Lowassa achanja mbuga; CHADEMA wammezea mate!

Lowassa achanja mbuga; CHADEMA wammezea mate!

HAMY-D

JF-Expert Member
Joined
Sep 18, 2011
Posts
7,146
Reaction score
3,829
Confirmed.

Nadhani hilo neno hapo juu sio geni kwako. Hivyo nina imani unajua vizuri matumizi ya neno hilo, na utaweza kulihusisha na hii habari.

Wana Ukumbi,

Katika hali ambayo imewaacha wengi midomo wazi na baadhi kubaki kukuna vichwa. Ni baada ya kugundua kuwa CHADEMA kwa sasa hali ni tete na inasemekana wamekosa kabisa mgombea atakae peperusha bendera ya chama kwa nafasi ya urais.

Lakini pia CHADEMA hao hao wameonelea sio vyema kuingia kwenye uchaguzi wakiwa hawana mtu anae kubalika na Watanzania wengi. Hivyo imewalazimu watazame vyama jirani vina nini kama ilivyo desturi kwao.

Sasa hapa kwenye nini CHADEMA wamepata kutoka vyama jirani ndio penye maajabu. Sikuwahi kutarajia CHADEMA itaweza kuibuka na jina la Lowassa kama tunu kwao kwenye kuelekea uchaguzi.

Ina maana huyu Lowassa sio yule aliyeitwa fisadi!?

Huyu Lowassa leo amebadilika nini hadi agombaniwe na vyama kugombea katika nafasi ya urais?

Au ni ukweli kwamba Lowassa alisingiziwa kuhusu ile tuhuma na sio kweli kuwa ni fisadi.

Je, kama Lowassa ni fisadi, kwanini Watanzania wawe nae bega kwa bega kwenye movement zake za kuwania urais?

Kweli maneno yametimia, "JIWE LILILO KATALIWA, LEO LIMEKUWA JIWE KUU LA PEMBENI".
 
Ndesamburo wa CHADEMA ambae ana uwezo wa kumuweka binti yake na mkwe wake kwenye viti maalum vya ubunge kupitia chadema, kaamuwa kuwachana na mgombea wa CHADEMA na kumpigia debe Lowassa.

Usifanye maskhara katika haya mambo.
 
Hiyo ndo siasa...

Shauri yenu mnaofukuzwa vyuo...kujeruhiwa kwenye maandamano kwa sababu ya Siasa....
 
Ndesamburo wa CHADEMA ambae ana uwezo wa kumuweka binti yake na mkwe wake kwenye viti maalum vya ubunge kupitia chadema, kaamuwa kuwachana na mgombea wa CHADEMA na kumpigia debe Lowassa.

Usifanye maskhara katika haya mambo.

Bora vyama vichanga vianvyojaribu kukaribisha kila mtu na kwa kuanzia na familia ili kujenga msingi, lakini pale waliobobea kwa miaka 50 bado wanaendesha misingi ya ki-royal full kurithishana, na wengine wanabaki kuwapigia tu makofi wakati wanadangaywa kwa vitu vidogo na kushia matatizo yale yale yasiyotatulika kwa miaka 50.

Hawa akina Ndesambaro ndio wanavunja pori kutafuta njia tofauti na ilivyo kwa akina Ridhiwani na wale wa kule Tosamaganga.
 
Hiyo ndo siasa...

Shauri yenu mnaofukuzwa vyuo...kujeruhiwa kwenye maandamano kwa sababu ya Siasa....

Ukishaona mfumo huu wa kuridhishana nafasi zilizoachwa wazi katika mazingira ya kisiasa kuna kitu nyuma ya pazia, kama si fukiafukia basi nani zaidi.
 
Zero, jua cdm ni bonge la chama cha siasa ambako ktk checkin point yake wengi wenye uwezo ndani ya cdm yenyewe, vyama vya siasa jirani, vyuo, watumishi mbalimbali, wakulima na wafanya biashara, wengi wame-parade kuingia na wengi uwezo wao kuwa rais ni mkubwa wanasubiri muda utimie. Kama wewe ndio yule ZERO wa katuni za gazeti la Mtanzania zamani ninapoteza muda, lakini kama sio wewe sikiliza: CDM itachambua kati ya waadilifu na mafisadi. Kwa lowasa itakuwa vigumu kukubalika japo yeye na wapambe wake wanatamani. Umashuhuri wake uko kwa baadhi ya wana mtandao alioutengeneza ccm labda watu kama mil. 2 hivi. Kwa watanzania wengine ni mchafu yaani fisadi la kutupwa, lisilo safishika na kuuzika hata kwa kupenyeza rupia. Hata hivyo Slaa bado sana pamoja na nguvu nyingi zinazutumika kumuchafua. Hachafuki kirahisi kama lowasa. Tunajua chuki walio nayo ccm dhidi yake. Cdm ipo kama ilivyo kutokana ilivyowapelekesha 2010, wakiwazia 2015 heri yake ni kuomba Slaa kutokuwepo.
 
Confirmed.

Nadhani hilo neno hapo juu sio geni kwako. Hivyo nina imani unajua vizuri matumizi ya neno hilo, na utaweza kulihusisha na hii habari.

Wana Ukumbi,

Katika hali ambayo imewaacha wengi midomo wazi na baadhi kubaki kukuna vichwa. Ni baada ya kugundua kuwa CHADEMA kwa sasa hali ni tete na inasemekana wamekosa kabisa mgombea atakae peperusha bendera ya chama kwa nafasi ya urais.

Lakini pia CHADEMA hao hao wameonelea sio vyema kuingia kwenye uchaguzi wakiwa hawana mtu anae kubalika na Watanzania wengi. Hivyo imewalazimu watazame vyama jirani vina nini kama ilivyo desturi kwao.

Sasa hapa kwenye nini CHADEMA wamepata kutoka vyama jirani ndio penye maajabu. Sikuwahi kutarajia CHADEMA itaweza kuibuka na jina la Lowassa kama tunu kwao kwenye kuelekea uchaguzi.

Ina maana huyu Lowassa sio yule aliyeitwa fisadi!?

Huyu Lowassa leo amebadilika nini hadi agombaniwe na vyama kugombea katika nafasi ya urais?

Au ni ukweli kwamba Lowassa alisingiziwa kuhusu ile tuhuma na sio kweli kuwa ni fisadi.

Je, kama Lowassa ni fisadi, kwanini Watanzania wawe nae bega kwa bega kwenye movement zake za kuwania urais?

Kweli maneno yametimia, "JIWE LILILO KATALIWA, LEO LIMEKUWA JIWE KUU LA PEMBENI".

Ni ajabu thread za udaku kama hizi kuachwa muda wote hapa.CHADEMA hakiko Desperate kiasi hiki
 
Ni ajabu thread za udaku kama hizi kuachwa muda wote hapa.CHADEMA hakiko Desperate kiasi hiki
Hela zenyewe za kwenda chalinze kwenye uchaguzi hamjapata wajerumani nao wamesitisha ufadhili mtajua zitto kuwa ni nani.
 
Lowasa sio fisadi bali ni tajiri na kila mtu anatafuta UTAJIRI wenye akili wanatajirika "mazuzu" hata kama ni wasomi wanabaki mikapuku. Kuwa tajiri haina maana wewe ni fisadi, funguka.
 
2015 hizi kelele ziishe mfanye kazi sasa.
maana watu wengine wanahisi Lowassa atawaletea mboga nyumbani sasa.
 
Huwezi jua formula za chadema kwa sasa subilini sapliz kama ya 2010


Sent from my iPhone 5 using JamiiForums
 
Lowasa sio fisadi bali ni tajiri na kila mtu anatafuta UTAJIRI wenye akili wanatajirika "mazuzu" hata kama ni wasomi wanabaki mikapuku. Kuwa tajiri haina maana wewe ni fisadi, funguka.

Inaelekea weekend kulikuwa na mgawo hivyo leo watu mmeamkia kutimiza kazi mliyotumwa na fisadi Lowassa & Rostam
 
Back
Top Bottom