Loliondo pananuka mauti


Yesu alitenda miujiza mbalimbali kuhihirisha Yeye ni Mungu. Aliacha mambo yatokee ili apate utukufu. Hata tukio la Lazaro kufa liliwaliza wengine Yeye akasema amelala tu, amini, atafufuka. Hivyo kufa kwa Lazaro haikuwa kwa bahati mbaya bali ni kusudi baba atukuzwe katika Mwana. Hata yule kiwete ambaye, Yesu walimuuliza, kazaliwa vile kwa dhambi za wazazi wake? Yesu aliwajibu kuwa, kazaliwa vile ili mapenzi ya Mungu yatimizwe. Hivyo si sahihi sana kuifananisha miujiza ya Yesu na hii ya sasa kwani sisi tumesha mjua Mungu tayari.
 
Babu ameleta balaa kubwa kwa unabii wake wa kutia mashaka, kusema amepewa dawa na MUNGU inayotibu maradhi yote sugu bila kuangalia dini gani kumesababisha maafa makubwa kulinganisha na ilivyotarajiwa.
Vifo vya mateso vya wagonjwa ktk mazingira magumu, mateso wanayopata wagonjwa njiani, vitendo vya ulanguzi wa kukithiri wa nauli, vyakula nk. haya yote ni matokeo ya unabii wake babu.
Tunajua haya yote yapo lakini kwa hili la loliondo ni matokeo ya babu.
Kwa mtazamo wangu huyu "MUNGU" aliye mtuma babu ni waajabu na hayuko fair at all kwa watu wake, mungu anayezidiwa na wagonjwa, mungu mwenye masharti kama sangoma, mungu katili asiyejali watu na kuwaongezea tabu,.
Hakika huyu si MUNGU wangu nimjuae ninaye msoma ktk Bibilia takatifu. Mungu wa rehema anaye taka watu wampokee na kuishi ktk yeye kisha watapata kwakadri ya neema yake. Mungu wangu asiyetuma watu kutoa tiba bali kutuma watu wamtumikie.
Mwisho Bwana asema hivi KWANZA UTAFUTENI UTUKUFU WA MUNGU NA MAMBO MENGINE MTABARIKIWA
 

.
Sema maandiko yasema hivi.... Japokuwa hata hivyo umeshindwa kuyanukuu vema.
WEE!! UNAJUA MAANA YA BWANA ASEMA HIVI, AU UNAAMUA KUROPOKA TU?
.
 

si damu na nyama vilivyokufunulia haya bali Baba yetu alie mbinguni.

ubarikiwe sana mpendwa.

Glory to God
 
 

Kwani Babu ametumwa na Shetani asiweze kufufua? Katika matendo yote makubwa ya miujiza ulimwona Mungu mwenyewe ameshuka? si anatumia watu wake tuu, sasa iweje babu asiweze kuwafufua ka dawa yake?
 
 
 
Kwani Babu ametumwa na Shetani asiweze kufufua? Katika matendo yote makubwa ya miujiza ulimwona Mungu mwenyewe ameshuka? si anatumia watu wake tuu, sasa iweje babu asiweze kuwafufua ka dawa yake?

Nadhani uelewa wako wa maandiko matakatifu una walakini,

Hata kama babu wa loliondo ametumwa na Mungu, bado narudia kukukumbusha kwamba mwenye uwezo wa kufufua wafu ni Mungu pekee, na katika hilo la kufufua wafu Mungu mwenyewe ndiye hutenda kazi. Usijaribu kumlinganisha babu wa loliondo na Yesu Mungu mwana.

Hapa hatuzungumzii matendo yote makubwa na ya ajabu kwa ujumla wake, tunazungumzia specifically hoja ya kufufua wafu, kitu ambacho hakuna mwanandamu yeyote amewahi kupewa uwezo, kipawa ama karama ya kufufua wafu.

Babu wa loliondo ametumwa na Mungu kwa kazi ya kuwapatia watu kikombe, na Mungu mwenyewe anatenda kazi kupitia hapo, suala la kufa ama kutokufa ni Mungu mwenyewe ndo anajua.
 
Ni upi ushahidi wa wazi kwamba babu katumwa na MUNGU?.
Je yeye kusema tu kwamba kaonyeshwa dawa ndotoni na MUNGU yatosha kutufanya sisi tuamini kwamba katumwa na MUNGU?.
Kama ukimwamini babu bila kuhoji, akitokea mtu mwingine akasema ameoteshwa na MUNGU kwamba kila mwisho wa mwezi lile fungu la kumi la mshahara wako umpe yeye( muotaji), utampa?.

Wandugu, yatupasa kuzipima kila roho zinazotumia jina la MWENYEZI MUNGU kufanya mambo yake.
 

Naona ulikuwa unamaanisha hizi.







Kama wenye ndugu wamewaacha hii haipendezi hata kidogo.
 

Je wewe una ushahidi gani kwamba hajatumwa na Mungu? una ushahidi gani kwamba katumwa na shetani??

Tatizo sio kuhoji, tatizo ni pale watu mnapomhukumu babu bila kuwa na ushahidi wa maandiko matakatifu, mnamhukumu kwa sababu zenu binafsi.

Nakubaliana na wewe kwamba tunapaswa kuzipima roho zinazotumia jina la mwenyezi Mungu, sasa nakuuliza swali hapa, je wewe umeipima hiyo roho inayotenda kazi kwa babu wa loliondo??
 
Kalale Loliondo wewe unaambiwa A unasema yei tukusaidiaje?
 
Huna hoja kumbe unabwabwaja tu. Mtakufa njaa mwaka huu, babu kachukua wafuasi wenu wote!!:lol:

yOTE KWA YOTE NI SIKU YA MWISHO! si babu si wewe si mimi hukumu iko swafi tu! hebu soma thread moja imo humu kwenye jukwaa la lugha imeandikwa WANASUBIRI HUKUMU YA MZEE GAZETI!
 
Kuna baazi ya wachangiaji wanaomhukumu babu kwa sababu tu eti Mungu anaemtumia hajajijulisha ni wa dini gani. Hii inanipa wasi wasi kama kweli tunazifahamu tabia za Mungu kwa watu wake. Kwa upande wa watu wa biblia Mungu hakuwahi kujinasibisha na dini yoyote. Au labda tusaidiane kwa upande wa manabii wa Mungu maana ndio huji
funua kwao, dini zao ama dini yao iliitwa je?
Labda tuanze na kina Henoko,Nuhu,Abraham,Isaka,Yakobo,Nehemia,Isaya,Yeremia,Ezekieli mpaka kwa Yahana mbatizaji na wa agano jipya, dini yao iliitwa je?
Au kwa kifupi tujiulize ni nabii yupi katika wote wa OT/NT aliyewahi kuwa na dhehebu?
.
 

Upo ushahidi mwingi ambao unaonyesha kuwa babu na Mungu wanatofautiana sana
1. Masharti- Wakati Mungu amewatuma watumishi wake kwenda ulimwenguni kote kuhubiri injili na kuponya wagonjwa, babu anasema hapana mimi siendi popote watu watanifuata Loliondo.

2. Wakati uponyaji wa Mungu ni for free, mmepewa bure, toeni bure, babu anatoza watu pesa.

3. Wakati palipo na uponyaji wa Mungu watu wanakuwa wazima, kwa babu watu wanakunywa kikombe halafu wanasikilizia kama watapona, wengine wanakufa.

4. Wakati Mungu ana namna tofauti za kuponya (very rich kwenye uponyaji), babu anategemea aina moja ya uponyaji.

Hiyo ya babu huwa tunaiita CULTIC AND DECEPTION MOVEMENT, wenye macho tunamjua AUTHOR wake. The author of this movement has come to KILL and DESTROY!! BE ON THE WATCH TANZANIA!!
 

Pia tumeambiwa tuwe na imani kwamba kikombe kinaponya. He! Hii ni ibada ya sanamu kabisa. Yaani Mungu anafananishwa na kikombe cha babu? Kwamba mzizi hauponyi ila nano lililomo ndani ya kikombe! Wee, wacheni kabisa habari yenu hiyo. Kristo ni NENO. Na huyo neno nimuabuduye mimi hakai kwenye kikombe cha Loliondo kwani yuko moyoni mwangu.
 

umehit penyewe kabisa mpendwa,

asomaye na afahamu, kweli sasa ni dhahiri, Neno wa Mungu hawezi kukaa kwenye kikombe wala sehemu nyingine yoyote zaidi ya moyoni mwa mwanadamu. tangu wakati wa Yesu hata sasa na hata milele na milele ijayo, ibada zetu ni za
1. roho
2. Kweli (Neno la Mungu)

hakuna ibada ya kikombe!

NENO wa Mungu alifanyika mwili akakaa kwetu nasi tukauona utukufu wake,
utukufu kama wa Mwana pekee wa Baba
amejaa neema na Kweli
 

Mkuu umejibu vema kabisa, mtu hato ishi wala kupona kwa kikombe cha babu bali kwa neno la uzima likikaa ndani yake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…