Lowassa hasafishiki

Lowassa hasafishiki

Mimi wala sina tatizo na Lowassa wala Makufuli, ila wasiwasi wangu hawa viongozi na wabunge wa upinzani jinsi walivyokuwa wanakomalia na kutuaminisha kwamba EL ni fisadi papa kisha leo hii kwa statement moja tu ya Lowassa eti yeye alisaini mkataba wa Richmond kwasababu alipewa go ahead from mamlaka ya juu ndio wao wote viongozi wa upinzani wanakubali kwamba EL ni msafi.
Sasa kwanini walikuwa wanatuaminisha hivi muda wote kwamba EL ni Fisadi kisha ghafla siyo fisadi. Yaani huwa naumia kuona hawa wanasiasa uchwara wanatugeuzi wananchi na kutufanya kama chapati. Hivi kama lengo ni kuitoa CCM madarakani kwanini wasingetumia sera nyingine za maana na za uhakika kuliko kusema mtu Fisadi kisha mara siyo fisadi tena.
Haya mambo yanazidi kutufanya watu tuchukie siasa manake wanasiasa wengi ni matapeli wa kutupa, wao wanaona sifa pale bungeni kusema ujinga wao usiokuwa na maana yoyote kumbe mwisho wa siku ni uongo mtupu.
 
Mkuu
Tangu rais ameingia madarakani hadi leo hii
Ulishawahi kumsikia Rais akisema kwa kinywa chake kuwa yeye na Lowasa ni marafiki?

Tafakali

Siku anamuapisha lowasa kua waziri mkuu alisema amemchagua kwa sababu ni rafiki yake.
 
Baada ya kupata maoni kuwa RICHMOND ina matatizo Edward Ngoyai Lowasa aliitisha kikao cha makatibu kwa ajili ya kujadili suala hilo na alishauri kama wanaafiki kuwa magumashi wavunje mkataba, Lakini amri ilitoka kutoka mamlaka ya juu kuagiza mchakato uendelee. Na ukaendelea.

Taarifa ya Dr. Harrison Mwakyembe pamoja na mambo mengine ilipendekeza kufutwa mikataba yote inayonyonya TANESCO na mlipa kodi lakini azimio hilo halikutekelezwa na matokeo yake ndio ESCROW ACCOUNT TEGETA.

Akiwasilisha ripoti kwa mbwembwe Dr. Harrison Mwakyembe alieleza kwamba wangeendelea kuchimbua zaidi kutokana na taarifa walizopata serikali ya JK ingeanguka kwa sababu muhusika mkuu ni IKULU.

Kudhiirisha anguko la mtu dhalimu halionekani machoni pake, kwa kuwa mboni za macho zake zimevikwa vazi la kiburi, sasa tunakuja kukutana na ESCROW ACCOUNT TEGETA. Mungu alitaka kuwaumbua kweupe madhalimu, kuwaumbua kweupe wadhulumaji.
Maazimio yote ya bunge kuhusu ESCROW ACCOUNT TEGETA mkulu JK aliyaongea kwa tabasamu na kuchekacheka tu akikwepa maazimio mahsusi kwa mara ya pili kufuta mikataba, kutaifisha mitambo kwa madai yasiyo na mashiko kama ya Prof.Lipumba alivyojizulu uongozi CUF.

Dr.Magufuli amewaahidi wana CCM wenzake hato waangusha, ina maana mikataba ya kinyonyaji sekta ya umeme itaendelea na watanzania tutaendelea kununua umeme kwa gharama kubwa. Mwaka 2008 kiasi cha tsh.10,000 nilipata UNIT 72 leo hii natumia tsh.30,000 kupata unit 64

Kuna unafuu tangu LOWASA aondolewe Uwaziri Mkuu? Huyo Mwakyembe aliyeandika kitabu akieleza serikali ya shirikisho ndio muafaka na kupitia hicho alifanikiwa kupata udaktari alibinua mdomo kuwaeleza wenzake katika bunge la katiba?

Samwel Sitta aliyesimamia vizuri bunge akiwa spika awamu ya kwanza JK, akijipambanua kusimamia haki, usawa na kutokomeza ufisadi. Si ndio huyo huyo kashiriki kufuta vifungu kadhaa Rasimu ya Warioba kuzuia kukimbiza pesa za umma akaunti za uswisi, kufuta tunu za taifa na kuruhusu zawadi za kitaifa kuwa za watawala?
 
Dr.Wilbroad Slaa alikatwa jina lake ngazi ya ubunge CCM mwaka 1995, baada ya kushauriwa na wafuasi wake alikubali kuhamia CHADEMA. Hakukufanyika kikao chochote kumjadili kabla ya kumpokea isipokuwa alipewa uanachama, na fursa ya kugombea ubunge kupitia CHADEMA na baadae kuja kupatiwa uongozi wa juu ndani ya chama na kuweza kukijenga chama kwa kiwango kikubwa sana.

Hilo linawezekana pia kwa Lowasa, watu waCCM kama wanafikiri kumsafisha Lowasa ni kazi basi kuogesha CCM HAIWEZEKANI.
 
Ndio maana watu makini kama dr. Slaa wapo pembeni wanawaacha kina mbowe waje kuaibika october. Uliona wapi kaniki yenye langi nyeupe

Maajabu ya mwaka leo hii Dk.Slaa amekuwa kipenzi cha wanaccm kisa hataki kushirikiana na kina Lowasa na hata uzinzi waliokuwa wanampakazia haupo tena ama kweli siasa mchezo mchafu
 
Kama ni ufisadi ndani ya nchi hii ni wengi sana hawtukanwi kwa kuwa hawajaondoka ktk system wakithubutu wataambiwa yote.Kama ni Dk Slaa kutshirikiana na Lowassa hata upande wa ccm wapo viongozi hawaonekani kumsapoti Magufuli zaidi ya mh.Kikwete
 
Kama ni ufisadi ndani ya nchi hii ni wengi sana hawtukanwi kwa kuwa hawajaondoka ktk system wakithubutu wataambiwa yote.Kama ni Dk Slaa kutshirikiana na Lowassa hata upande wa ccm wapo viongozi hawaonekani kumsapoti Magufuli zaidi ya mh.Kikwete

Nape alisema lowasa ana kashfa nyingi na nyingine ni za jinai ambazo Takukuru wanazitayarishia mashtaka ya jinai. Kama wanao ushahidi wanasibiri nini? Wasije wakatutega dakika za mwisho Ukawa tukose mgombea.
 
Onajua ccm tatizo lao ni kukariri saiv freedom is coming tomorrow
 
Lowasa kachoka hawezi kushinda popote pale kuanzia mwili mpaka akili anatawaliwa na ufisadi wa wazi kabisa mzee mwizi sana.

chief, huyu bwana anaweza kuwa "mwizi sana" kama ulivyopenda kumwita...granted.

lakini kinachotutatanisha wengi wetu hadi sasa....

1. je ni kwa nini huyu "mhalifu" hayuko Segerea/Ukonga kama wale makada wengine akina Mramba?

2. au basi walau tusikie kuwa mali zake "za wizi" zimetaifishwa....mbona hapa napo anaachwa atambe mtaani na "mali zetu" huyu "jizi la kutupwa"??

3. sisi wengine tusio mashabiki wake huyu "jizi" tunangojea kwa hamu sana kanusho au majibu kutoka Ikulu kuhusu tuhuma nzito sana alizotoa huyu "jizi" dhidi ya bosi wake kuwa eti yeye (mkulu) ndiye haswa Mr Richmond.
 
cDM wanastahili kuaminika kwa wasiofikiria vizuri ..mtu akikwambia kitu cha kijinga na wewe ukakubali basi wewe ndo unakuwa mjinga zaidi, haiwezekani jana wamezunguka nchi nzima wakatwambia fulani mchafu kama kinyesi alafu leo wanarudi wanamsema eti ni msafi ..haiwezekani, kuna tatizo mahala hapa, kama si waliotaangaza ndo wenye tatizo basi aliyeyangazwa ana tatizo ama sisi tuliotangaziwa tunatakuwa na tatizo ..haya mambo ni makubwa na kwa watu kama sisi hatuwezi kuyacha yakapita bila kuquestion, hapa kuna mchawi na lazima tumbaini ikiwa angari mapema la sivyo huu ni utahira wa kutupwa
 
lile Dudumizi la richmond bado lipo ndani ya ccm .lowasa aliondoka 2008 tukajua sasa serikali ya ccm safi ghafla.Dudumizi la richmond likaamka likajibadili na kujiita Tegeta escrow limetutafuna mpaka utumbo limeshiba nasasa limelala tafakari likiamka litajitaa nani?
 
lile Dudumizi la richmond bado lipo ndani ya ccm .lowasa aliondoka 2008 tukajua sasa serikali ya ccm safi ghafla.Dudumizi la richmond likaamka likajibadili na kujiita Tegeta escrow limetutafuna mpaka utumbo limeshiba nasasa limelala tafakari likiamka litajitaa nani?

Hao unaowataka wameanza kununuana hata kabla hawajafika Ikulu, wakifika Ikulu si ndo watakuwa fundi mchundo? Lakini pia ni bora tukawa na wale wenye kujua kulinda amani kuliko wakutuletea vita asubuhi
 
Safari hii kila Mtu kawa mchambuzi wa siasa
 
Kama ni ufisadi ndani ya nchi hii ni wengi sana hawtukanwi kwa kuwa hawajaondoka ktk system wakithubutu wataambiwa yote.Kama ni Dk Slaa kutshirikiana na Lowassa hata upande wa ccm wapo viongozi hawaonekani kumsapoti Magufuli zaidi ya mh.Kikwete

Subiri mkapige kura ndo mtajua mioyo yetu watanzania imebeba nini
 
Back
Top Bottom