Wewe ni mwongo wa kutupwa,
Kwanza hata hujui Askofu aliyewekwa wakfu ni nani na ni wa Dayosisi ipi (na kwa hakika inavyoonekana huelewi chochote kuhusu Ukristo,Uaskofu,KKKT na masuala ya wakfu maana hueleweki ulichokiandika hapa)
Pili,nimehudhuria Ibada ya kuwekwa wakfu Baba Askofu Dr.Frederick Onaeli Shoo wa Dayosisi ya Kaskazini,ibada iliyofanyika leo katika Kanisa Kuu la KKKT Mjini Moshi,ukweli ni kwamba hakuna kiongozi yeyote wa kisiasa aliyepewa nafasi ya kuzungumza zaidi ya Mh.George Huruma Mkuchika aliyefika kumwakilisha Mh.Rais Kikwete.
Nasisitiza hivyo,hakuna kiongozi aliyepewa nafasi ya kusalimia,si Lowassa tu,walikuwepo viongozi wengi na watu maarufu wengi -mfano, Mh.Sumaye,Lazaro Nyalandu,Mh.Mbowe,Mh.Mbatia,Mh.Lema,Mh.Mengi,Felix Mosha nk....lakini ukweli ndo huo hakuna yeyote kati yao aliyepata nafasi ya kuzungumza.
Mods please futilia mbali uzi huu na ingefaa mleta uzi apigwe ban ya mwezi mzima ili awe na discipline; uzushi wa namna hii hauna afya kwa jukwaa hata kidogo.