Loliondo hii nayo kali

charndams

JF-Expert Member
Nov 12, 2010
436
128
wanajamvi, naomba ushauri wenu. natamani sana kwenda kupata kikombe kwa babu lakini sina uhakika wa kile anachokifanya. sina ugonjwa wowote mwilini ila nasikia ugonjwa si lazima ninaweza kwenda kupata kinga. nimesoma kwenye vyombo vya habari jinsi watu wengi tena wenye hadhi wanavyokimbilia loliondo nami najiuliza, je is there anything special in this concoction? je ni kweli inafanya kazi? na jee kuna shuhuda zozote zimetolewa kuhusu matibabu ya babu na ni ngapi? mimi nasikia tu mambo ya imani lakini najiuliza imani na dawa ni vitu viwili tofauti. imani ni spiritual na dawa ni physical treatment, mbona nachanganyika? nikidhani ukipata malaria unapewa dawa mseto hospitali wala hakuna daktari atakuambia kunywa kwa imani.
natangulisha shukrani zangu
 
Ndugu yangu sina ushauri wa moja kwa moja,ila nitakusimulia machache.
Mimi ni tabibu ktk kitengo cha UKIMWI.Baadhi ya wagonjwa wangu wamekwenda kwa Babu.Kwa imani kubwa waliyokuwa nayo kwa babu huyu,wengine waliamua kuacha dawa za ARVs,hawa wamefariki watano kwenye clinic yangu,wengine wote HIV status zao ni POSITIVE.Ndugu zangu wenye kisukari na pressure wamekwenda kwa babu lakini hadi leo hali zao bado ziko vilevile.
Ninayokueleza hapa ni ukweli mtupu na ukumbuke mimi nina kiapo.FANYA MAAMUZI.
 
Ndugu yangu sina ushauri wa moja kwa moja,ila nitakusimulia machache.
Mimi ni tabibu ktk kitengo cha UKIMWI.Baadhi ya wagonjwa wangu wamekwenda kwa Babu.Kwa imani kubwa waliyokuwa nayo kwa babu huyu,wengine waliamua kuacha dawa za ARVs,hawa wamefariki watano kwenye clinic yangu,wengine wote HIV status zao ni POSITIVE.Ndugu zangu wenye kisukari na pressure wamekwenda kwa babu lakini hadi leo hali zao bado ziko vilevile.
Ninayokueleza hapa ni ukweli mtupu na ukumbuke mimi nina kiapo.FANYA MAAMUZI.
Acha kupotosha umma!...Hakuna ukweli katika usemayo.
Njaa yako ya vipande 30 vya fedha itakudhalilisha!
Nimegundua kuwa una hiana na babu, na hofu yako ni kwamba utapungukiwa customers!
Tafuta njia za kawaida za kuvutia wateja, boresha vyoo hapo kwenye clinic yako, na uache ku-hike bei za dawa!
Kwa babu watu wanapona!
 
Acha kupotosha umma!...Hakuna ukweli katika usemayo.Njaa yako ya vipande 30 vya fedha itakudhalilisha!Nimegundua kuwa una hiana na babu, na hofu yako ni kwamba utapungukiwa customers!Tafuta njia za kawaida za kuvutia wateja, boresha vyoo hapo kwenye clinic yako, na uache ku-hike bei za dawa!Kwa babu watu wanapona!
nadhani wewe ndio mpotoshaji mkubwa!
 
Hakuna hata mtu 1 aliekwenda kwa babu akapona,niutapeli tu unaoendelea kufanyika.ila werevu walishtuka tokea mwanzo kua ni utapeli tu.
 
Watu ninaowafahamuu wamepona wanafika watano including baba yangu sukari kushney!
Wapo wanaokufa hasa kama una historia ya ushrikina au kuuwa watu ukinywa kikombe lazima uvute nina ushaidi wa watu watatu
 
wanajamvi, naomba ushauri wenu. natamani sana kwenda kupata kikombe kwa babu lakini sina uhakika wa kile anachokifanya. sina ugonjwa wowote mwilini ila nasikia ugonjwa si lazima ninaweza kwenda kupata kinga. nimesoma kwenye vyombo vya habari jinsi watu wengi tena wenye hadhi wanavyokimbilia loliondo nami najiuliza, je is there anything special in this concoction? je ni kweli inafanya kazi? na jee kuna shuhuda zozote zimetolewa kuhusu matibabu ya babu na ni ngapi? mimi nasikia tu mambo ya imani lakini najiuliza imani na dawa ni vitu viwili tofauti. imani ni spiritual na dawa ni physical treatment, mbona nachanganyika? nikidhani ukipata malaria unapewa dawa mseto hospitali wala hakuna daktari atakuambia kunywa kwa imani. natangulisha shukrani zangu
Usiende mkuu, walioenda wanajuta sasa, wengi wamezidiwa au kupoteza maisha.
 
hapa utapata ushauri wa kwenda na kutokwenda...ukitaka kupata uhakika nenda na uje utupe testimony hapa jukwaani.
 
wanajamvi, naomba ushauri wenu. natamani sana kwenda kupata kikombe kwa babu lakini sina uhakika wa kile anachokifanya. sina ugonjwa wowote mwilini ila nasikia ugonjwa si lazima ninaweza kwenda kupata kinga. nimesoma kwenye vyombo vya habari jinsi watu wengi tena wenye hadhi wanavyokimbilia loliondo nami najiuliza, je is there anything special in this concoction? je ni kweli inafanya kazi? na jee kuna shuhuda zozote zimetolewa kuhusu matibabu ya babu na ni ngapi? mimi nasikia tu mambo ya imani lakini najiuliza imani na dawa ni vitu viwili tofauti. imani ni spiritual na dawa ni physical treatment, mbona nachanganyika? nikidhani ukipata malaria unapewa dawa mseto hospitali wala hakuna daktari atakuambia kunywa kwa imani.
natangulisha shukrani zangu
Kama unahisi unazo pesa za kukufikisha na kujikimu uko Loliondo, nakushauri bora utafute kituo cha kulelea mayatima uwapatie hizo pesa, kuliko kwenda kupoteza muda na wakati wako bure, ukaja kujuta maisha yako yote.
 
Back
Top Bottom