Lowassa kuongea na Wananchi 14/05/2015 kupitia Clouds FM

Lowassa kuongea na Wananchi 14/05/2015 kupitia Clouds FM

CCM patachimbika mwaka huu! yetu macho,pigeni sarakasi zote mnazojua, tarehe 25october tuwapige chini.
 
Ataongea na wananchi kama nani? asifikirie kilia mtanzania anatumia tumbo kufanya maamuzi.
 
Hata atumie JIK hawezi kufanikiwa kuondoa japo ukurutu wa juu kwenye uchafu wake.
Mimi naona wengi mnaomuona Lowassa kama mchafu, fisadi, mwizi na mengine mengi machafu mnayompamba, hamna ushahidi wa wazi kuonesha hayo mnayodai kwani wengi mmekuwa bendera fuata upepo. Hilo suala la Richmond alishasema lilikuwa limeamuliwa na baraza la mawaziri chini ya rais na ndio maana alisema kila alichokifanya alikuwa anamjulisha rais. Mwenye Richmond alikuja hapa akaongea na waandishi wa habari kisha akaenda mpaka ikulu. Ulishasikia kaenda kwa Lowassa. Mnamtuhumu kwa ushahidi wa kimazingira tu. Ingekuwa leo naye angesafishwa kama wale wengine sema wakati wake fitna zilikuwa nyingi. Kuhusu yeye kuwa na pesa nyingi kwa maana ya kuwa tajiri, hilo sio kosa ili mradi hajamwibia mtu. Mbona matajiri wako wengi tu hapa nchini kwanini EL? Mtafika mahali mtaaibika pale kweli itakapo dhihili kwani ukweli huja mwishoni!
 
Hayo maswali kama wanauliza wale watangazaji wa mawingu hakuna kipindi hapo
 
Siku hiyo tasingizia naharisha ili nisiende kazini kumsikiliza raisi wa awamu ya 5 na ikiwezekana abadili katiba akae miaka 20 kabisa madarakani.
 
Ataingia mtini Mark my word!!!! labda aonge Bashee
 
"We will cross the brigde when we reach there" Kwa kiswahili tungesemaje?
Tutuvuka daraja tukilifikia...Ma Presdent is lowasa siwezi kuongozwa na njozi na mzee wa watabiri a.k.a joka la mdmu......iwe ni kupitia ccm au kuptia familia yake yeye ndye rais wangu mtarajiwa na nitahakikisha mimi binafsi namtaftia wapga kura 1000 moja kwa Jina la Yesu na Mungu anipe uwezo
 
baada ya kusoma uchambuzi wa Mtatiro ndo ameona IPO haja ya kuongea????....

Hapana ameshitushwa kuona wezi wa escrow ambao pia ni washindani wake ktk kuwania viatu vya babaliz wanasafishwa na ikulu huku yeye akiachwa afe kivyake. Nahisi atakuwa ameamua kujisafisha na kutangaza niya rasmi. Tar 16 May pia atakuwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha kuongea na wananchi.
 
Anaongea na wananchi kama nani?

Ina maana humjui Lowasa? Yeye ni mtu aliejipatia Umaarufu mkubwa kwa utendaji wake uliotukuka , akiwa ni mtu anaetegemewa na wananchi wengi zaidi katika nafasi ya Urais kuliko mtu mwingine Yeyote.
 
Tutuvuka daraja tukilifikia...Ma Presdent is lowasa siwezi kuongozwa na njozi na mzee wa watabiri a.k.a joka la mdmu......iwe ni kupitia ccm au kuptia familia yake yeye ndye rais wangu
Asipopita utafanyaje? Utahama nchi?
 
jamaa anazungumzwa kila pembe ya nchi ngoja tusubiri labda anahamia ACT ya Zitto
 
Back
Top Bottom