Ndyali
JF-Expert Member
- Nov 24, 2011
- 1,678
- 971
Po
leo katika vyombo vya habari, wakili wa kujitegemea na Diwani wa Kata ya Mabogini (cdm) ametoa kasoro za kisheria kwa Mwanasheria Mkuu wa cdm juu ya hukumu ya kitila mkumbo na zitto kabwe. Msando alisema katiba ya cdm inaeleza kuwa kiongozi yeyote hatachukuliwa hatua za kinidhamu kabla ya kupewa mashtaka kwa maandishi na mamlaka husika na kupewanafasi ya kujibu mashtaka hayo kwa maandishi, mwisho wa kunukuu.
napenda kumwambia Msando akasome katiba ya cdm vizuri hicho kifungu anachosema ni kwa viongozi yeyote wale wa kuchaguliwa, wa mabaraza, wenyeviti wastaafu, wawakilishi wa madiwani na wabunge ndio inawapaswa kufanya ivyo na sio wajumbe wa kuteuliwa kama wakina Kitila MKUMBO. kifungu ambacho kinawapa mamlaka ya kuwavua nyazifa ni hiki hapa.
7.7.16 Kazi za Kamati Kuu zitakuwa:-
(v) Kumwachisha ujumbe wa Kamati Kuu mjumbe mteule ambaye ataenda kinyume nakatiba, kanuni na maadili au kushindwa kukidhi matakwa ya kuteuliwa kwake.
Mkuu hapa kwenye (V), Tueleweshane vizuri, Kamati kuu in mamlaka ya kumvua uongozi mwanachama kwa KAMATI hi pekee au hata kwa kamati nyingine zote???
Binafsi mimi naona hiki kifungu ni kwa ajili ya Wajumbe wa kamati kuu tu!! Je kuhusu Wajumbe wa kamati nyingine CC pia inaweza kuwaachisa uongozi??
Fafanua vizuri ili twende kazi!!!
Mkuu Manyi,Michango yako humu inatudhalilisa watu wa Mbozi, acha kujitoa ufahamu.