Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 57,103
- 128,723
Wanabodi,
Mungu na Shetani
Hiii ni moja ya Mada zangu za holistic approach zinazotumia dhana dhanifu ya Mungu na shetani。
Hii ni mada fikirishi.
Outline.
JF ni ukumbi huru wa kuhabarishana, kuelimishana, kuburudishana, na kitu kikubwa zaidi, kusaidiana. Kama kuna kitu unakijua, na unaona kinafanyika ndivyo sivyo, unajitolea kusaidia kuwaelimisha wengine kuhusu kitu hicho, na hiki ndicho mimi ninachofanya humu JF, kuwaelimisha wengine kile nilichobahatika kukifahamu, na elimu hii naitoa humu jf, kupitia makala zangu za kwa Kwa Maslahi ya Taifa, ambazo pia zinachapishwa kwenye magazeti ya Mwananchi na Nipashe, kila Jumatano na Jumapili na pia zinakwenda sambamba na kipindi cha TV cha jina hilo hilo la KMT, kinachoruka kila Jumapili saa 3:00 usiku na Jumatano saa 9:30 alasiri on Channel Ten
Declaration of Interest
Mimi ni kada wa chama cha siasa, ila ninapoandika hapa, siandiki kama kada, bali naandika kama Mtanzania Mzalendo, ambaye ni mwandishi wa habari aliyehudumu newsroom kwa zaidi ya miaka 30, na pia ni mwanasheria na wakili wa kujitegemea, hivyo ukinisoma with preconceived opinions kuwa huyu ni kada wa chama fulani, hutaweza kuiona the rationale behind bandiko hili, na elimu ninayoitoa, hivyo nakushauri bora uishie hapa.
3. Holistic Approach
Mada ya leo, japo ni mada ya kisiasa,lakini naijadili kwa mtindo wa holistic approach kwa kutumia dhana dhanifu ya Mungu na Shetani。Kila kinachotokea duniani, jambo lolote, ni ama ni mpango wa Mungu ama ni mpango wa Shetani.
4. Mungu na Shetani ni nani na wako wapi.
Kwa vile vyama vya siasa ni public parties, viongozi wa vyama, mna wajibu wa kuviendesha vyama vyenu kwa kutanguliza mbele maslahi ya umma na sio maslahi binafsi ya viongozi wenu, msiruhusu ignorance, insanity, selfishness na utumishi wa shetani kwa baadhi ya viongozi wenu wabinafsi, kuviangamiza vyama vyenu kwa ignorance, insanity, selfishness yao, na mpango wa shetani wakati miongoni mwenu sio wote mko insane.
ila inawezekana hii no reforms no election ni mpango wa Mungu kwa Tanzania anao letwa kwa mtindo wa blessing in disguise,ili hizo reforms ziondoe ule ushetani uliofanywa kwenye katiba yetu,hivyo Chadema ni mpango wa Mungu na Tundu Lissu ni mpango wa Mungu kuwakomboa Watanzania kurejeshewa haki zao。
Kipimo cha mwisho NRNE na Tundu Lissu kama ni mpango wa Mungu au wa shetani,tutakipima kwa performance and the end justifies the means,kama NRNE ni mpango wa Mungu,then Mungu atatenda,reforms zitafanyika kabla ya uchaguzi na tutafanya uchaguzi huru kweli na wa haki kweli na kama kusipofanyika reforms,uchaguzi haitafanyika, sio Tundu Lissu, Chadema na wafuasi wao kukinukisha,bali kwa Mungu Baba muweza wa yote kufanya kitu kitakachofanya uchaguzi usifanuike!。
Kama NRNE,ni mpango wa shetani,hakutafanyika reforms zozote,na uchaguzi utafanyika kama kawaida,huo mpango haramu wa kuzuia uchaguzi mkuu usifanyike,utashindwa!, mipango ovu ya maajenti wa shetani,washindwe na walegee!
Mungu Ibariki Tanzania!
Nawatakia Jumatatu Njema na mapumziko mema ya Karume Day。
Paskali
Mungu na Shetani
Hiii ni moja ya Mada zangu za holistic approach zinazotumia dhana dhanifu ya Mungu na shetani。
Hii ni mada fikirishi.
Outline.
- Utangulizi
- Declaration of Interest
- Holistic Approach
- Mungu na Shetani ni nani na wako wapi.
- Mpango wa Mungu na Mpango wa Shetani.
- No Reform No Election ni Mpango wa Mungu au Shetani?.
- Tundu Lissu ni Mpango wa Mungu au ni Ajent wa Shetani?
- Msingi Mkuu wa Nchi Yetu ni Katiba na Inapata Mamlaka kutoka kwa Wananchi
- Haki Mbili Kuu za Kikatiba,Kuchagua na Kuchaguliwa,zimeporwa Kishetani!Reforms Zitazirejesha!。
- Vyama vya Siasa Tanzania ni Public Parties Lazima Vitangulize Mbele Public Interests
- Baadhi ya Viongozi wa Vyama vya Siasa Sio Tu ni Insane Bali Baadhi ni Ma Ajent wa shetani!
- Insanity Inawapataje Viongozi wa Siasa?..
- Mtu Kuwa Insane Sio Kosa, ni Hali Tuu, Lakini Kikundi cha Watu, Chama, Kikao au Wanachama Wote Kukubali Kufuata Ushauri wa Isane, Wote Mtaonekana Insane!.
- Je Kila Uamuzi wa Kugomea Jambo au Kususia Kitu ni Ujinga, Insane ?
- Hitimisho
JF ni ukumbi huru wa kuhabarishana, kuelimishana, kuburudishana, na kitu kikubwa zaidi, kusaidiana. Kama kuna kitu unakijua, na unaona kinafanyika ndivyo sivyo, unajitolea kusaidia kuwaelimisha wengine kuhusu kitu hicho, na hiki ndicho mimi ninachofanya humu JF, kuwaelimisha wengine kile nilichobahatika kukifahamu, na elimu hii naitoa humu jf, kupitia makala zangu za kwa Kwa Maslahi ya Taifa, ambazo pia zinachapishwa kwenye magazeti ya Mwananchi na Nipashe, kila Jumatano na Jumapili na pia zinakwenda sambamba na kipindi cha TV cha jina hilo hilo la KMT, kinachoruka kila Jumapili saa 3:00 usiku na Jumatano saa 9:30 alasiri on Channel Ten
Declaration of Interest
Mimi ni kada wa chama cha siasa, ila ninapoandika hapa, siandiki kama kada, bali naandika kama Mtanzania Mzalendo, ambaye ni mwandishi wa habari aliyehudumu newsroom kwa zaidi ya miaka 30, na pia ni mwanasheria na wakili wa kujitegemea, hivyo ukinisoma with preconceived opinions kuwa huyu ni kada wa chama fulani, hutaweza kuiona the rationale behind bandiko hili, na elimu ninayoitoa, hivyo nakushauri bora uishie hapa.
3. Holistic Approach
Mada ya leo, japo ni mada ya kisiasa,lakini naijadili kwa mtindo wa holistic approach kwa kutumia dhana dhanifu ya Mungu na Shetani。Kila kinachotokea duniani, jambo lolote, ni ama ni mpango wa Mungu ama ni mpango wa Shetani.
4. Mungu na Shetani ni nani na wako wapi.
5, Mpango wa Mungu na Mpango wa Shetani.Dhana ya Mungu na shetani ni dhana dhanifu kuwa Mungu ndie mmumba wa dunia hii na vyote vilivyomo, msaidizi mkuu wa Mungu ni malaika mkuu Lusiferi, akaasi kwa kutaka kupoka madaraka na mamlaka ya Mungu kwa na yeye kutaka kuabudiwa, hivyo kukatokea vita kati ya Mungu na malaika watiifu na shetani na malaika waasi, Mungu akashinda, shetani akashindwa, shetani na malaika waasi wakafukuzwa peponi na kutupwa motoni.
Japo dini nyingi zinawafundisha watu Mungu anakaa mbinguni na peponi, na shetani anakaa kuzimu na motoni, ukweli ni kwamba wote wawili, Mungu na shetani ni Omnipotent, wana nguvu za kufanya kila kitu ila nguvu za Mungu ni kubwa zaidi za shetani. Omniscience, (wana jua kila kitu ), ni Omnipresent (wako popote).
Ile siku Mungu anatuumba, ile pumzi ya uhai aliotupulizia, ina Uungu ndani yake, hivyo kila binadamu hai, ana Mungu ndani yake na ana nguvu za Mungu, na shetani pia yupo ana taka kuchukua nafasi ya Mungu. Hivyo kila binadamu ana miili miwili, mwili wa nyama (physical body) na mwili wa roho (spiritual body), na ndunia hii tunayoishi kuna ulimwengu wa mwili (physical world), na ulimwengu wa roho, (spiritual body), hivyo mbinguni na peponi ni hapa hapa duniani, kwenye ulimwengu wa roho!.
6. No Reform No Election ni Mpango wa Mungu au Shetani.Mpango wa Mungu kwenye kumuumba binadamu ni ili amche Mungu na kutenda yalio mema, mambo yote mema na mazuri ya kheri ni mpango wa Mungu, na mambo yote mabaya, majanga na dhambi ni mpango wa shetani.
Mungu ndie huweka serikali za mataifa hivyo viongozi wote wa nchi ni mpango wa Mungu, hivyo viongozi wanapaswa kuwaza, kusema na kutenda mema,viongozi wanapotenda maovu kwa nchi na wananchi wake,japo ni watu wa Mungu,wanakuwa wamegeuka ni ma agenti wa shetani!
Kuna wakati Mungu anarumruhusu shetani kutenda mambo mabaya, kuleta majanga, hadi vifo, ambayo tunaita ni mapito,majaribu na mitihani ya Mwenyezi Mungu ili kukupima umesimamaje kukupitisha kwenye tanuru la moto kukuimarisha kukuandaa kwa majukumu makubwa zaidi, hivyo jambo lolote zuri au baya likitokea, japo linasababishwa na shetani, tunatakiwa kushukuru Mungu kwa yote kwasababu Mungu ndie Alfa na Omega, ameruhusu hayo yatokee.
Mfano lile la Ayubu, au Yesu kujaribiwa na shetani, inawezekana hata mapito ya Lissu,ni mpango wa Mungu kuonyesha utukufu wake!
Kuna wakati Mungu anaifanya mioyo ya watu iwe migumu ili kudhihirisha utukufu wake kama Nabii Mussa na Farao, na kuna wakati, Mungu anaacha mambo mabaya yakukute ili kuja kudhihirisha utukufu wake, kama kusulubiwa kwa Masiha.
Kuna wakati Mungu anaruhusu viongozi wetu kutenda mambo ya kishetani,na bado akawabariki,kama King David alipomtamani mke wa Uria,akamuua Uria na kumtwaa mke wake,Beersheba,na kumfanya mkewe,huyu ndie mama wa Sulemani.
7. Je Tundu Lissu ni Mpango wa Mungu au ni Ajent wa Shetani?Inawezekana hii No Reform No Election ni mpango wa Mungu kwa Tanzania kutupatia ukombozi wa pili wa Mtanzania kwa reforms kuzirejesha zile haki kuu mbili za msingi za kikatiba, haki ya kuchagua na haki ya kuchaguliwa zilizoporwa kishetani kwenye katiba yetu?。Au ni mpango wa shetani kukisambaratisha Chama cha Demokrasia na Maendeleo,Chadema,kukinukisha kutaka kuzuia uchaguzi mkuu,kitu ambacho ni utopia,hakiwezekani hivyo Chadema itasusia uchaguzi,itakosa ruzuku na kujifia natural death?
8. Msingi Mkuu wa Nchi Yetu ni Katiba na Inapata Mamlaka kutoka kwa Wananchi。Na je Tundu Lissu ni mpango wa Mungu kwa Tanzania ndio maana akampa muujiza wa kusurvive risasi 16 ,hivyo ameponywa kwa makusudi fulani ili Mungu kumtumia Lissu kuonyesha utukufu wake kwa binadamu? na hata ushindi wa Tundu Lissu alivyomshinda Mbowe kwenye uchaguzi wa ndani wa Chadema ni mpango Mungu, hivyo Chadema pia ni chama mpango wa Mungu?, na kupitia Tundu Lissu,inawezekana Mungu anakwenda kulifanya lile jiwe walilo likataa waashi,litafanywa kuwa jiwe kuu la pembeni?,au Lissu ni agent wa shetani anayetumiwa kutaka kuleta ushetani wa no election kwenye taifa la Mungu hivyo mpango wa Lissu kukinikisha kuzuia uchaguzi ni mpango wa shetani?。
9. Haki hizi mbili za kuchagua na kuchaguliwa ndio haki kuu mbili za msingi sana za kisiasa ndani ya katiba yetu.Msingi mkuu wa nchi yetu ni Katiba ya JMT ya mwaka 1977。 Katiba ndio kila kitu!
Kwa mujibu wa katiba yetu, kitu muhimu kuliko kitu kingine chochote ni kwanza ni nchi, pili ni watu, wananchi. “we the people”, ndie mamlaka kuu ya nchi, aliyeipa mamlaka katiba, ndie mwenye nchi, ndie mwenye katiba, ndie muhimu kuliko kitu kingine chochote!
Mwananchi ametengeneza katiba yenye dhima, na dhamira ambapo dhima ya mtunga katiba, mwananchi ndio kila kitu!. Mwananchi ndie mwenye nchi, mwenye katiba, mwenye sheria, anamuajiri rais wa JMT kupitia kura yake na kumlipa mshahara kupitia kodi yake, hivyo rais wa JMT ni mtumishi wa Mwananchi, sambamba na mihimili yote mitatu.
9. Haki Mbili Kuu za Kikatiba,Kuchagua na Kuchaguliwa,zimeporwa Kishetani!Reforms Zitazirejesha!。
Ibara ya 5 ya katiba, imetoa haki kwa kila mwananchi aliyetimiza umri wa miaka 18,ana haki ya kupiga kura kumchagua kiongozi anayemtaka, na ibara ya 21 imetoa haki ya kila mwananchi aliyetimiza umri wa miaka 21,ana haki ya kugombea nafasi yoyote ya uongozi.
10. Vyama vya Siasa Tanzania ni Public Parties Lazima Vitangulize Mbele Public InterestsSerikali yetu kupitia Bunge letu Tukufu, ikapitiwa na shetani fulani, likafanya ushetani。fulani wa mabadiliko batili ya katiba kwa kuchomekea huo ushetani ndani ya kipengele batili cha kishetani ndani ya katiba yetu kwenye ibara ya 39 na ibara ya 67, ambazo zimepora zile haki kuu mbili za msingi za mwananchi kuchagua na kuchaguliwa na kuzikabidhi kwa kinyangarika fulani kinachoitwa chama cha siasa!.
Sasa mwananchi hana tena ile haki na uhuru wa kumchagua kiongozi anayemtaka, analazimishwa kumchagua kiongozi atakaye letewa na chama cha siasa!
Pia Mtanzania hana tena ule uhuru wa kugombea uongozi, kupigiwa kura kuchaguliwa,sasa analazimishwa lazima kwanza ajiunge na chama cha siasa, hiki chama kimdhamini ndipo aruhusiwe kugombea!.
Hii ni kinyume cha dhima na dhamira ya mtunga katiba, hivyo imetokea tuu, mimi member wenu humu JF, nimejaaliwa kamwanga kidogo cha kuisoma katiba yetu na kuibaini dhima na dhamira ya mtunga katiba, hivyo sasa nakatumia haka ka mwanga kadogo nilichojaaliwa nacho, kumulikia na wengine nao angalau waone mwanga jinsi shetani anavyoweza kujiinua na kupenya mpaka ndani ya katiba yetu!。Hivyo inawezekana hizo reforms za no reforms ni mpango wa Mungu,kuzirejesha haki pendwa,na kama ni kweli ni mpango wa Mungu,then ni Mungu atafanya kitu hadi reforms zitafanyika kabla ya uchaguzi,na zisipofanyika,ni Mungu mwenyewe ndie atausimamisha uchaguzi mkuu usifanyike,kwasabu Lissu,Chadema,taasisi yoyote au mtu yoyote hana uwezo wa kusimamisha uchaguzi wa taifa la Mungu,ila kama no election nayo ni mpango wa Mungu,then lisilowezekana kwa mwanadamu,kwa Mungu linawezekana!。
11. Baadhi ya Viongozi wa Vyama vya Siasa Sio Tu ni Insane Bali Baadhi ni Ma Ajent wa shetani!.Japo vyama vya siasa ni mali ya wanachama na kuhudumiwa na michango ya wanachama, kwa Tanzania, vyama vya siasa ni private parties vya wanachama, wakati tuu wa kuanzishwa, lakini vikiisha ingia kushiriki uchaguzi na kushinda, status ya vyama hivyo ina change from private parties za wanachama into public parties za umma wa wananchi na ndio maana vinalipwa ruzuku ya serikali ambazo ni fedha za wananchi. Fedha za serikali, ni fedha za umma,public money, ni fedha za wananchi, yoyote anayelipwa kwa fedha za imma wa wananchi, by taxpayers money ni public entity, kufuatia viongozi wa vyama hivyo kuchaguliwa na wananchi, the public, to hold a public office, serikali za mitaa, udiwani, ubunge hadi urais, walio wachagua ni public ya Watanzania na sio wanachama wao pekee, hivyo hivi vyama vyote vya siasa vyenye viongozi waliochaguliwa na wananchi ni public parties.
Kufuatia status hii ya vyama vya siasa kuwa ni public parties, then maamuzi yoyote ya chama kuhusu uchaguzi, lazima yazingatie the public interest na sio the selfish motives ya viongozi wake, na kiukweli baadhi ya viongozi wa baadhi ya vyama vyetu vya siasa ni watu muflisi kabisa!wanatoa kauli za kiajabu ajabu za kuhatarisha amani kama kauli ya “kukinukisha”,inawezekana ni ma agenti wa shetani ?na wengine kiukweli kabisa kwa kauli zao,hawa sio ni vichaa kabisa?! Kuwa kichaa sio mpaka kuokota makopo! Je, Tanzania tuna vichaa wengi kuliko tunavyojidhania?
Japo mgombea lazima adhaminiwe na chama cha siasa kugombea nafasi yoyote ya uongozi wa umma, kwa maoni yangu, udhamini una lengo zuri ili kupata viongozi bora na viongozi safi wenye uwezo wa uongozi, lakini kwa vile katiba inatoa haki kwa kila mtu kuwa huru kugombea nafasi yoyote ya uongozi, kitendo cha kulazimisha kila mtu lazima kudhaminiwa na chama cha siasa, huu sio tu ni ujinga, bali huu ni ushetani fulani!。 Kitendo cha haki kuu za msingi za kikatiba kuzuiliwa kinyume cha katiba, ni ushetani, na japo sasa ushetani huu, umehalalishwa kishetani kwa kuchomekewa kiubatili kwa koshetani shetani ndani ya katiba yetu kinyume cha dhamira ya mtunga katiba, kitendo cha vyama vya siasa kuutumia ubatili huu wa kishetani kama fimbo ya kuwachapia wanachama wake wanao hoji utimamu百na ukichaa wa viongozi wao, hakikubaliki!, ni uonevu na kinyume cha katiba ya JMT kwa dhima ya mtunga katiba!, huu pia ni ushetani!
12. Insanity Inawapataje Viongozi wa Siasa?.Kuwa kichaa sio mpaka kuokota makopo! Je, Tanzania tuna vichaa wengi kuliko tunavyojidhania?Wanabodi, hapa kwenye hili,naomba kutanguliza ashakum, na kuomba radhi kwa haya ninayoyaandika kuhusu baadhi ya viongozi wetu wa vyama vya siasa kuwa sio tuu ni insane bila ya wao kujijua kuwa they are insane!, ila pia ni maajenti wa shetani bila wao kujijua,wanatumika na shetani kwa kumtumikia shetani kwa kufanya kazi za kishetani ndani ya vyama vya siasa!。
Utawajua viongozi mashetani hawa kwa mawazo, maneno ya kauli zao za kiajabu ajabu na matendo yao ya kuhatarisha amani na umoja wetu!。 Mfano kuna kauli za kiajabu ajabu zinazotolewa na baadhi ya viongozi wetu, zinastaajabisha hadi mtu unajiuliza kama viongozi hawa wanao toa kauli hizi wana akili timamu?!.
Ili kuielewa hii dhana ya viongozi insane, karibu hapa na twende taratibu ili umjue insane ni nani na ajenti wa shetani ni kiongozi wa aina gani na utamtambuaje na kumtofautisha na mtu mwenye akili zake timamu Kuwa kichaa sio mpaka kuokota makopo! Je, Tanzania tuna vichaa wengi kuliko tunavyojidhania?
13。Mtu Kuwa Insane Sio Kosa, ni Hali Tuu, Lakini Kikundi cha Watu, Chama, Kikao au Wanachama Wote Kukubali Kufuata Ushauri wa Isane, Wote Mtaonekana Insane!. Wale Wasio Insane, Wasikubali Maamuzi ya Kijinga!.Kama nilivyoeleza pale juu, mtu kuwa insane ni hali tuu, kwa Kiswahili kizuri ni kughafilika. Mtu unaweza kuwa timamu kabisa, lakini ukatibuliwa na jambo fulani, ukachukia ukachukua maamuzi ya hamaki, hasira na kufanya kitendo ambacho sio cha kawaida sometimes hata kuua!, halafu ukiisha tulia, ndipo akili zinakurudia,unajiuliza umefanya nini na kuanza kuujutia uamuzi wako!。
Lengo la chama cha siasa, ni kushika dola, hivyo viongozi wanaogombea nafasi mbali mbali kwa lengo la kushika dola (urais), kushika jimbo (ubunge), kata (udiwani), na mitaa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa. Akitokea kiongozi wa siasa akazuia chama ama wanachama kushiriki zoezi la uchaguzi huru na wa haki,then kiongozi huyo ni insane,na akitokea kiongozi wa chama cha siasa,akasema atakinukisha mpaka uchaguzi usifanyike,kiongozi wa type hii, sio tuu ni insane,bali pia ni agent wa shetani bila yeye kujijua!
Sasa katika kugombea, kukijitokeza umati mkubwa wa watu katika mikutano yako, wanakushangilia sana,unajaza sana nyomi, kunakupa matumaini hewa ya kukubalika, hivyo mgombea unakuwa na too great expectation ya kushinda, kumbe ni just some false hopes, hivyo uchaguzi ukifanyika, matokeo yakaonyesha umeshindwa, unapagawa, unachanganyikiwa unakuwa huamini matokeo, hivyo unaghafilika, unarukwa na akili, una despair, hiyo hali inakusababishia hali inayoitwa preudo insanity, hivyo unatoa maamuzi ya ajabu ajabu, hatua ya kwanza inaitwa denial, hukubali matokeo, unaamini ulishinda ukaibiwa kura, hivyo una wamobilize wafuasi wako muingie barabarani kukinukisha!, this is madness! kutaka kuwafolenisha watu kuwaingiza barabarani kuwadanganya utasimamisha uchaguzi isifanyike kwa kukinukisha!huu ni ishetani! kiongozi wa aina hii, anaweza kuwa ni agent wa shetani anamtumikia shetani bila kujijua!。
Hatua ya pili ni kutoa taarifa kuwa hukubali matokeo, hii ni kawaida kwa kila asiyakubali kushindwa. Hatua ya tatu ni kusema huwatambui walioshinda. Unaweza usiwatambue kwa muda, lakini walioshinda wakiisha apishwa, kutowatambua ni muendelezo wa insanity!. Hatua ya nne ni kususa, na kutaka kuwazuia wengine walioshinda kihalali, au kususia kutoa ushirikiano kwa walioshinda, kama hili la kugomea kutoa majina ya wabunge wa viti maalum!.
Kuna wanaoshindwa na kubakia kuwa stable, lakini kuna wanaoshindwa na kuchanganyikiwa hadi kurukwa akili, sasa hawa walioshindwa na kurukwa akili wakitoa maamuzi ya ajabu ajabu, kama kukinukisha,wenye akili timamu mkiwafuata, wote mtaonekana insane!, hivyo lile kundi la G-55 ndio wenye akili timamu!
14. Je Kila Uamuzi wa Kugomea Jambo au Kususia Kitu ni Ujinga, Insane ?Uchaguzi uliopita umepita, walioshinda, wameshinda, iwe walishinda kihalali kimbinu,kwa bao la mkono,that is bygone,let the bygones be bugones, walioshindwa wameshindwa, sasa uchaguzi mwingine unakuja, zipo taarifa za baadhi ya viongozi walioshindwa kutaka kuwazuia wanachama na wafuasi wao wasishiriki uchaguzi kwa kuwahadaa utauzuia uchaguzi kwa kukinukisha!, this is madness!.
Wito wangu kwenye hivyo vyama, kama kuna viongozi ambao sio insane, please stop this madness ndani ya vyama vyenu, vinginevyo wote mtaonekana ni vichaa mnatumika na shetani!。
Hitimisho.Hapana, sio kila kugomea jambo au kususia jambo fulani ni ujinga. Kugomea jambo fulani ili kutuma ujumbe mzito kwa watawala, kuwa this is not right, kunakubalika, hivyo maandamano ya kutuma ujumbe, demonstrations au industrial actions kwa wafanyakazi, kudai haki zao, ni migomo halali na ina justification kwa ajili ya kutimiza malengo fulani, ndio maana ninainga mkono reforms kuondoa ule ushetani kwenye katiba yetu!
Kipimo cha kususia jambo fulani au kugomea fulani, kipi ni uamuzi sahihi na kipi ni ujinga na uendawazi, ni kipimo cha kutumia matokeo, jee ukigomea jambo fulani, una goma ili kuachive nini?, kama unagoma tuu ili mradi kugoma, au unasusa tuu ili mradi kususa, kwa kugoma huko, huta achieve anything, huku ndio kugoma kwa ujinga na uendawazimu, na kumtumikia shetani,,viongozi wa vyama wanaohimiza vyama vyao kususia uchaguzi,huku ni kugoma ambapo there is nothing they'll achieve kwa kususa huko au kugoma huko, huu ndio uendawazimu ninaouzungumza hapa! Swali kuhusu tabia ya kususa, kugomea au kuzira: Je, si tabia za kike, si utoto?
Unaweza kususa kushiriki uchaguzi kwasababu uko huru kushiriki uchaguzi au usishiriki,lakini huwezi kuwazuia wengine kushiriki uchaguzi,ni madness,lakini kitendo cha kusema utazuia uchaguzi usifanyike kwa kukinukisha!,huku ni kumtumikia shetani na kuwa ajenti wa shetani!
Kwa vile vyama vya siasa ni public parties, viongozi wa vyama, mna wajibu wa kuviendesha vyama vyenu kwa kutanguliza mbele maslahi ya umma na sio maslahi binafsi ya viongozi wenu, msiruhusu ignorance, insanity, selfishness na utumishi wa shetani kwa baadhi ya viongozi wenu wabinafsi, kuviangamiza vyama vyenu kwa ignorance, insanity, selfishness yao, na mpango wa shetani wakati miongoni mwenu sio wote mko insane.
ila inawezekana hii no reforms no election ni mpango wa Mungu kwa Tanzania anao letwa kwa mtindo wa blessing in disguise,ili hizo reforms ziondoe ule ushetani uliofanywa kwenye katiba yetu,hivyo Chadema ni mpango wa Mungu na Tundu Lissu ni mpango wa Mungu kuwakomboa Watanzania kurejeshewa haki zao。
Kipimo cha mwisho NRNE na Tundu Lissu kama ni mpango wa Mungu au wa shetani,tutakipima kwa performance and the end justifies the means,kama NRNE ni mpango wa Mungu,then Mungu atatenda,reforms zitafanyika kabla ya uchaguzi na tutafanya uchaguzi huru kweli na wa haki kweli na kama kusipofanyika reforms,uchaguzi haitafanyika, sio Tundu Lissu, Chadema na wafuasi wao kukinukisha,bali kwa Mungu Baba muweza wa yote kufanya kitu kitakachofanya uchaguzi usifanuike!。
Kama NRNE,ni mpango wa shetani,hakutafanyika reforms zozote,na uchaguzi utafanyika kama kawaida,huo mpango haramu wa kuzuia uchaguzi mkuu usifanyike,utashindwa!, mipango ovu ya maajenti wa shetani,washindwe na walegee!
Mungu Ibariki Tanzania!
Nawatakia Jumatatu Njema na mapumziko mema ya Karume Day。
Paskali