Mh. Edward Lowassa kabla ya kupokelewa na Chama Cha Chadema, aliwekewa sharti la kusema ukweli wote kuhusiana na tuhuma alizokua akituhumiwa.
Alifanya hivyo na kamati kuu ya Chama Cha Demokrasia, ikaridhia kumpokea, isipokua katibu mkuu Dr. Slaa ambaye haonekani katika majukumu yake mpaka sasa.
Ikumbukwe kwamba, hayo aliyoyakiri Lowasa mbele ya kamati kuu alikua akiyafanya kipindi alipokua katika utumishi wa uma.
Lowassa kama mtumishi wa uma, alikua akipokea mshahara na marupurupu yote ambayo yanatokana na kodi zetu sisi wananchi. Hivyo wananchi tunakila sababu ya kujua ni ambo gani hayo yamezungumzwa kwa kamati kuu, ambayo yamewafanya wampokee.
Kamati kuu ya chadema, si wananchi wote wa Tanzania. Na kamati kuu pekee haikua ikilipa kodi ambazo zilitosha kulipa utumishi wa bwana lowassa, hivyo kama kuna maovu aliyoyafanya, aje akiri mbele yetu wote, tuyasikie na kuyapima, ili kama tunaamua kumsamehe na kumpa kura zetu, tufanye hivyo bila kurubuniwa na wachache ambao ndio waliomsikiliza.
Bila hilo kufanyika, bwn. Lowassa atakua mgombea wa kamati kuu ya chadema na si mgombea wa wanachadema, na akiwa rais, atakua rais wa kamati kuu ya chadema.
Bw. Lowassa, tunasubiri kukusikiliza, utuambie, tuamue wenyewe.