Elections 2010 Live From TV's: Upigaji wa kura, matokeo na yatokanayo

Hii ni hali halisi niliyoikuta saa 12.00 asubuhi nilipowasili kituoni:

attachment.php
 

Attachments

  • DSC00001.jpg
    DSC00001.jpg
    50.8 KB · Views: 237
Nikilinganisha na Uchaguzi wa Mwaka 2005 naona kuwa kwa muda wa saa 12.00 asubuhi waliojitokeza ni wengi.

Katika sub-vituo vyote 9 katika kituo chetu, wasimamizi wa uchaguzi walikuwepo wakati huo na askari wa kutosha: Police, Magereza na Askari wa Jiji. Hakika kwa hili wamejiandaa na wanastahili pongezi walau kwa wakati nilipowaona.


Hii ni mfano wa karatasi ya Kura ya Urais:

attachment.php
 

Attachments

  • DSC00003.jpg
    DSC00003.jpg
    27 KB · Views: 253
  • DSC00002.jpg
    DSC00002.jpg
    38.9 KB · Views: 257
  • DSC00004.jpg
    DSC00004.jpg
    27.3 KB · Views: 256
Na haya ni maelekezo kwa wapiga kura:

attachment.php
 

Attachments

  • DSC00007.jpg
    DSC00007.jpg
    51.7 KB · Views: 226
  • DSC00006.jpg
    DSC00006.jpg
    38.6 KB · Views: 220
na mimi nimetoka kupiga kura sasa.. saa kumi na mbili na robo nilikuwa kituoni huku Tegeta Bahari beach... ilipofika saa moja kamili juu ya alama watu wakaanza kuingia kupiga kura!!!!! mpaka naondoka kituoni hali ilikuwa shwari,... watu walikuwa watulivu... na askari walikuwa wametulia na kuelekeza vizuri.. hii ni taarifa mpaka naondoka kituoni... sijui yatakayojili baada ya hapo....
 
Wana JF;

Nimerejea baada ya safari ya takribani wiki mbili ili na mimi niweze kutumia vema haki yangu ya kupiga kura. Nikishapiga kura naondoka tena nikaendelee na harakati za maisha.

Nimesikia kutoka ITV kuwa watatuletea matangazo LIVE ya mchakato wote wa upigaji wa kura kutoka Studio zao mpya walizoziita Studio One (Masako na Nyangasa) na Studio Two (Gondwe). Nimeona mwonekano wa studio hizi umeboreshwa kama zile za watani wetu wa jadi. Bila ya shaka TBC1 na TV zingine nao watakuwa hewani.

Nami bila hiana nimeamua kwa hiari yangu kesho niwe mtumishi wenu. Nitaamka saa 10.30 alfajiri ili niwahi foleni ya kupiga kura na baada ya hapo nirejee kwenye laptop yangu kwa ajili ya kuwaletea kinachojiri toka nitakaporejea.

Najua wengi mtapata fursa ya kusikia matangazo, kwa hiyo tutasaidiana kuposti.

Natoa wito wote tuhamasishane kwenda kupiga kura na kuwachagua viongozi ambao watatutumikia katika kipindi cha miaka 5 ijayo.

Stay tuned!

Thanx Superman...Hope hii itaendelea mpaka watakapoanza kutoa matokeo....Mungu akupe Afya na nguvu...Kila la kheri...
 
So far Hali ikoje??? Hasa maeneo ya Buguruni (Sheli, Mnyamani, Madenge,Rozana, Ghana na Malapa??)
 
Nilipiga Kura yangu saa 1.30 asubuhi nikiwa mtu wa 5.

Uhakiki wa wapiga kura unachua muda:

Ofisa wa Kwanza wa NEC anapokea kadi ya mpiga kura na kuangalia kama jina lako lipo.

Ofisa wa pili anaangalia kama uko katika daftari ya wapiga kura. Akiona jina anaoanisha na picha na kisha mawakala wa vyama nao wanashuhudia. Baada ya hapo anasoma namba yako na niliona mawakala wa CUF, CCM na CHADEMA wananakili namba ya mpiga kura.

Baada ya hapo unaenda kwa msimamizi wa kituo, anakagua kadi yako na kisha anaisoma kwa sauti na mawakala wanahakiki. Kisha anakupa karatasi tatu. Ya blue nyuma - Urais, Nyeusi nyuma - Ubunge na nyeupe nyuma - Madiwani. Anazikunja na kisha kugonga mihuri miwili kwa nyuma katika kila karatasi. Kisha anakupatia.

Kisha unaenda katika sehemu iliyoandaliwa kupiga kura kuna pen hapo, unakunjua karatasi zako na kuweka vema kwa mgombea unayemtaka na kisha unazikunja.

Ukimaliza: Blue-Urais unatumbukukiza katika sanduku la kura za Rais, Black-sanduku la Ubunge na Nyeupe sanduku la mwadiwani.

Ukimaliza hapo kuna mdau wa NEC anakupaka wino katika kidole kidogo kisha unaondoka.
 
Wana JF;

Nimerejea baada ya safari ya takribani wiki mbili ili na mimi niweze kutumia vema haki yangu ya kupiga kura. Nikishapiga kura naondoka tena nikaendelee na harakati za maisha.

Nimesikia kutoka ITV kuwa watatuletea matangazo LIVE ya mchakato wote wa upigaji wa kura kutoka Studio zao mpya walizoziita Studio One (Masako na Nyangasa) na Studio Two (Gondwe). Nimeona mwonekano wa studio hizi umeboreshwa kama zile za watani wetu wa jadi. Bila ya shaka TBC1 na TV zingine nao watakuwa hewani.

Nami bila hiana nimeamua kwa hiari yangu kesho niwe mtumishi wenu. Nitaamka saa 10.30 alfajiri ili niwahi foleni ya kupiga kura na baada ya hapo nirejee kwenye laptop yangu kwa ajili ya kuwaletea kinachojiri toka nitakaporejea.

Najua wengi mtapata fursa ya kusikia matangazo, kwa hiyo tutasaidiana kuposti.

Natoa wito wote tuhamasishane kwenda kupiga kura na kuwachagua viongozi ambao watatutumikia katika kipindi cha miaka 5 ijayo.

Stay tuned!


ITV kweli wanafanya kweli! Nawapa BIG-UP kwa sana! Yaani matokeo yanakuja live, kituo kwa kituo, TANZANIA NZIMA! Picha ni za Dar es Salaam, lakini wanaongea kwa njia ya simu. Safi sana! HII ndio maana halisi ya TEKNOHAMA!

Hongereni sana ITV!
 
Back
Top Bottom