Superman
JF-Expert Member
- Mar 31, 2007
- 5,695
- 1,696
Wana JF;
Nimerejea baada ya safari ya takribani wiki mbili ili na mimi niweze kutumia vema haki yangu ya kupiga kura. Nikishapiga kura naondoka tena nikaendelee na harakati za maisha.
Nimesikia kutoka ITV kuwa watatuletea matangazo LIVE ya mchakato wote wa upigaji wa kura kutoka Studio zao mpya walizoziita Studio One (Masako na Nyangasa) na Studio Two (Gondwe). Nimeona mwonekano wa studio hizi umeboreshwa kama zile za watani wetu wa jadi. Bila ya shaka TBC1 na TV zingine nao watakuwa hewani.
Nami bila hiana nimeamua kwa hiari yangu kesho niwe mtumishi wenu. Nitaamka saa 10.30 alfajiri ili niwahi foleni ya kupiga kura na baada ya hapo nirejee kwenye laptop yangu kwa ajili ya kuwaletea kinachojiri toka nitakaporejea.
Najua wengi mtapata fursa ya kusikia matangazo, kwa hiyo tutasaidiana kuposti.
Natoa wito wote tuhamasishane kwenda kupiga kura na kuwachagua viongozi ambao watatutumikia katika kipindi cha miaka 5 ijayo.
Stay tuned!
Nimerejea baada ya safari ya takribani wiki mbili ili na mimi niweze kutumia vema haki yangu ya kupiga kura. Nikishapiga kura naondoka tena nikaendelee na harakati za maisha.
Nimesikia kutoka ITV kuwa watatuletea matangazo LIVE ya mchakato wote wa upigaji wa kura kutoka Studio zao mpya walizoziita Studio One (Masako na Nyangasa) na Studio Two (Gondwe). Nimeona mwonekano wa studio hizi umeboreshwa kama zile za watani wetu wa jadi. Bila ya shaka TBC1 na TV zingine nao watakuwa hewani.
Nami bila hiana nimeamua kwa hiari yangu kesho niwe mtumishi wenu. Nitaamka saa 10.30 alfajiri ili niwahi foleni ya kupiga kura na baada ya hapo nirejee kwenye laptop yangu kwa ajili ya kuwaletea kinachojiri toka nitakaporejea.
Najua wengi mtapata fursa ya kusikia matangazo, kwa hiyo tutasaidiana kuposti.
Natoa wito wote tuhamasishane kwenda kupiga kura na kuwachagua viongozi ambao watatutumikia katika kipindi cha miaka 5 ijayo.
Stay tuned!