Loliondo, OBC, Dowans: The disturbing connection and secrets

Sad story about the abuse of our own people in their own mother land....shame to the government they have not yet reacted now DONOR countries are making noise. I am surprised this question was not raised in the recent JK live question and answer TV show.... or was the show censored for sensitive issue

 
wajameni mimi naomba kuuliza
KAMA NYERERE ANGEYAFANYA HAYA KATIKA MIAKA YAKE 23 ALIYOKAA IKULU HII TZ INGEKUWEPO?
KAMA KWA MIAKA MICHACHE HII WALIOPOKEZANA URAISI (MWINYI, MKAPA NA JK), WAMEIMALIZA NCHI WALIYOIKUTA VIRGIN KABISA

RIP NYERERE
NA WALAANIWE WOTE WALIOKUFUATA KWENYE UONGOZI (MWINYI, MKAPA NA JK)
 
Loliondo ingeulizwa CCM wana majibu ya hiyo hifadhi.

Ushenzi mtupu tu kudaddeki nina usongo sana na Loliondo. Mungu yupo na waliohusika watampata tuu kiboko yao. Huyu Mwinyi na mke wake wseng sana.
 
je hamfahamu kuwa hili ni shamba la bibi ambalo kila mwenye shida huja kuvuna?ni kama vile hakuna viongozi wala nchi haina wenyewe,hili ni dharau kubwa kwa nchi yetu
 
Watanzania tunayataka wenyewe,Unategemea serikali Itafanya nini? Mfumo wote umeharika hakuna anae jali hata kidogo inasikitisha unapo ona mambo ya yanayo fanyika huko loliondo jamani hivi kweli viongozi wetu hawaoni?

Mnataka mpaka fujo itokee?
 
Wakazi wa Loliondo wavamia Ikulu Dar Sunday, 13 September 2009

Wananchi wanaodai kubomolewa makazi yao kwa lengo la kumpisha mwekezaji eneo la Loliondo, Wilaya ya Ngorongoro, Arusha wakiwa nje ya lango kuu la kuingilia Ikulu ya Rais Jakaya Kikwete, Dar es Salaam jana ambapo walikwenda kumuona ili wamueleze kilio chao.(Picha na Rajabu Mhamila)

*Mkuu wa Wilaya awatuliza, FFU wakaa chonjo
*JWTZ yatahadharisha, yasema jeshi sio katili

Na Rajabu Mhamila

WAKATI kampeni ya kuwaondoa wananchi walioweka makazi katika eneo la Loliondo lililoko katika Hifadhi ya Ngorongoro ikiendelea, baadhi ya wananchi waishio katika eneo hilo jana walivamia lango la Ikulu jijini Dar es Salaam wakitaka kuonana na Rais Jakaya Kikwete kuhusiana na mgogoro huo.

Akizungumzia suala hilo msemaji wa wakazi hao waliobomolewa majengo yao Bi.Paulina Tipap, alisema kuwa waliamua kwenda Ikulu kupata tamko kutoka kwa Rais mwenyewe kwa kuwa hawana mahali pa kuishi kutokana na makazi yao kubomolewa.

" Nia yetu kubwa ya kuja hapa ni kuonana na Rais kwa sababu sisi ni wapiga kura wake halali tuliomchagua kwa kura zote na tunasikitishwa na kitendo cha kuondolewa bila hata taaratibu zozote," alilalamika.

Hata hivyo baada ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bw. Evans Balama kuwasili maeneo ya Ikulu na kuzungumza nao waliamua kuondoka na kuazimia kwamba endapo tatizo lao halitapatiwa ufumbuzi atarudi tena na safari hii watalala katika lango kuu la Ikulu.

Bw. Balama aliwashukuru kwa kuwa waelewa na kuwajibu kwamba Rais asingeweza kuonana nao kwa vile alikuwa kwenye kikao muhimu. Hata nikiwaambia njooni kesho sina uhakika kama mtaonana nae," alisema

Hata hivyo mkuu huyo wa wilaya alikabidhiwa tamko la wakazi hao ili aliwasilishe kwa Rais Jakaya Kikwete mwenyewe.

Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Suleiman Kova na askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia walifika katika eneo hilo ingawa hawakuchukua hatua yoyote baada ya Mkuu wa Wilaya kuwatuliza wananchi hao.

Naye Gloria Mhiliwa anaripoti kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii Bi. Shamsa Mwangunga amezungumzia mgogoro uliopo Loliondo wilayani Ngorongoro kufuatia Serikali kuendesha operesheni ya kuwaondoa wafugaji waliojenga kwenye kitalu cha uwindaji na kusema kuwa operesheni hiyo ilifanyika kwa maslah ya taifa.

Waziri Mwangunga aliyasema hayo jana Ngorongoro muda mfupi baada ya makabidhiano ya mradi wa asasi ya ERETO kwa Baraza la Wafugaji wa Ngorongoro pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro ambapo alisema kuwa operesheni ya kuwaondoa wafugaji hao ilifanyika kwa utulivu isipokuwa baadhi ya taasisi zisizokuwa za kiserikali [Ngos] ambazo zimekuwa zikitumia baadhi ya vyombo vya habari kupotosha kweli kwa maslah yao na Taasisi zao.

Alisema kuwa eneo la Loliondo ni pori tengefu ambalo linalipatia Serikali fedha nyingi sana na wananchi wa eneo hilo kupitia makubaliano yao na mwekezaji wa kampuni ya uwindaji ya Otterlo Business Company[ (OBC) ambapo kwa mwaka Serikali inapata milioni 500 na wananchi wa vijiji nane vinavyopakana na eneo hilo la OBC hupewa kila mwaka shilingi milioni 300 kupitia makubaliano yao.

Alisema Serikali haiwezi kukaa kimya kuona uharibifu wa mazingira ukiendelezwa Loliondo kwa kuwaacha watu wakate miti ya kujenga maboma pamoja na kuendeleza shughuli za kilimo.

Alisema kuwa wananchi wa vijiji hivyo hususani katika eneo la pembezoni na eneo la uwindaji waliruhusiwa kupeleka mifugo kwa ajili ya malisho lakini siyo kujenga maboma ambapo hukata miti mara kwa mara ama kulima na kwamba kufanya hivyo ni kuharibu mazingira ambayo yatasababisha kutoweka kwa wanyamapori.

Alisema kuwa bila ya pori la Loliondo hifadhi ya Taifa ya Serengeti haitakuwepo kwa kuwa maji yote ya hifadhi hiyo kama mto Grumeti vyanzo vyake vipo kwenye msitu wa Loliondo pia ni mapito ya wanyamapori kutoka Ngorongoro, Serengeti kwenda Masai mara nchini Kenya pia ni chanzo cha maji cha Loliondo yenyewe.

Alisema kuwa uharibifu wa mazingira kwenye eneo hilo la msitu ulianza taratibu kuanzia mwaka 2006 na ndipo Serikali ilipoamua kuanzisha operesheni hiyo Julai 4 ya mwaka huu ambapo viongozi wa vijiji walishirikishwa inagawa waziri Mwangunga alikiri kuwa kulikuwa na mapungufu kidogo katika kuwashirikisha wananchi japokuwa ni mapungufu madogo sana.

'Mimi mwenyewe nimekwenda Loliondo mara nyingi tangu mgogoro huo uanze lakini hakuna mwananchi aliyebakwa wala aliyechomewa chakula chake kama nilivyosema hapo awali baadhi ya taasisi ndizo zinazowapotosha wananchi zinawapa nauli kwenda Dar na kuwaeleza mambo ya kuzungumza kwa nini wawaeleze vitu vya kuzungumza hapa kuna maslahi binafsi inatakiwa eieleweke' alisema Mwangunga.

Wakati huo huo Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ) limetoa tahadhari kuwataka wananchi wa Kata ya Mashono, Arusha kutoandamana kwenda Ikulu kwa kuwa mgogoro huo ulikuwa ukitafutiwa ufumbuzi.

Akizungumza na waandishi wa habari Makao Makuu ya jeshi hilo jana, Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Kanali Abraham Shimbo, alisema Waziri wa Ulinzi na JKT, Dkt. Hussein Mwinyi na Mkuu wa Majeshi, Jenerali Davis Mwamunyange wametoa maelekezo ya muafaka wa kumaliza mgogoro huo.

Alisema jeshi hilo haliwezi kuwa katili kwa wananchi wake inaowalinda japokuwa hukalia ardhi hiyo kwa mujibu wa sheria sawa na taasisi nyingine kulingana na Sheria ya ulinzi wa Taifa ya mwaka 2002.

Alisema ardhi inayomilikiwa na jeshi hutumika kuweka kambi, zana za ulinzi,mafunzo, mazoezi, shule, maghala, karakana, hospitali, viwanda,viwanja vya ndege, viwanja vya shabaha,mafunzo ya zana, mafunzo ya vikosi maalum na mashamba ya uz na maghala yote ni salama.alishaji mali.

Alisema baadhi ya wananchi wamekuwa wakijitwalia ardhi ya jeshi wanapokuta eneo la wazi au msitu bila kujua eneo hilo limetengwa kwa kazi hizo.

Luteni Kanali Shimbo alisema wananchi ndiyo wanaofuata huduma katika kambi za jeshi lakini badala yake wamekuwa wakali kuondoka wanapotakiwa kufanya hivyo kupisha kazi nyingine.

Aliwashauri wananchi wanaofuata huduma katika kambi za JWTZ kuanza ujenzi baada ya kupata ridhaa ya Manispaa zinazohusika na Wizara ya Ardhi na maendeleo ya Makazi.
 
Hivi tangu tuingie mkataba na Ortelo na kukodisha ardhi ya Loliondo, ni mapato kiasi gani yamepatikana na yametumika vipi? Kuna mtu mwenye takwimu kuonyesha mapato tuliyoyapata tangu 1992?
 
Hivi tangu tuingie mkataba na Ortelo na kukodisha ardhi ya Loliondo, ni mapato kiasi gani yamepatikana na yametumika vipi? Kuna mtu mwenye takwimu kuonyesha mapato tuliyoyapata tangu 1992?
Rev.
You always ask the unaskable questions!
 




..Mnadhimu Mkuu wa JWTZ ni Luteni Jenerali Abdulrahman Amir Shimbo.

..ni makosa makubwa sana kwa mwandishi kumteremsha ngazi na kumtambulisha kama Luteni Kanali.

Jasusi,Rev.Kishoka,

..Waziri anadai vijiji nane vinapata millioni 300 kila mwaka.

..kama kweli zingekuwa zinawafikia walengwa sidhani kama wangekuwa na malalamiko na hasira kiasi hiki.
 
Kuna Docs hapa maana refer yale ya wakati ule kuanzia kipindi cha Mwandishi yule marehemu aliandika sana kuhusu Loliondo. Kuna docs zinacconect mkuu wangu
 
loliondo ni nchi ya uarabu ndani ya nchi ya Tanzania. hata ukifika na simu yako pale utakuwa una-roam na unapewa ujumbe kabisa. hatari
 
jokaKuu,
Millioni 300 ukizigawa kwa 8 ni hela kidogo sana. Haziwezi hata kukidhi mahitaji ya shule ya msingi katika kijiji kimoja. The question is huyo "mwekezaji" anapata nini katika mbuga hizo ukilinganisha thamani ya uwekezaji kwa mwenye ardhi na mwenye mtaji? Who is taking who for a ride?
 
this was the msg "Welcome to UAE Enjoy your stay while roaming and surfing with Zain. For Customer Care assistance please call +255784105401 (chargeable call)"
huwezi amini hii ni kweli nendeni mkaone. maskini stanley katabaho aliona mbali
 
Jasusi,

..nakubaliana na wewe kwamba ni hela ndogo kwa vijiji vinane.

..lakini hao wawekezaji si wamekuwepo huko tangu end of 90s.

..na wanadai wanatoa millioni 300 kila mwaka.

..hizo pesa ukizipeleka kwa kijiji kimoja kimoja kila mwaka unaweza kufanya mambo ya maana na maendeleo.

..kwa upande mwingine nakubaliana na wewe kwamba fedha hizo ni kiduchu kulinganisha na kile ambacho "mwekezaji" anakipata Loliondo.

NB:

..binafsi nahisi hizo hela hazijawafikia wenye stahiki nazo.

..kuna wakazi kutoka mikoa yenye uwezo hapa Tanzania walikusanyana kufanya fundraising kwa ajili ya elimu, and they couldnt raise 300 mill Tshs.
 
Huo ni uzushi wa hali ya juu tupe na data za mbuga zingine zilizokodishwa na wazungu? au zao zilikuwa hazina wakazi?
 
Huo ni uzushi wa hali ya juu tupe na data za mbuga zingine zilizokodishwa na wazungu? au zao zilikuwa hazina wakazi?

Na kwenyewe wameandamwa! Wenye Grumeti waliisha wahi kupigiwa kelele kuhusu mahusiano yao na wahadzabe.

Sasa unataka kutuambia kwa vile wazungu nao wanafanya uovu basi tusiwaandame waarabu? Unaipenda kweli nchi yako au umeweka mbele uhusiano wako wa kidini?

Amandla....
 

FM:

Pesa haina dini au rangi. Cha muhimu ni kuangalia taratibu na haki kama inatendeka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…