MBUNGE wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA), amesema kuwa kuna haja ya Watanzania kuungana ili kuzuia mbinu chafu za Chama cha Mapinduizi (CCM) za kugeuza nchi kuwa dola ya kipolisi.
Lissu alisema hayo mwishoni mwa wiki kwenye mkutano wa hadhara wa CHADEMA uliofanyika kwenye viwanja vya kata ya Majengo, Manispaa ya Moshi, mkoani Kilimanjaro.
Akizungumza kwenye mkutano huo, Lissu alisema yanayoendelea kutokea Tarime ni mfano mzuri kuwa lengo la CCM ni kuigeuza Tanzania dola ya kipolisi baada ya Rais Jakaya Kikwete na chama chake kushindwa kuongoza kwa hoja.
Watanzania tusilifumbie macho suala la Tarime kwa sababu yanayotokea yanatuhusu sisi sote na mwisho ya siku yatahamia katika mikoa mingine kutokana na mipango inayofanywa na CCM kuhakikisha kuwa majimbo ambayo CHADEMA inapendwa yanachukiwa na ikiwezekana kuwaua watu bila sababu, alisema Lissu.
Tunachotaka ni kuzuia nchi hii isiweze dola ya kipolisi maana ndio agenda yao pekee iliyobaki, kuwapa polisi uhuru wa kuwaua raia,kuwatesa na kujeruhi,alisisitiza.
Alisema wananchi hawatakiwi kukaa kimya pindi wanapoona mamlaka yanatumiwa vibaya wananchi wenye ambao ndo wenye mali wana haki ya kuichukua tena mamlaka yao.
Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Moshi, Japhary Michael alisema kuwa Rais anatakiwa kuwachulia hatua viongozi wanaokuwa kikwazo kwenye maendeleo ya nchi, huku akitolea mfano jitihada za CHADEMA kwenye suala la elimu bure kwa wananchi ambalo limekuwa likiwekewa vikwazo.
Source: Tanzania Daima
Lissu: Yanayotokea Tarime mpango wa CCM
Lissu alisema hayo mwishoni mwa wiki kwenye mkutano wa hadhara wa CHADEMA uliofanyika kwenye viwanja vya kata ya Majengo, Manispaa ya Moshi, mkoani Kilimanjaro.
Akizungumza kwenye mkutano huo, Lissu alisema yanayoendelea kutokea Tarime ni mfano mzuri kuwa lengo la CCM ni kuigeuza Tanzania dola ya kipolisi baada ya Rais Jakaya Kikwete na chama chake kushindwa kuongoza kwa hoja.
Watanzania tusilifumbie macho suala la Tarime kwa sababu yanayotokea yanatuhusu sisi sote na mwisho ya siku yatahamia katika mikoa mingine kutokana na mipango inayofanywa na CCM kuhakikisha kuwa majimbo ambayo CHADEMA inapendwa yanachukiwa na ikiwezekana kuwaua watu bila sababu, alisema Lissu.
Tunachotaka ni kuzuia nchi hii isiweze dola ya kipolisi maana ndio agenda yao pekee iliyobaki, kuwapa polisi uhuru wa kuwaua raia,kuwatesa na kujeruhi,alisisitiza.
Alisema wananchi hawatakiwi kukaa kimya pindi wanapoona mamlaka yanatumiwa vibaya wananchi wenye ambao ndo wenye mali wana haki ya kuichukua tena mamlaka yao.
Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Moshi, Japhary Michael alisema kuwa Rais anatakiwa kuwachulia hatua viongozi wanaokuwa kikwazo kwenye maendeleo ya nchi, huku akitolea mfano jitihada za CHADEMA kwenye suala la elimu bure kwa wananchi ambalo limekuwa likiwekewa vikwazo.
Source: Tanzania Daima
Lissu: Yanayotokea Tarime mpango wa CCM