**Mkuu wake wa kazi anasema Martha aliacha kazi mwezi mmoja uliopita
**Baba wa marehemu anasema mtoto wake alitekwa na kupakiwa kwenye gari na sio bodaboda pia figo lake liliharibiwa inawezekana alipewa drugs ndo akapigwa moto
Hapa kisasi cha mapenzi au kazi aliyokuwa anafanya yaweza kuwa chanzo
Basi taarifa ya kwanza kuhusiana na kifo chake ina mapungufu makubwa kwakuwa anatambulishwa kama mfanyakazi ngazi ya uhasibu bank ya BOA Shinyanga/Kahama
Taarifa ya Jeshi la Polisi Kibaha
JESHI la Polisi mkoani Pwani limesema mhasibu wa benki ya BOA tawi la Kahama ameuawa kwa kumwagiwa petroli na kuchomwa moto.
Inadaiwa kwamba mhasibu huyo alikuwa amefika Kibaha kwa wazazi wake.
Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Pius Lutumo amemtaja marehemu ni Martha Towo (30) mkazi wa Kwa Mbonde wilayani Kibaha.
Kamanda Lutumo aliwaeleza waandishi wa habari mjini Kibaha jana kuwa chanzo cha mauaji hakijafahamika na wanaendelea kuchunguza.
Inadaiwa kuwa Martha alitekwa jioni ya Machi 3 mwaka huu na saa 4:30 usiku siku hiyo hiyo alikutwa akiungua katika maeneo ya Mitamba Kata ya Pangani.
“Watu wasiojulikana walimteka kisha kummwagia mafuta na kumchoma moto,” alisema.
Kamanda Lutumo alisema taarifa zilitolewa na wasamaria polisi wakafika eneo la tukio na kumchukua kisha kumpeleka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani ya Tumbi.
“Mgonjwa alihamishiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa uangalizi zaidi wa kimatibabu lakini alifariki Alhamisi Machi 9,” alisema.
Lutumo alisema kutokana na utata kuhusu tukio hilo, polisi wanaendelea kuchunguza chanzo cha Martha kutekwa na kuchomwa moto hadi akapoteza maisha.
Halafu ndio imeongezewa hii
Wakati Jeshi la Polisi mkoani Pwani likithibitisha kutokea kwa kifo cha Martha Towo (30) ambaye aliuawa kwa kuchomwa moto baada ya kutekwa usiku wa Machi 3 mwaka huu wilayani Kibaha mkoani Pwani, Bank of Afrika (BOA) imesema, marehemu alishaacha kazi karibu mwezi mmoja uliopita