singidadodoma
JF-Expert Member
- Nov 11, 2013
- 4,394
- 1,538
Pamoja na maigizo yanayoendelea kati ya Ukawa na mgombea wao Lowassa, Nawausia Ukawa kuwa wanajitafutia aibu kwakuwa mgombea wao hakarabatiki na wakilazimisha mtafedheheka wote kwani watanzania sio mandondo kama wanavyofikiria. Ndiyo maana aliingia kirahisi mno kwenye tope la Richmond linalomtafuna kabisa katika medani za siasa kila siku.
Sitaki kurudia hoja kuu zinazothibitisha kwamba Lowassa hakuonewa. Hii ni kwa sababu, Lowassa mwenyewe anafahamu fika hakuonewa katika suala zima la Richmond anajifariji kwa kutuonyesha maigizo.
Lowassa aliwahi kusema, "hakufanya kosa hata moja kwenye suala la Richmond na kuwa hata tukimwamsha leo usingizini atarudia maamuzi yaleyale kwa namna ile ile. cha ajabu leo anaikana hiyo kauli ya na kusema alionewa.
Pamoja Viongozi wa CHADEMA kumtaja kwamba yeye ni FISADI kwenye "List of shame" na leo wanajaribu kumsafisha kwa udi na uvumba lakini watanzania wanakumbuka kauli ya mwalimu Nyerere aliomtakia Lowasa baada ya kuonana na Nelson Mandela kwenye Ubalozi wa Afrika Kusini mjini Dar es Salaam, "wewe tumekutoa juzi tu toka Umoja wa Vijana. Ghafla una mali kupindukia, umezitoa wapi?
Wewe ni mchafu, ondoa jina lako kwenye wagombea" ni ya kweli? Je, anaweza kuwaeleza Watanzania mali alizochuma katika kipindi kifupi cha uwaziri mkuu na jinsi alivyozipata?
Sitaki kurudia hoja kuu zinazothibitisha kwamba Lowassa hakuonewa. Hii ni kwa sababu, Lowassa mwenyewe anafahamu fika hakuonewa katika suala zima la Richmond anajifariji kwa kutuonyesha maigizo.
Lowassa aliwahi kusema, "hakufanya kosa hata moja kwenye suala la Richmond na kuwa hata tukimwamsha leo usingizini atarudia maamuzi yaleyale kwa namna ile ile. cha ajabu leo anaikana hiyo kauli ya na kusema alionewa.
Pamoja Viongozi wa CHADEMA kumtaja kwamba yeye ni FISADI kwenye "List of shame" na leo wanajaribu kumsafisha kwa udi na uvumba lakini watanzania wanakumbuka kauli ya mwalimu Nyerere aliomtakia Lowasa baada ya kuonana na Nelson Mandela kwenye Ubalozi wa Afrika Kusini mjini Dar es Salaam, "wewe tumekutoa juzi tu toka Umoja wa Vijana. Ghafla una mali kupindukia, umezitoa wapi?
Wewe ni mchafu, ondoa jina lako kwenye wagombea" ni ya kweli? Je, anaweza kuwaeleza Watanzania mali alizochuma katika kipindi kifupi cha uwaziri mkuu na jinsi alivyozipata?