Lowassa apigwa shinikizo kali


Ni ndoto kwa watanzania kumchagua Lowasa kuwa rais wa nchi yao. Hao watu aliowapa pesa wampigie debe mara kwa vijana au boda boda ni wachache sana hawawakilishi watanzania hata chembe. Akitaka kujimaliza yeye pamoja na upinzani ajaribu kuingia upinzani. Mrema alipata wafuasi wakati ule kwa sababu kuna watu ambao moyoni mwao (labda kiusahihi au kimakosa) waliamini Mrema ni mchapa kazi mwenye nia nzuri na nchi hii. Ndio maana japo hakuondoka na viongozi wa serikali au CCM alipata sapoti ya hao wananchi walioamini uwezo wake. Ni tofauti sana na Lowasa. Yeye Lowasa anaondoka na sapoti ya viongozi walliopokea pesa kutoka kwake ili wamsapoti, haondoki na wananchi. Badala yake wananchi wanajua kuwa Lowasa ni fisadi asiyeitakia mema nchi hii. Sasa akiruhusu CCM nayo iingie katika kumtangaza kuwa ni fisadi ndio maana akaenguliwa basi itakuwa mwisho mbaya sana kwa Lowasa. Abaki tu CCM watamheshimu hawataanika uozo wake uliosababisha aenguliwe.
 

Mkuu unajua hata CCM wenyewe walishindwa kumwondoa kwa sababu za ufisadi, kwa kuwa ni vigumu kwa fisadi kumnyooshea kidole fisadi mwenzie. Inawezekana sisi tunadhani kuwa jina lake lilikatwa kwa sababu ya ufisadi...be sure hiyo si sababu. Kuna sababu nyingine tu.

Mara akadhaa Lowassa amekuwa akisema mwenye ushahidi kuwa yeye fisadi ajitokeze kusema hadharani, nani aamejitokeza hado leo? hakuna.

Ila sasa omba yeye asitaje mafisadi. kuingia kwake oppostion ni jinamizi kubwa kwa CCM.

Kumbuka mwalimu alivyosema, shoka lenye mpini wa mti linakata miti kuliko lenye mpini wa chuma. Do not under estimate this.

Pia unatakiwa kukumbuka kuwa electorate imebadilika sana, very possible that anything can happen.
 
Atoe maamuzi sasa hizi habari za uongo kila siku zipungue.
 
lowasa kwa jinsi alivyodhalilishwa dodoma ana option mbili tu. nazo ni kuachana na siasa na ccm pia au kutoka ccm na kujiunga na upande mwingine. nje ya hapo lowasa amekwisha.
Kuachana na siasa ndio option ya muhimu sana kwake kwa sasa.
 
Ushauri wako ungekuwa wa maana kama ungeondoa maneno ya serikali na kuweka CCM inaelekea uelewa wako bado ni mdogo sana juu ya uendeshaji wa nchi. Serikali itakuwepo tu hata ccm ikifa.
Mkuu kwani tunaposema Serikali ya Chama tawala tuna maana gani?
 
Rais anayekuja atakuwa amewatendea haki watanzania akiliunganisha hili fisadi na kina Mramba huko jela.

watanzania tunapenda kutawaliwa na mafisadi.ndo maana mpaka leo ccm inatawala
 

Wewe kwa vyovyote vile ni lazima fisadi mwenza, ama ulikuwa unaonja hela za hili fisadi lililosababishia taifa matatizo ya huduma ya umeme, ama ni mjinga, au mpumbavu, au ---- ama lofa sijui nikuiteje lakini inaelekea huna uwezo wa kufikiri na ni watu kama nyie mnaoendelea kushabikia ujinga mpaka kabirini. Kwahiyo unaona lowassa ni bora kuliko Magufuli na yeye na Slaa ndio wana sifa zinazoendana? Kwanini hao Chadema mnaowakimbilia ndio walikuwa mstari wa mbele kushinikiza atolewe madarakani wakimchafua ni fisadi kila kona. Huwa naudhika sana ninapoona watu wajinga wajinga wanaropoka humu. Ondoa uchafu wako kamuimbie lowassa wako ngonjera zako hizi.
 

ndani ya ccm hakuna asiye fisadi kamwe. wanatofautiana tu...
 

Ndoto za abunuwasi, jipe moyo, endelea kutapatapa kwa maana wewe ni dhahiri kabisa mfa maji. Na ile adha ya taifa kukosa umeme haikukuuma kabisa. Kuna mtu aliyekuwa anajidai mbabe kuliko lowassa wako? Kama kuchafuka alitaka mwenyewe mbona wako wengi tu wasafi mmojawapo ndio raisi wako ajae. Shimo la mavi aliingia mwenyewe usisingizie wanaolinda maslahi ya chama. Kama ana la kusema aje aseme mwenyewe kukaa kimya hakumsaidii kitu na ndio story kuhusu alivyoumiza taifa zitazidi kusambaa na kuaminika. Kuwa mzalendo acha ushabiki wa kijinga. Sikiliza sera za wagombea walioko mbele yako sio ukae kulilia mtu aliyeshindwa kazi ya chini mnataka achukue mzigo mkubwa zaidi ataweza vipi?
 
Watanzania tunapata tabu yote hii kwa sababu ya TB Joshua! Ule utabiri wake na uhakikisho kwamba EL atakuwa Rais basi imekuwa sheeeedah
 
ndani ya ccm hakuna asiye fisadi kamwe. wanatofautiana tu...

Hakuna mwanasiasa msafi, si CCM wala upinzani, wote wana ajenda either za chama ama za kwao wenyewe na ndo maana ukawa mpaka leo wanahaha kupata mgombea alafu mnataka kuwaachia nchi, watagawana kama ubwabwa kwenye sinia. Mwalimu alisema and i quote "Rushwa ipo kila mahali duniani, ila inatofautiana, bara la Asia ikitoka tender ya barabara atapewa mtoto wa raisi, na Afrika pia atapewa mtoto wa raisi, tofauti yake ni kwamba, Asia barabara itajengwa" sisi huo umeme wa richmond ulivyotutesa na hela wakala na umeme haukuonekana hata chembe.
 
lowasa kwa jinsi alivyodhalilishwa dodoma ana option mbili tu. nazo ni kuachana na siasa na ccm pia au kutoka ccm na kujiunga na upande mwingine. nje ya hapo lowasa amekwisha.
Ningekuwa mimi ningeachana na siasa na kuomba suluhu na Chama changu waridhie suluhu nirudi kijijini nikachunge ng'ombe wangu huku nikipata zile haki za Waziri Mkuu Mstaafu. Nisingetaka tena kuwachokoza kwa kuwa sikustaafu uwaziri mkuu
 

Asante, wazalendo bado tupo naamini
 

Umesema kitu kizuri sana.
 

Mkuu ushahidi kauchukue kwa Slaa kwenye list of shame.
 

Waambie hao, waache kuishi kwa hisia
 
Watanzania tunapata tabu yote hii kwa sababu ya TB Joshua! Ule utabiri wake na uhakikisho kwamba EL atakuwa Rais basi imekuwa sheeeedah
hata hivyo siku si nyingi neno lake bwana litatimia
 

Mi nahisi hilo neno lako "vision" ulikuwa unamaanisha "hallucinations" na ndio alizokuwa nazo babu yako mamvi team wapigaji mtalalamika sana mwaka huu mshajua hamli hela za wananchi kupitia fisadi wenu mkuu lazima mtanyooka tu. Hata kura upeleke wapi tingatinga kishapita. Pole sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…