Uchaguzi 2020 Lissu muulize mpinzani wako, ‘Jina lako ni nani?’

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Mara kadhaa nimelinganisha mtanange wa uchaguzi wa mwaka huu na pambano la ngumi kati ya Muhammad Ali na George Foreman.

Leo hii nitagusia jambo ambalo nadhani wengi mtakuwa mmeligundua. Nalo ni hii tabia ya mgombea wa Urais wa CCM, John Magufuli kukataa kata kata kutaja jina la mpinzani wake mkuu, Bw. Tundu Lissu. Sikumbuki kama nimewahi kumsikia Magufuli akitaja jina la Lissu hata siku moja.

Najua kwenye medani za saikolojia, kutotaja jina la adui yako inaweza kuwa ni ishara ya kumdharau na kujaribu kuonyesha kuwa haumuwazii lakini inaweza kuwa ishara ya woga uliozidi kipimo.

Muhammad Ali, bondia maarufu kuwahi kutokea duniani aliwahi kubadilisha dini yake iliyopelekea kubadili na jina lake kutoka kuitwa Cassius Clay. Media na baadhi ya watu walisuasua kuanza kutumia jina lake jipya jambo ambalo kumbe lilikuwa linamkera sana Ali.

Siku moja akawa anapambana na bondia Ernie Terrell. Bondia huyu alikuwa anakataa kumuita Ali kwa jina lake jipya hata walipokutana katika TV Show kabla ya pambano. Ali akamwambia:

"My name is Muhammad Ali, and you will announce it right there in the centre of that ring after the fight, if you don't do it now,". Terrell bado akakataa!

Kilichofuata ni Ali kumchakaza Terrell kwa kipigo cha mbwa koko katika moja ya mapambano ya kihistoria yanayokumbukwa katika mchezo wa ngumi. Ali alikuwa anamchakaza mpinzani wake huku akimrushia maneno ya hasira na kejeli, “Jina langu Nani? What’s my Name?”.

6769F0BC-4BC4-4363-BA17-82D2D206B9CC.jpeg

Lissu amekuja katika uchaguzi huu kutoa changamoto ya karne katika medani za siasa. Anajua hilo, wapinzani wake wanajua hilo, na sisi tunajua hilo.

Kuna siku aje amuamuru hasimu wake mkuu, alitaje jina lake sasa au atakuja kulitaja akiwa katika mazingira yasiyo rafiki sana kwake. Itapendeza akimuuliza hilo swali September 07, 2020.
 
Mmh! Kwamba Lissu ni tishio kwa Magufuli hata awe akimtaja kwa jina wakati wa Campaigns?

Sijui umri wako mleta mada; iwapo umefikisha 40s, basi, usiendelee kusumbua kichwa. Waliwahi pita akina Mrema, Lowasa. Hii ya huyu bwana mdogo Lissu mbona ni cha mtoto tu. Watanzania wana siasa wanazijua wenyewe. Watajaa kukusikiliza. Watasukuma hadi gari lako ati usimalize mafuta; kwenye kura sasa! Hapo ndiyo yanaanza, Nimeibiwa kura!

Lissu hawezi kumshinda Magufuli na kama bado huamini, subiri hiyo 28, Oktoba 2020.
 
Mmh! Kwamba Lissu ni tishio kwa Magufuli hata awe akimtaja kwa jina wakati wa Campaigns?

Sijui umri wako mleta mada; iwapo umefikisha 40s, basi, usiendelee kusumbua kichwa. Waliwahi pita akina Mrema, Lowasa. Hii ya huyu bwana mdogo Lissu mbona ni cha mtoto tu. Watanzania wana siasa wanazijua wenyewe...
Saizi tumeamua mkuu tayari mtaani tunahamasishana lisu kura anapata na za kutosha ,ukweli Ni kwamba ccm watu wameichoka wananchi wanaugulia moyoni ndio maana saiz tumeamua hii Ni 2020 kura yangu nampa lisu magu nilimpa 2015 ila hajaitendea haki saiz inaenda chadema
 
Usiteseke hilo limeshaeleweka singida ulikuwa among top region's alikoenda kuangukia wazazi wa mpinzani kwamba. Mwambieni mtoto wenu aniachie na ninyi nichagueni yeye nitampa ajira. Pengine nimekosea ku kuyarudia maneno ila sipo mbali.

Hilo kiroho ni kukubadili kuwa huyu siyo saizi yangu, sitamuweza, wazee nisaidieni.
 
Hiki Ni kipindi tofauti kabisa na vipindi vingine vilivyopita.

Ni kipindi ambacho tunashuhudia mabadiliko makubwa ya teknolojia, kizazi kipya kimeibuka Cha vijana wengi wanaojitambua.

Chaguzi za nyuma kulikua na wimbi kubwa la watu wasioelewa Nini serikali inatakiwa kuwafanyia, wengi walikua wanarubuniwa kwa maneno na vijizawadi kidogo uchaguzi ukikaribia, na katika chaguzi hizo wapiga kura walikua Ni watu wazima ambao wengi hawakuelimika.

Kipindi hiki Kuna mwamko mkubwa sna wa watu wanaojitambua kupiga kura, na hili tumeliona katika kura za maoni za chaka Cha mapinduzi CCM, hivyo Kuna watu wanatakiwa wajiandae kisaikolojia kwa chochote kitakachotokea.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mmh! Kwamba Lissu ni tishio kwa Magufuli hata awe akimtaja kwa jina wakati wa Campaigns?

Sijui umri wako mleta mada; iwapo umefikisha 40s, basi, usiendelee kusumbua kichwa. Waliwahi pita akina Mrema, Lowasa. Hii ya huyu bwana mdogo Lissu mbona ni cha mtoto tu. Watanzania wana siasa wanazijua wenyewe. Watajaa kukusikiliza. Watasukuma hadi gari lako ati usimalize mafuta; kwenye kura sasa! Hapo ndiyo yanaanza, Nimeibiwa kura!

Lissu hawezi kumshinda Magufuli na kama bado huamini, subiri hiyo 28, Oktoba 2020.
Watu werevu hIshi na wakati, hawaishi kwa mazoea.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila Ma
Usiteseke hilo limeshaeleweka singida ulikuwa among top region's alikoenda kuangukia wazazi wa mpinzani kwamba .... mwambieni mtoto wenu aniachie na ninyi nichagueni yeye nitampa ajira.... pengine nimekosea ku kuyarudia maneno ila sipo mbali.

Hilo kiroho ni kukubadili kuwa huyu siyo saizi yangu, sitamuweza, wazee nisaidieni.
Hivi maandamano aliyoitisha nchi nzima pale Zakiem Mbagala yanaanza lini?
Au na wananchi nao wanamdharau?
 
Hiki Ni kipindi tofauti kabisa na vipindi vingine vilivyopita.
Ni kipindi ambacho tunashuhudia mabadiliko makubwa ya teknolojia, kizazi kipya kimeibuka Cha vijana wengi wanaojitambua .
Chaguzi za nyuma kulikua na wimbi kubwa la watu wasioelewa Nini serikali inatakiwa kuwafanyia, wengi walikua wanarubuniwa kwa maneno na vijizawadi kidogo uchaguzi ukikaribia, na katika chaguzi hizo wapiga kura walikua Ni watu wazima ambao wengi hawakuelimika.
Kipindi hiki Kuna mwamko mkubwa Sana wa watu wanaojitambua kupiga kura, na hili tumeliona katika kura za maoni za chaka Cha mapinduzi ccm , hivyo Kuna watu wanatakiwa wajiandae kisaikolojia kwa chochote kitakachotokea.

Sent using Jamii Forums mobile app
Vijana wengi wana elimu gani?
Hii ambayo Lisu anaiponda?
 
Nipo huku jimbo la Singida mashariki. Lisu hakuna kitu huku, lissu huku ni kama dagaa tu.
 
Mmh! Kwamba Lissu ni tishio kwa Magufuli hata awe akimtaja kwa jina wakati wa Campaigns?

Sijui umri wako mleta mada; iwapo umefikisha 40s, basi, usiendelee kusumbua kichwa. Waliwahi pita akina Mrema, Lowasa. Hii ya huyu bwana mdogo Lissu mbona ni cha mtoto tu. Watanzania wana siasa wanazijua wenyewe. Watajaa kukusikiliza. Watasukuma hadi gari lako ati usimalize mafuta; kwenye kura sasa! Hapo ndiyo yanaanza, Nimeibiwa kura!

Lissu hawezi kumshinda Magufuli na kama bado huamini, subiri hiyo 28, Oktoba 2020.
Yaeleekea wewe akili yako kila siku inasoma LEO,
Haisho KESHO
Haisomi KESHO KUTWA
Akili yako inauwezo wa kusoma jioni tu na siyo asubuhi, mchana na usiku.

Napata shaka juu ya familia uliyonayo ni familia ya aina gan!

Maana kama huwezi kutambua mabadiriko ya watanzani, mabadiriko ya nyakati, mabadiriko ya watu kimtazamo na kifikra

Familia ya itakuwa ya ajabu sana, maana wewe wanakwita mama na mkeo wanamwita baba, kwakuwa umewarithisha kutotofautisha.
Tambua mtanzania wa lyatonga na lowasa siyo mtanzania wa Lissu.

MWAKA HUU MTAKAKOMA
 
Mmh! Kwamba Lissu ni tishio kwa Magufuli hata awe akimtaja kwa jina wakati wa Campaigns?

Sijui umri wako mleta mada; iwapo umefikisha 40s, basi, usiendelee kusumbua kichwa. Waliwahi pita akina Mrema, Lowasa. Hii ya huyu bwana mdogo Lissu mbona ni cha mtoto tu. Watanzania wana siasa wanazijua wenyewe. Watajaa kukusikiliza. Watasukuma hadi gari lako ati usimalize mafuta; kwenye kura sasa! Hapo ndiyo yanaanza, Nimeibiwa kura!

Lissu hawezi kumshinda Magufuli na kama bado huamini, subiri hiyo 28, Oktoba 2020.
Una maana hata kwa jpm wanajaa tu lakini kura hawampi(?
 
Back
Top Bottom