kochakindo
JF-Expert Member
- Nov 3, 2014
- 784
- 531
nakushukuru lissu
![]()
MBUNGE wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu, amesema chama chao kinatarajia kupata wanachama wengi baada Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa kujiunga na chama hicho.
Lissu ametoa kauli hiyo baada ya kuwepo taarifa kwamba wapo wanachama wa Chadema ambao watakihama chama hicho kutokana na kutokubaliana na ujio wa Lowassa ndani ya Chadema.
Akizungumza leo na waandishi wa habari Lissu amesema, Kama wapo watakao jiondoa Chadema, wengi zaidi watakuja. Tupo katika kipindi ambacho hatujawahi kuwepo tangu mfumo wa vyama vingi uanze.
Mfumo tawala unabomoka vipande vipande. Unapo bomoka, dalili zake ni watu ambao wamekuwa katika mfumo huo kuondoka kama alivyofanya Lowassa.
Mabadiliko katika nchi yanatokea pale mfumo tawala unapo pasuka. Lowassa ni mfano mzuri.
Tunamkaribisha kwetu sio kwa sababu ni mwanasiasa msafi. Tumempokea kwa sababu tunaongeza nguvu kubwa kwa wale wanaotaka mabadiliko. Imetokea Zambia Mawawi, Nigeria na Kenya, amesema Lissu.
Akizungumza kuhusu Chadema kumtuhumu Lowassa kwamba ni fisadi kabla ya kujiunga na chama hicho Lissu amesema, hatukuwa na makosa hata kido kumweka Lowassa katika kundi la watuhumiwa wa Richmond. Mambo yalizungumzwa bungeni. Aliwajibika na amesema mwenyewe aliwajibika.
Alijiuzuru uwaziri mkuu kwa sababu ya Richmond. Tulimweka katika orodha ya mafisadi kwa sababu ya Richmond. Na jana alisema alimwambia rais tuvunje mkataba rais akaataa. Angefanyeje?. hilo ni vumbi, litakapo tulia Chama Cha Mapinduzi na mfumo tawala utakuwa umeanguka, tutajenga nchini.Bila kuvunja mfumo tawala hakuna kusonga mbele, ameeleza Lissu.
Ahsante sana Lissu. Mungu akubariki sana.
Mwanaccm yeyote inatakiwa wamweshimu Lowassa kwani ameteseka kwa miaka kumi. Kama angeyasema haya anayoyasema Leo sidhani kama hao akina nape na wengine wangekuwepo ccm. Kikwete asingekuwa madarakani inamana uchaguzi ungefanyika. Lakini alivumilia kwa kuilinda serikali na chama chake ccm. Ni wachache sana ambao watamwelewa lkn Kikwete mwenyewe anajua na ipo siku tutasimuliwa haya. Lowassa anayo haki ya kuhama chama mwacheni. CCM wafanye siasa za kistarabu ili hata kama wanarudi madarakani warudi kwa haki. Na kama Upinzani wanachukua madaraka wachukue kwa haki kwani wote ni Watanzania na Tanzania ni yetu sote
Safi sana Lissu.... Tena waondoke haraka sana, sio kupiga kelele tu hapa
Mkuu hapa cha msingi ni kwa vipi ccm watazileta hizo documents fake..maana watakuwa wanajivua nguo wenyewe na kutembea uchi..kwa nn hawakumpeleka mahakamani? Suala hapa ni credibility ya maccm kwa wananchi..kipi watakachoongea wananchi watakiamini wakati wao wenyewe ni mafisadi wa kutupwa na wamethibitisha hivyo toka 2008 alipojiuzulu EL..ufisadi umeongezeka mara dufu..ni mjinga tu atakayewaamili hata wakija na mlima wa madocuments..haitasaidia..its too late I guess! Jiandikisheni wananchi..tuwatoe wajinga hawa!