wanajamvi, naomba ushauri wenu. natamani sana kwenda kupata kikombe kwa babu lakini sina uhakika wa kile anachokifanya. sina ugonjwa wowote mwilini ila nasikia ugonjwa si lazima ninaweza kwenda kupata kinga. nimesoma kwenye vyombo vya habari jinsi watu wengi tena wenye hadhi wanavyokimbilia loliondo nami najiuliza, je is there anything special in this concoction? je ni kweli inafanya kazi? na jee kuna shuhuda zozote zimetolewa kuhusu matibabu ya babu na ni ngapi? mimi nasikia tu mambo ya imani lakini najiuliza imani na dawa ni vitu viwili tofauti. imani ni spiritual na dawa ni physical treatment, mbona nachanganyika? nikidhani ukipata malaria unapewa dawa mseto hospitali wala hakuna daktari atakuambia kunywa kwa imani.
natangulisha shukrani zangu
natangulisha shukrani zangu