Lowassa amtaka Zitto kujiunga UKAWA ili mpambano uwe kati yake na Magufuli.
Mazungumzo Makali yanaendelea namna gani ya kumjumuisha Zitto.
Chanzo: Magazeti ya Leo na Jana RAIA mwema
Lowasa anajua madhara ya kuingia upinzani. Kamwe hataondoka CCM hata kama hatakuwa active kisiasa ila atabaki ndani ya CCM. Swala la Zitto naamini hata Lowassa anafahamu kuwa Zitto ni sehemu ya CCM. Kwa vyovyote vile kina Nchimbi akiwa waziri wa mambo ya ndani atakuwa amemweleza Lowasa jinsi walivyomtumia Zitto kudhoofisha upinzani hivyo hata kama Lowasa angehamia upinzani (japo haitatokea) Zitto angekuwa sumu kali kwa sababu anajua fika jinsi ambavyo yuko upinzani kisanii na kikazi kwa ajira ya CCM na serikali yake.