Lissu: Wanaotaka kuondoka CHADEMA ruksa

Lissu: Wanaotaka kuondoka CHADEMA ruksa

Hii nchi ina watu waoga sana duh...

Mleta mada asante kwa hiyo picha ya kamanda Lissu uliyotumia
 
angekuwa na nia ya dhati angeyasema haya mapema.. tafuteni sababu nyingine...

mie nawatakia kila lakheri kwenye safari yenu ya matumaini... nitakuwa sehemu ya mabadiliko kwa namna nyingine.. sio kila kitu nishabikie maana tumeembiwa wengine nikinani wakati maprof madr wabunge ,kamati kuu wanajua zaidi wameshakubali wengine ni kinani kupinga huu uamuzi muhimu ni kukaa kando kutizama mchezo tu..wenye chama washaa amua...


Mkuu kuwa mpole, ulitaka aseme ukweli upi kwa kipindi kile, tafakari zaidi hayo alafu utapata jibu


Usiwe na jazba tunachohitaji ni kuiondoa ccm tu
 
Sijuwi nimemfahamu Lissu au vipi, inamana Lowassa atakuwa rais wa Ukawa??? itakuwaje kwenye kampeni ccm wakileta documents japo za kughushi kuhusu ufisadi kwa Lowassa?? na je Ukawa itapambana vipi na ufisadi ilhali Rais atakayesimamishwa kama ni Lowassa alishawahi kunaswa na harufu ya ufisadi?

Ukawa itakuwa na nguvu gani kupambana na hili na vipi bungeni wataweza kusimama tena kupinga ufisadi? Lissu ningependa zaidi angeogelea kwenye haya.

La maana hapa CCM itakua imeng'ooka, mengine kama ni marekebisho yatafuata.
 
Ondoka tu ndugu kwani hakuna namna nyingine, utauachaje mtaji mkubwa kiasi hicho? Mabadiliko ni hatua. Huo ni uhuru wako lakini ukirudi CCM utakuwa umepoteza zaidi.

Ni kweli Mkuu, unafiki wa kumkubali Lowasa utanitesa sana,
Slaa anafunga maombi ya toba
 
Sijuwi nimemfahamu Lissu au vipi, inamana Lowassa atakuwa rais wa Ukawa??? itakuwaje kwenye kampeni ccm wakileta documents japo za kughushi kuhusu ufisadi kwa Lowassa?? na je Ukawa itapambana vipi na ufisadi ilhali Rais atakayesimamishwa kama ni Lowassa alishawahi kunaswa na harufu ya ufisadi?

Ukawa itakuwa na nguvu gani kupambana na hili na vipi bungeni wataweza kusimama tena kupinga ufisadi? Lissu ningependa zaidi angeogelea kwenye haya.

Mkuu hapa cha msingi ni kwa vipi ccm watazileta hizo documents fake..maana watakuwa wanajivua nguo wenyewe na kutembea uchi..kwa nn hawakumpeleka mahakamani? Suala hapa ni credibility ya maccm kwa wananchi..kipi watakachoongea wananchi watakiamini wakati wao wenyewe ni mafisadi wa kutupwa na wamethibitisha hivyo toka 2008 alipojiuzulu EL..ufisadi umeongezeka mara dufu..ni mjinga tu atakayewaamili hata wakija na mlima wa madocuments..haitasaidia..its too late I guess! Jiandikisheni wananchi..tuwatoe wajinga hawa!
 
TUNDU-LISSU-SEP-06-620x307.jpg



MBUNGE wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu, amesema chama chao kinatarajia kupata wanachama wengi baada Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa kujiunga na chama hicho.

Lissu ametoa kauli hiyo baada ya kuwepo taarifa kwamba wapo wanachama wa Chadema ambao watakihama chama hicho kutokana na kutokubaliana na ujio wa Lowassa ndani ya Chadema.

Akizungumza leo na waandishi wa habari Lissu amesema, “Kama wapo watakao jiondoa Chadema, wengi zaidi watakuja. Tupo katika kipindi ambacho hatujawahi kuwepo tangu mfumo wa vyama vingi uanze.

Mfumo tawala unabomoka vipande vipande. Unapo bomoka, dalili zake ni watu ambao wamekuwa katika mfumo huo kuondoka kama alivyofanya Lowassa.”

“Mabadiliko katika nchi yanatokea pale mfumo tawala unapo pasuka. Lowassa ni mfano mzuri.

Tunamkaribisha kwetu sio kwa sababu ni mwanasiasa msafi. Tumempokea kwa sababu tunaongeza nguvu kubwa kwa wale wanaotaka mabadiliko. Imetokea Zambia Mawawi, Nigeria na Kenya,” amesema Lissu.

Akizungumza kuhusu Chadema kumtuhumu Lowassa kwamba “ni fisadi” kabla ya kujiunga na chama hicho Lissu amesema, “…hatukuwa na makosa hata kido kumweka Lowassa katika kundi la watuhumiwa wa Richmond. Mambo yalizungumzwa bungeni. Aliwajibika na amesema mwenyewe aliwajibika.”

“Alijiuzuru uwaziri mkuu kwa sababu ya Richmond. Tulimweka katika orodha ya mafisadi kwa sababu ya Richmond. Na jana alisema alimwambia rais “tuvunje mkataba” rais akaataa. Angefanyeje?. hilo ni vumbi, litakapo tulia Chama Cha Mapinduzi na mfumo tawala utakuwa umeanguka, tutajenga nchini.Bila kuvunja mfumo tawala hakuna kusonga mbele,” ameeleza Lissu.

Lissu kwenye ubora wake MTAKOMA KURINGA WANOKO.
 
Sawa bakini na chama chenu,

Lakin Lissu kaa ukijua kile ni chama cha kina Mbowe na jana alisema tena usijione umefika
Kwa hiyo zile mil 300+ alizosema Slaa pia alishawajibika?

toka lini ulikua chadema? Mnalo mwaka huu.
 
wanaoona ujio wa lowasa ni tatizo sio mbaya kama wakiondoka kimya kimya waende wanakoamini kuna asali na maziwa
 
Leo Tundu anamsafisha fisadi. Halafu tunampongeza kama mazuzu vile. Kweli akili zeti zimeshikwa.
 
Sijuwi nimemfahamu Lissu au vipi, inamana Lowassa atakuwa rais wa Ukawa??? itakuwaje kwenye kampeni ccm wakileta documents japo za kughushi kuhusu ufisadi kwa Lowassa?? na je Ukawa itapambana vipi na ufisadi ilhali Rais atakayesimamishwa kama ni Lowassa alishawahi kunaswa na harufu ya ufisadi?

Ukawa itakuwa na nguvu gani kupambana na hili na vipi bungeni wataweza kusimama tena kupinga ufisadi? Lissu ningependa zaidi angeogelea kwenye haya.



Hayo ccm hawatathubu maana maswali yote itabidi wayajibu wao

Kumbuka lowassa jana alisema nn

Kama una ushahidi nenda mahakamani, ana amini anachokiongea

Ngoma inogileee
 
Back
Top Bottom