Loliondo pananuka mauti


Si rahisi sana kama sio mtu wa rohoni kuyatambua mambo kama haya! Babu haui, dawa yake haiui, serikali haiui, wagonjwa hawajiui ila Hii ni mbinu kubwa ya shetani kuua watu!
 
Nadhani problem tree yako ingeonyehsa mzunguko kamili, kwani ilioita matokeo, mengine ndio yamesababisha tiba ya babu kuwa kama ilivyo,
Tiba hii ni kati ya matokeo ya matatizo makubwa tulionayo. umasikini, ujinga na maradhi!!!

hahahahahahahahaha wewe umekula kweli mchana huu?
 

Wewe ndo mwenyewe mwayaaa!
 
Aisee umenifurahisha sana yaaniView attachment 25819
 
Too late. Kwani umewmuliza akasema 'hapana''? Tafakari kwanza mwenyewe.

Inaonekana umeandika ukiwa usingizini?? Inaumaje ukweli ukisemwaaaaa??? Babu ni mganga wa jadi
 
.... babu hana shida SHIDA NI KWAMBA INATAKIWA BABU AWEKE WAZI TU KWAMBA YEYE NI MGANGA WAJADI (naogopa kusema) pia watu wanatakiwa watambue kuwa huo unaweza kuwa mtego mbaya wa shetani ili awaue watu!

Usiogope Mkuu....kwa mujibu wa sheria za Tanzania (The Traditional and Alternative Medicines Act, 2002) Babu ni Traditional Health Practitioner, bahati mbaya sheria imeandikwa kizungu. Lakini kwa tafsiri nyepesi yes, kisheria anaangukia kwenye kundi la 'waganga wa jadi' (Traditional Health Practitioners).
 
 

my goodness! yani sasa umefikia kiwango cha kusema Yesu alifanya makosa? Tafadhali sana...kubali kuwa huelewi hii ishu. Hapa utaishia kukufuru bure! Sema tu mimi sio mjuzi, na haya ni mawazo yangu. Kwisha. Usijaribu kabisa kueleza vitu usivyojua. Utakosa uzima wa milele bure. Kama huamini Loliondo na unaona kuna vitu basic kwenye biblia vimevunjwa...sawa weka wazi. lakini kama unaanza kwa kuweka story nusu nusu za biblia, utaishia kukufuru kabisa.
Yesu alijua toka mwanzo kuwa atamfufua Lazaro. Huu ulikuwa ni mmoja wa miujiza yake mikubwa. Na 'kuchelewa' kwake (siku tatu) kulikuwa ni njia ya kutimiza huo muujiza.
But my point remains, kuwa watu wanaweza kufa wakiwa wanasubiri msaada Mungu. Huwezi sema kuwa kufa ukiwa njiani ina maana kuwa Mungu hayupo involved. It may suggest that but its not a strong suggestion. Wewe fanya sala muombe Mungu akufunulie ukweli juu ya hii ishu.
 
Wacha kukosoa na amplify hoja inayolenga! Kama Yesu aliambiwa mapema kwenda kumombea Mgonjwa na akachelewa unadhani ilikuwa haki? Na lazima uelewe si kila mtu akisema kukosea amamaanisha unavyodhamiria wewe! Unaonekana hata hujui maana ya kufuru! Vipi? mbona hujengi hoja iliyokuwa inaendelea?? Yesu alienda kumponya Lazaro hata kama alikufa babu amemponya nani aliyekufa?? BABU MUUAJI TU! WIZI WA NAMNA HIYO HAUVUMILIKI!
 
Haya ndiyo alikuambia Babu au wewe mwenyewe umejitungia?

Mbona anawaambia watu watumie dawa nyingine? Mnajitungia na kuanza kuamini....

Babu hawezi kukataza mtu kutumia hiyo dawa ya kurutubisha mwili uliochakaa.....

Kwani umeambiwa Babu anatoa KINGA? Babu anaponya tu, basi.

Unataka kusema babu kasema pia ukinywa dawa basi USILE maana UMEPONA? Ila dawa ni kama Chakula.

Hakuna aliyechakachua ila wenyewe MNAJIDANGANYA na mwisho mnaamini MATAPISHI YENU.

Kasitisha matibabu kwa WIKI moja sasa mtapumua maana HOSPITAL zilikuwa zimekauka, hahahaaaa........
Acheni kupamba hoja zilizowazi! Hairuhusiwi kunywa ARV ukinywa dawa ya Babu haya ndiyo masharti ya awali labda kama mmeyachakachua sawa!
 
Acheni kupamba hoja zilizowazi! Hairuhusiwi kunywa ARV ukinywa dawa ya Babu haya ndiyo masharti ya awali labda kama mmeyachakachua sawa!

Usipende kutumia chanzo kimoja cha habari ili kufikia conclusion,

Kwa bongo hii ambayo vyombo vya habari vinaandika habari kutokana na matakwa binafsi ama kutia chumvi habari kwa maslahi binafsi, unatakiwa kufuatilia vyombo vingi vya habari kabla hujatoa hukumu.

Hii habari ya kwamba babu kazuia waathirika wa VVU kutotumia ARVs unaikuza tu ili kujenga hoja dhidi ya babu, ama umepotoshwa na chanzo chako cha habari.

Nitakupa mfano mmoja tu, jana kwenye kipindi cha njia panda kinachorushwa na clouds fm kila jumapili kuanzia saa nane kamili mchana, kuna binti anaitwa jack ametoa ushuuda wake, alikwenda loliondo kupata kikombe na yeye ni muathirika.

Alikanusha kabisa hii propaganda kwamba babu amewazuia wagonjwa wa ukimwi kuendelea kutumia ARVs, babu ameendelea kuwasisitizia wale wote walioathirika waendelee na tiba zao hadi hapo watakapopima na kuthibitika kupona.Na si waathirika wa ukimwi tu, bali pia na wanaougua maginjwa mengine hawajazuiliwa kuendelea na tiba zao.
 

hahaha...umeanza na kubadilisha maneno. Kubali hujui tu na huna jipya.
babu amesema anaponya au kikombe na imani ndio vinaponya? Yeye kapewa maagizo specific. Hayo mengine ni juu yenu. Kama unataka ku-disprove, onyesha kuwa kikombe na imani haviponyeshi. Sio unakuja hapa na story nyingi.
 
Ya kaisari mpe Kaisari na ya MUNGU mpe MUNGU! Huwezi kumjaribu BWANA MUNGU wako! MUNGU alimtoa YESU auawawe kwa ajili yetu, MUNGU pia alileta gharika na kuteketeza kizazi chote na kumuacha NUHU na wanyama aliowateua, Mungu pia anasema kila roho itaonja mauti ili ifike kwake. Haina maana kuwa ukinywa kikombe cha Babu hautakufa na kuwa utaishi milele! Babu haombei bali anakupa dawa unywe hivyo tusimbeze umati wote huu unaoenda kwake unaonesha wazi yote ni ya kweli kama ni uongo ungejulikana mapema na watu wangesitisha! Kumbuka huwezi kumjaribu BWANA MUNGU wako!!!!
 
 

Hmethod kaka kumbe Babu haombei tena?
Siku mbili zilizopita ilikuwa inasemekana humu anaombea kwa jina la Yesu!!!
Na tukisafari na hoja ya wengi wape, sijui kama itafaa kwa kila kitu aisee.
Ujue ni mateso na matatizo tu, ndio yanayowafanya watu wahangaike hivi.
 

Mwenye uwezo na mamlaka ya kufufua wafu ni Mungu pekee.

Kama mnataka kumlinganisha babu na Mungu hapo ndipo mnaposhindwa hata kuyaelewa maandiko matakatifu, badala yake mnajaribu kujificha kwenye maandiko matakatifu kumshambulia babu kwa sababu ya chuki zenu binafsi.

Ndugu yangu usiwe unasoma Biblia kama unavyosoma gazeti la udaku, unahitaji uwezo wa KiMungu kuisoma na kuielewa Biblia.
 
Si rahisi sana kama sio mtu wa rohoni kuyatambua mambo kama haya! Babu haui, dawa yake haiui, serikali haiui, wagonjwa hawajiui ila Hii ni mbinu kubwa ya shetani kuua watu!

Labda nikuulize swali la msingi hapa, mtu wa rohoni ni nani? na utamtambuaje?
 
Hivi kuna KUPONYA mtu ALIYEKUFA?

Mie nilikuwa najua kuwa Mtu aliyekufa akipata UHAI basi ni kuwa KAFUFUKA.

Na kwa maana hiyo, huko siyo kuponya bali KUFUFUA.

Kweli mie Mnyamwezi sifahamu KISWAHILI.
 
Nionavyo mimi ni kwamba huduma anayoifanya babu sii ya kawaida kama wanavyofikiri wengi. Kuna watu wanamjadili babu kwa muono wa kuhubumia watu mia kadhaa. Kwa babu kuna mkusanyiko usio kawaida kwa maana ya wingi bila support ya miundombinu stahiki. Hata hivyo serikali imekubali kumonitor zoezi la kuhakiki idadi itakayokuwa haimuelemii babu kwa siku. Na kutengeneza mazingira ikiwa ni pamoja na vyoo na mashimo ya taka na mahema ya kujikinga mvua. Kama barabara zingepitika na watu kumfikia babu kwa siku moja tu nafikiri kusingekuwa wingi wa vifo.
Sitaki nifikiri kwamba wale waliokufa wamepungukiwa na imani, kwani kutoroka hospital na kwenda kuunga foleni ni imani tosha. Tatizo ni mazingira tu. Kwa watu wa imani na hasa ya ukristo tunapaswa kufahamu kuwa hata wana wa Israel walipotoka Misri Musa aliwaambia kwamba wanaelekea nchi ya ahadi. Jangwani mchana walifunikwa na wingu jua lisiwapige na usiku wingu la moto liliwaangazia nuru lakini hata hivyo pamoja na uwepo mkuu wa Mungu walikufa mbele zake na kuzikwa jangwani. Tena tunaambiwa kati ya wote waliondoka misri wakiwa na akili za kupambanua ni wawili tu walioingia Kaanani.
Binafsi mimi namwona babu kama mtu anaeupendeza moyo wa Mungu na wanadamu pia kwa kuwa pamoja na muujiza aliopewa hana kiburi cha kujisikia. Anasikilizana na viongozi wa kitaifa na kuafikiana nao katika masuala mihimu, bila kuyaasi maono aliyodai kupewa na Mungu.
Tujiulize pia kwamba hospitali zote za tanzania ndugu wamewatorosha wagonjwa wao tena wale sugu kuelekea kwa babu, kwa hali ya kawaida tu tukiondoa ushabiki na chuki, hatutarajii vifo? Maana waliopaswa kuwekwa mortuary zote nchini kwa wakati huo wapo njia moja kuelekea kwa Babu.
.
 
Hii mada ya Loriondo siipendi kwa sababu haina mambo endelevu zaidi ya kuleta utata wa matusi, na kejeli kwenye maanadiko ya Mungu. Ebu, acha wafu wawazike wafu wenzao. Kama wewe una akili timamu unamchukua mgonjwa mahututu umpeleke kwa babu, obvious kuna mawili kufa unasubiri dawa au hujafika.

ACHA WAFU WAWAZIKE WAFU WENZAO.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…