Mnama
JF-Expert Member
- Oct 13, 2010
- 3,225
- 3,180
Jamani mke wangu haniamini kabsaaa. Nikienda ofisini nikachelewa kurudi anaamini nilikuwa kwa mademu. Nikichelewa ananifanyia suprise anakuja office bila taarifa ananikuta tena peke yangu, lakini bado haniamini. Hali hiyo imedumu kwa miaka mingi sana mpaka naona nimefika mwisho siwezi ivumilia. Issue inaanzania mbali kidogo, wakati bado sijamuoa aliwahi kunikuta na daftari la mshikaji wangu ambaye miandiko yetu inafanana. Hilo daftari jamaa alikuwa kaorodhesha mademu wote aliotembea nao. Sasa kulikuwa na column tatu NAMBA, JINA, na HALI. kwa mfano: NAMBA 1, JINA: Jenifa Kalalu, HALI: tight. Sasa idadi ilikuwa inafika 94 mpaka wakati huo. Wife anaamini list ilikuwa yangu, na kwenye list hiyo kulikuwa na majina ya watu wa karibu yake. Kila tukigombana ananitusi kuwa mie malaya sana na anauliza kuwa list yangu wamefika wangapi. Sasa mi naumia sana!! Ishu ya miaka kama 10 iliyopita halafu sio daftari langu lakini anafanya ndio reference kila tunapokwaruzana. Sasa sijui hata nimfanyeje??
Duu duniani kuna mambo why keep the list ? Kaa chini ongea na Mkeo kwamba hata kama list ni yako that was back then now you with her and her alone na mweleze katika list yako she was the best above all ndio maana ukamchagua awe mkeo,she better trust you or else atembee mbele maana kundelea kukutuhumu kwa mambo ya miaka kumi iliyopita haina maana na bado anaendelea kuishi na wewe. BTW kwani ye ulimkuta bikra ?