Hongereni sana vijana wa Simba kwa kuonyesha kwamba mmeimarika tofauti na kipindi kile mmemaliza mzunguko wa kwanza, mmecheza vizuri hasa kipindi cha pili tuseme tu kwamba bahati haikuwa upande wenu hii leo maana kucheza mechi sita ndani ya siku kumi na tatu na mkaruhusu kufungwa goli moja tu sio kitu kidogo mnahitaji pongezi.
Kuteleza si kuanguka na hata kama ukianguka haimanishi ndo umeumia kiasi kwamba huwezi kunyanyuka na kuendelea, mmeteleza na kuanguka hivyo sisi mashabiki wenu tunawambia nyanyukeni na muendelee na maandalizi ya ligi mzunguko wa pili.