.

Mwaka huu, sijasikia tena akienda kuchangia tena.

Tunajifunza nini juu ya harakati zake?
Ina maana makanisa na miskiti haiitaji tena michango yake?
Nini tofauti ya watoa misaada wa nje na wa ndani?
Mimi sina cha kujifunza kwani kama ni kuwafahamu wanasiasa basi nina u-profesa (sio kama wa Kikwete lakini). Mwanasiasa wa kiafrika anaji-behave kulingana na mazingira aliyopo na upepo unavyovuma. Akiona upepo unaovuma ni ''safari za nje kwa wingi'' basi atatetea kuwa zina tija na kusifia kabisa. Akiona upepo unaovuma ni ''kukataza safari za nje'' basi atasifu na kusema kusafiri nje ni uzezeta. Hivyo kwa Lowassa wala sishangai kwani hakuona umuhimu wa tume huru ya uchaguzi wala wizi wa kura alipokuwa CCM lakini mara baada ya kutoka macho yakafumbuka.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom