Live..mdahalo shivji,kingunge...itv

kuna watu ambao hawana faida kabisa katika jamii yetu zaidi ya kutafuna rasilimali zetu tu kama huyu kigagula gobole mwitu,hana cha maana anachosaidia katika nchi hii na yupo tu bado anakula jasho letu,huwa nikimuona nahisi maumivu makali moyoni kwa jinsi ninavyomchukia

that is going to be your downfaal, or stumbling block.
Acha hasira, hapa ni kigoda cha mwalimu nyerere ana point ila tu historia yake haimlindi.
Hili sio jukwaa la kisiasa
 
Majumuisho (yanaendelea...)

2. Prof Issa G. Shivji: Mwalimu alikuwa ni kiongozi mzuri mwenye maadili. Alijaribu kusimamia mfumo japokuwa hakufanikiwa kujenga UJAMAA. Zamani kulikuwa na mabeberu ambao sasa wanaitwa "wawekezaji." Kwa sasa tunaenda kutafuta uongozi toka kwao. Tumeanza kumsaliti Mwalimu tulipoanza mfumo wa Kiliberali mamboleo, tukaleta uwekezaji. Tatizo la sasa ni mfumo. Someni Mwongozo wa CCM wa mwaka 1981 kwamba limejitokeza tabaka jipya dhidi ya Ujamaa, tabaka hilo litashinda. Hakuna Mwongozo mzuri kama huo, utafuteni muusome. Sasa tumeanza kutambua baada ya kuanza Uliberali Mamboleo, miaka 20 sasa, kwamba wakombozi wetu sio wawekezaji. Kilimo Kwanza: PM alienda Brazili, vijana wetu tumewafanya kuwa wavivu. Je, wakulima wetu tunapouza ardhi tunawapeleka wapi? Sisi tunazungumzia juu ya UTAWALA BORA, mimi sipendi UTAWALA BORA bali Azimio la Arusha lilizungumzia juu ya UONGOZI BORA. UTAWALA BORA ni wazo la World Bank. Je, utakuwa na Ubepari wa Kitaifa chini ya Ubeberu? Kuna mabadiliko makubwa ya Sheria ya Ardhi yanakuja ambayo yataleta uwekezaji...

Hapo ameongea mpaka nimetamani kwenda kuwafukuza Barrick na Tanzaniate One wezi wa rasilimali zetu
 
Hivi Kingunge mbona anafanana na wachina? Au umaxist wake umemfanya afanane na wachina?
 
Hakika kwenye Red huyo ndio the true son kama Mwalimu JK. Watanzania wajue kuwa hakuna mwingine aliyesalia anaejua kupanga namna ya kutuvusha.Yaaani hakika huyi ndie mfuasi halisi wa Mwalimu kwa maneno na kwa matendo."

Kama tunataka mfuasi wa kutuvusha kwenye mpito huu wa shaka ni huyu Mzee Pro Shvji hakika mmeona kupitia shairi alilosoma Pro Bashiru kwa niaba ya Mzee huyu.

Hakika shairi lilisomwa na Bashiru ni cheche mpya na salamu kwa watawala.

Nimepapenda sana point anamtambulisha kigogo wa siasa za CCM [Kingunge] wa Propaganda za CCM akatumia neno kisayansi tena kwa kusisitiza [Please] wenye akili zao waende kichwani.

chukua tano mkuu
 
Mbona huyu dingi sielewi anachoongea? Mhhh, namzungumzia Kingunge, eti weupe wa Mzungu ndio nguvu yake.....wakati sisi tunaendesha mambo kwa ushirikina (CCM)

wazeeeee .. hawafai kutamka kitu kwa hali ya nchi ilivyo sasa... yani kama una malaria 2... yaweza panda mpaka 40..
 
Mpwa kwa sasa nipo kwa simu, naomba kama utaweza unitumie kwene PM ili nikiwa kwa PC niucheki, natunguliza shukrani

Mpwa Elli, ukitumiwa pia niforwadie na mimi kwenye PM., niupate pia. Natanguliza shukrani .
 
Kuanzia leo nampenda kingunge, ana point na amewaachia vijana wajenge nchi kwa vitendo,
 
Comrade anasema amewashauri watawala kwenye kikao kizito kuwa watu wakubwa wa ulimwenguni esp founders, siku yao huadhimishwa tarehe waliyozaliwa na sio siku waliyokufa, amesema katika kikao hicho hakuna aliyempinga, lakini hakuna utekelezaji as usual, watu wakacheka!
 
Mpwa Elli, ukitumiwa pia niforwadie na mimi kwenye PM., niupate pia. Natanguliza shukrani .

Asante nimeona Mpwa ameshanitumia, naomba uni-PM ili niweze kukumbuka nikiwa kwenye PC nikutumie....namshukuru sana
 
Kuanzia leo nampenda kingunge, ana point na amewaachia vijana wajenge nchi kwa vitendo,
Haika, babu nilikuwa sijawahi kumpa attention yangu kama leo, yaani hadi uso umeniota kunyanzi kwa kujitahidi kumsikiliza...lol!
 
Afadhali kale kadingi kamemaliza

To be fair, mzee Kingunge amejitahidi sana. ukizingatia kwamba alikuwa amezungukwa na maprofesa wa nguvu, na kwamba historia haiko vizuri kwa upande wake, kwa kweli naweza kusema katika wazungumzaji wa CCM walioshika microphone kuongea katika kumbi za UDSM baada ya enzi za Nyerere, nadhani yeye anaweza kushika nafasi ya kwanza - na ushahidi ni kwamba hakuzomewa kwa kupigiwa makofi ya kejeli kama ambavyo imekuwa ikitokea kwa wazungumzaji kutoka CCM hapo UDSM. ameongea mambo mazito sana kwa lugha rahisi. lakini pia alikuwa cryptic, na unaweza kuelewa hilo kutokana na position yake katika CCM na serikali yake. asingeweza kutumia lugha kali zaidi ya hiyo, na ilikuwa lugha kali kwa utawala uliopo. mtu yeyote anaweza kufanya makosa, lakini ana mazuri yake. mfano wengi wetu tumezoea kusikia tu "the big Five" yaani ile mikoa inayozalisha chakula kwa wingi: Ruvuma, Iringa, Mbeya na Rukwa. sasa mzee Kingunge ameeleza jinsi alivyoshiriki kujenga hizo big five. na hata maprofesa walikubaliana naye na kuanza kujenga hoja kwamba inaonekana mkulima mdogo anaweza kuleta mabadiliko, hivyo kwa nini tena "watawala" wanatafuta wawekezaji waje kulima...mzee Kingunge hakuja pale kutetea mfumo uliopo, bali ametoa maoni yake ambayo kwa kweli ni ya kutuonesha mbele tunakotaka kwenda.
 
Back
Top Bottom