Stroke
JF-Expert Member
- Feb 17, 2012
- 34,736
- 41,062
Lissu ni Dikteta kwa kuwa anamshawishi Rais Samia kutozingatia utawala bora na kuingilia mihimili mingine.
Lissu anataka Samia avunje Ibara ya 62 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuingilia Bunge la JMT kwa kuwaondoa wabunge wanaowawakilisha wananchi tena jambo baya zaidi wabunge hao ni wa chama cha upinzani ambao Rais hana mamlaka nao kwani yeye anatoka chama kingine.
Lissu anataka Rais Samia avunje Ibara ya 107A na 107B ya katiba kwa kuingilia uhuru wa mahakama pale alipomtaka Rais kufuta kesi ya Mbowe.
Kwa kufanya hivyo Rais atakuwa ameingilia Mhimili wa Mahakama ambao upo katika mchakato wa kutoa maamuzi kuhusiana na suala la Mbowe.
Inasikitisha mno kwamba Lissu kama kiongozi wa Chama Cha Upinzani anahimiza matendo ya uvunjifu wa katiba wazi wazi tena akiwa mtaalam wa sheria.
Lissu anafanya yote haya akiwa hana mamlaka.
Je akiyapata? Nina imani kabisa kabisa kwamba endapo mtu kama huyu akipewa mamlaka tutashuhudia uvunjifu mkubwa wa katika kuwahi kutokea katika historia ya Taifa letu.
Ni hitimishe kwa kusema kwamba Lissu ametukosea sana watanzania kwa kuweka pembeni taaluma yake ya sheria kwa kuhimiza matendo ya uvunjifu wa katiba wazi wazi.
Watu wa aina hii hawapaswi kuaminiwa kupewa mamlaka ya nchi.
Lissu anataka Samia avunje Ibara ya 62 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuingilia Bunge la JMT kwa kuwaondoa wabunge wanaowawakilisha wananchi tena jambo baya zaidi wabunge hao ni wa chama cha upinzani ambao Rais hana mamlaka nao kwani yeye anatoka chama kingine.
Lissu anataka Rais Samia avunje Ibara ya 107A na 107B ya katiba kwa kuingilia uhuru wa mahakama pale alipomtaka Rais kufuta kesi ya Mbowe.
Kwa kufanya hivyo Rais atakuwa ameingilia Mhimili wa Mahakama ambao upo katika mchakato wa kutoa maamuzi kuhusiana na suala la Mbowe.
Inasikitisha mno kwamba Lissu kama kiongozi wa Chama Cha Upinzani anahimiza matendo ya uvunjifu wa katiba wazi wazi tena akiwa mtaalam wa sheria.
Lissu anafanya yote haya akiwa hana mamlaka.
Je akiyapata? Nina imani kabisa kabisa kwamba endapo mtu kama huyu akipewa mamlaka tutashuhudia uvunjifu mkubwa wa katika kuwahi kutokea katika historia ya Taifa letu.
Ni hitimishe kwa kusema kwamba Lissu ametukosea sana watanzania kwa kuweka pembeni taaluma yake ya sheria kwa kuhimiza matendo ya uvunjifu wa katiba wazi wazi.
Watu wa aina hii hawapaswi kuaminiwa kupewa mamlaka ya nchi.