Ngaramu
JF-Expert Member
- May 7, 2009
- 382
- 78
SAFARI YA MA TUMAINI
Kauli mbiu hii bado inanisumbua kwakweli. Watanzania tuna matatizo mengi yanayotukabili na tunataka yatatuliwe. Matatizo ya ayfa, uchumi, ufisadi elimu nk.
Mtu akipimwa akakutwa na HIV anashauriwa kuishi kwa matumaini. Yaani alikubali tatizo na kufuata masharti, hii ikimaanisha tatizo lake kwa sasa bado halina ufumbuzi lakini kwa kurefusha maisha huenda akaishi mpaka dawa itakapogunduliwa. Safari ya matumaini ina maana hiyo? Je, ufumbuzi wa matatizo yetu bado haujapatikana na badala yake sasa tuishi kwa matumaini? Maana ya kauli mbiu hii hebu iwekeni vizuri. Tutasafiri kwa matumaini mpaka lini? Na ni kwa nini iwe hivyo?
Kwanini EL anataka kutupeleka kwenye Safari ya MATUMAINI wakati Tz ina RASRIMALI kibao???