Lowassa kukaangwa kama Yesu!

Lowassa kukaangwa kama Yesu!

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
25,956
Reaction score
25,345
Kuna taarifa kwamba CCM wana mpango wa kurefusha kifungo cha makada waliofungiwa kwa mwaka mmoja zaidi mpaka uchaguzi utakapokwisha lengo kubwa hasa likiwa kumkaanga Lowasa.

Kada maarufu wa CCM ambaye hakutaka kutaja jina lake anayefanya kazi Makao Makuu ya CCM, Dodoma alisema kuwa mpango huo wa kumuangamiza Lowasa umekamilika na hakuna mtu anayeweza kuupindua.

"Si unajua kwamba amehukumiwa pamoja na makada wenzake...hivyo njia nzuri ni kuwafungia wote ili kupunguza malalamiko kutoka kwa wafuasi wake (Lowasa) na kugawanyika kwa chama. Unajua huyu mtu ana wafuasi wengi sana hivyo tukimfungia ovyo anaweza kukigawa chama chetu". Alisema.

KAMA YESU?
Wakristo mnakumbuka wakati mtoto Yesu alipozaliwa, mafarisayo waliwaua watoto wote wa kiume lakini target yao hasa ilikuwa ni kumuua Yesu. Naona CCM wameamua kukopa mbinu hiyo kwa kum-target Lowasa. Hili ni jambo la ajabu sana.

MAONI YANGU
CCM mnajaribu kuliziba jua kwa kutumia ungo lakini mjiandae vizuri kwa madhara yatakayotokea. Lowasa hazuiliki.

:israel:
 
CCM jiandaeni kumkubali Lowasa...huyu ni mwali wenu, mnapaswa kumkubali jinsi alivyo na hakuna jinsi ya kumuepuka. Kwanini mnawekea mikingamo ya ovyo ovyo? Nyota ya mtu iking'ara hakuna awezaye kuizima isipokuwa Mungu tu. Kwani CCM mmekuwa Mungu hadi mumzibie njia Laigwanan Lowasa? Acheni hizo figisufigisu zenu.
 
Kuna taarifa kwamba CCM wana mpango wa kurefusha kifungo cha makada waliofungiwa kwa mwaka mmoja zaidi mpaka uchaguzi utakapokwisha lengo kubwa hasa likiwa kumkaanga Lowasa.

Kada maarufu wa CCM ambaye hakutaka kutaja jina lake anayefanya kazi Makao Makuu ya CCM, Dodoma alisema kuwa mpango huo wa kumuangamiza Lowasa umekamilika na hakuna mtu anayeweza kuupindua.

"Si unajua kwamba amehukumiwa pamoja na makada wenzake...hivyo njia nzuri ni kuwafungia wote ili kupunguza malalamiko kutoka kwa wafuasi wake (Lowasa) na kugawanyika kwa chama. Unajua huyu mtu ana wafuasi wengi sana hivyo tukimfungia ovyo anaweza kukigawa chama chetu". Alisema.

KAMA YESU?
Wakristo mnakumbuka wakati mtoto Yesu alipozaliwa, mafarisayo waliwaua watoto wote wa kiume lakini target yao hasa ilikuwa ni kumuua Yesu. Naona CCM wameamua kukopa mbinu hiyo kwa kum-target Lowasa. Hili ni jambo la ajabu sana.

MAONI YANGU
CCM mnajaribu kuliziba jua kwa kutumia ungo lakini mjiandae vizuri kwa madhara yatakayotokea. Lowasa hazuiliki.

:israel:
Lowasa amekaangwa kama shetani alivyokaangwaa
Mda mfupi baada ya kuasi alitupwa nje yeye Shetani na Malaika zake
Hivyo tutegemee watu wote ndani ya CCM aambao walitegemea Lowasa kuwa mgombea wao wa urais na wao walitegemea kugombea ubunge na udiwani basi ni lzima nao watupwe !!
Kumbuka hapa kuna mtego , kama watu hao watajitokeza kupinga maagizo hayo basi nao wataonekana wanapinga maagizo halali ya CCM na watakosa sifa za kugombea nafasi ndani ya CCM kwa kuonekana wasaliti

Hapo ndo linatimia neno kuwa halitasalia jiwe juu ya jiwe!!
Lowasa ni mwizi na anafedha za wizi ambazo amekuwa anahonga makanisa na wachungaji !!
Mungu hanunuliwi !!
 
Huwe kufananisha YESU na yuda aliyemsaliti YESU. lowasa kwa watz ni km yuda coz aliwasaliti kwa kushinikiza na kuunda kampuni feki akishirikiana na mapacha wake kikwete na rostamu......
ACHENI KUMDHALILISHA MUNGU/YESU kwa kutolea mifano ya majambazi sugu na fisadi papa km lowasa
 
Lowasa amekaangwa kama shetani alivyokaangwaa
Mda mfupi baada ya kuasi alitupwa nje yeye Shetani na Malaika zake
Hivyo tutegemee watu wote ndani ya CCM aambao walitegemea Lowasa kuwa mgombea wao wa urais na wao walitegemea kugombea ubunge na udiwani basi ni lzima nao watupwe !!
Kumbuka hapa kuna mtego , kama watu hao watajitokeza kupinga maagizo hayo basi nao wataonekana wanapinga maagizo halali ya CCM na watakosa sifa za kugombea nafasi ndani ya CCM kwa kuonekana wasaliti

Hapo ndo linatimia neno kuwa halitasalia jiwe juu ya jiwe!!
Lowasa ni mwizi na anafedha za wizi ambazo amekuwa anahonga makanisa na wachungaji !!
Mungu hanunuliwi !!

mkuu, ngoja tuwasubiri wenyewe waje kujitutumia hapa.

CC: FaizaFoxy, Ritz, laki si pesa Simiyu Yetu, MwanaDiwani MUSSA ALLAN, Tata, TataMadiba, thatha, Agogwe, Nyani Ngabu, gsu, Lizaboni KATIBA MPYA, & the rest of team lumumba B7.
 
Last edited by a moderator:
Naunga mkono hoja
naisingependa kumwita mtoq uzi sole ya kiatu ambayo hutumika kukanyaga popote na haiwezi kujiongoza yenyewe!
sielewi wapi alipomwona Yesu anakaangwa! sielewi alipoona Lowasa anaandaliwa tayari kukaangwa, sioni uhusiano kati ya ccm na Yesu. tumia akili na si tope ndugu.
 
sasa kuna kitu sijaelewa ina maana wana huo mpango wa kurefusha kifungo hadi lini?au ndio hakutakuwa na mgombea kabisa toka upande huo?sijaelewa elewa kabisa hizi fununu
 
CCM jiandaeni kumkubali Lowasa...huyu ni mwali wenu, mnapaswa kumkubali jinsi alivyo na hakuna jinsi ya kumuepuka. Kwanini mnawekea mikingamo ya ovyo ovyo? Nyota ya mtu iking'ara hakuna awezaye kuizima isipokuwa Mungu tu. Kwani CCM mmekuwa Mungu hadi mumzibie njia Laigwanan Lowasa? Acheni hizo figisufigisu zenu.

Ndiyo amekutuma kuja kumsemea ujinga huu kamwambie hatutaki viongozi mafisadi.
 
Ni upuuzi kumfananisha fisadi papa na Mtumishi wa Mungu

kama hujui kitu ni bora ukae kimya. CCM wanataka kuwakaanga makada wote waliofungiwa kwa nia ovu ya kumlenga Lowasa. mafarisayo walipanga kuwaua watoto wote wa kiume waliozaliwa katika Bethelehem ya Uyahudi lakini lengo lao kubwa lilikuwa ni kumuua Yesu. huoni huo mfanano? mpuuzi mkubwa weye!
 
Ndiyo amekutuma kuja kumsemea ujinga huu kamwambie hatutaki viongozi mafisadi.
Bora tuongozwe na Fisadi aliyetuibia na akawekeza hapa kuliko kuwa na viongozi mafisadi waliotuibia na hatujui wamewekeza wapi!
 
Back
Top Bottom