Umenifurahisha sana, siku izi vijijini ukienda kwenye shughuli yoyote. Usipokuwa mjanja ukatafuta sehemu hotels ya kuifadhi baadhi ya vitu vyako Lazima upate changamoto kama ya kuibiwa nguo na vitu vidogo vidogo kama simu na vinginevyoHuko msibani hakuna nyumba?
Post sent using JamiiForums mobile app
Wakuu naomba mwenye kujua Lodge ambayo naweza kufikia pale Kyela ambayo haiko mbali na stand. Isizidi 20k. Kama nitapata mawasiliano kwa ajili ya booking sio mbaya.
Asanteni
Post sent using JamiiForums mobile app
Safi sana mkuu unaonekana mwenyeji OK!
!
Zipo kibao aisee.... Nakuelekeza hapa ukihitaji maelezo zaidi utauliza. Kuna matema Beach hotel hii ipo karibu na chuo cha ufundi na biashara cha Kyela Polytechnic iko poa sana japo facilities sio kiviiile ila iko fresh. Kuna unenamwa inn hii ni 12,000 nadhani ila kuna bar hapo hapo kwa hiyo kuna kelele yes ila iko so safe aisee. Pia kuna guest moja iko mitaa ya [HASHTAG]#sinza[/HASHTAG] ukitokea huku sativa kuelekea escape moja kwa moja chini kule ni 15,000 pako poa sana. Ya mwisho ni mjini kuna lodge ipo mitaa ya karibu na ML. Ukifika ML opposite kuna lodge pia ila hizi ni zaidi ya 20k. Nyuma ya hii lodge nyingine kuna lodge ya 15,000 iko poa sana. Nimekueleza kutokana na hela yako.
Mrejesho: Baada ya kusoma mchango wako nilimuelekeza mgeni wangu niliekuwa namtafutia lodge kuwa akifika aitafute hii Gold so alienda na alipata chumba hapo. Shukrani sana.Fika lodge inaitwa Gold Lodge mkuu. Ni 15,000/-Tsh. Iko maeneo ya karibu na Sativa.
Hapo ndipo huwa nafikia kila nikiwa na ziara Kyela.
Iko poa sana na vyumba vyao vina space nzuri na kwa upande wa ulinzi kuko salama sana.