Lissu kumjibu Nape kesho

MCHARA

Senior Member
Jan 15, 2011
109
22
Mwanasheria wa Chadema na Mwanaharakati Mh Tundu Lissu anaunguruma kesho kwenye viwanja vya Magomeni kata ya Kirumba wilayani Nyamagana katika mkoa wa Mwanza kesho alasiri baada ya kutoka kumtetea Mbunge wa Ilemela David Kiwia(cdm). Mpango mzima ni kuendeleza mapambano ya ukombozi wa Taifa letu!
 
Daaah, hawa jamaa wanatupenda sana watanzania. Kaona asiondoke jijini bila kuzungumza na wana Mwanza waliotukanwa kuwa watashikishwa ukuta na Nape. Kama magamba wangekuwa karibu hivi na watanzania mbona huu umaskini tungeridhika nao tu. Mh Lissu gombea urais wa Tanzania 2025 Dr Slaa akimaliza vipindi vyake viwili kwa mujibu wa katiba...
 
Hivi huyu jamaa muda gani anawatembelea wapiga kura wake. Sifa zitamuumbua 2015.
 
Vipi kesi ya Kiwia inaendelea vipi maana najua chini Ya Tundu Lissu hakuna kesi inayoshindikana
 
Hivi huyu jamaa muda gani anawatembelea wapiga kura wake. Sifa zitamuumbua 2015.
Kazi ya ubunge sio kama karani wewe, au sio kushinda vijiweni kama Mtemvu na Iddi Azani... Hivi wewe mbunge wako asipokuwepo jimboni unalala na njaa?
 
Kumekucha, nadhani maana yake hapa ni kupima kina cha maji..... viva lakini...!!!
 
Kazi ya ubunge sio kama karani wewe, au sio kushinda vijiweni kama Mtemvu na Iddi Azani... Hivi wewe mbunge wako asipokuwepo jimboni unalala na njaa?
ah haaa haaaa haaaaaaaaaaaa...................you made my day mkuu.
 
Back
Top Bottom