Lipumba yuko 'blackmailed'?

The "system" is trying to rig this election in order to create internal conflict. Nani anafaidika kwa huu mtafaruku ndani ya CUF? Jibu unalo Mkuu.

Wanaompa maagizo
huoni alikuwa analindwa na polisi?
jiulize polisi wanawezaje kumlinda mtu bila 'amri kutoka mamlaka ya juu'?
 
Kajitia aibu sana, huyu ni msomi wa kiwango cha juu katika ubobezi wa uchumi, dunia inamhitaji sasa iweje aendelee kung'ang'ania siasa wakati siasa imeisha mkataa baada tu ya kitendo chake cha usaliti. Mtu anapelekeshwa kama mtoto aibu sana
 
Maswala ya kusema kwamba Prof. Lipumba anategemewa na dunia katika maswala ya uchumi ni uongo ulio wazi.

Prof. Lipumba anawashauri kiuchumi Uganda lakini hata sisi Tanzania tunawashinda kwa hiyo ni uongo. Yeye angewashauri na wakatushinda ningemkubali
 
Hao wanaompa polisi kumlinda na kumsaidia kuleta mtafaruku ndani ya CUF kwanini wasimkaribishe wao kwenye chama chao? Au wanaona ana umuhimu mkubwa kwao kuendelea kubaki ndani ya CUF kuliko akiwemo ndani ya chama chao!?

 
Pesa ni sumu kali inakuvua nguo wakati hupendi vilevile pesa ni tamu mana unakuwa una Power ukitakacho kinafanyika kwa wakati mwafaka..Lipumba pumzika kabla hawajakuacha mtupu
 
Heshima yake iliharibika alipojitoa tu sasa changanya na hili la kutaka kurudi kabisa kaishaharibu
 
Kumbuka kuwa yeye ndiye aliyemkaribisha na sisi tuliokuwepo tunajua kila kitu.. Swali la kujiuliza ni kwanini baada tu ya kumaliza huo mpango akasaliti?
Hujui propaganda za kisiasa Dk Slaa akamkaribisha wapi Lowassa? Elewa Lowassa alienda Chadema kila kitu kikiwa kimeishatafunwa hata yeye alimpokea kama dodoki tu hakuwa na cha kufanya.

Ndiyo maana baada ya akili kumrudia akaamua kuingia mafichoni na baadaye akajiondoa kuachana na undumila kuwili wa akina Mbowe.
 
Nadhani pale Tabora kuna nuksi, mji wenye zaidi ya miaka 100 na hauendelei. Ukijumlisha Lipumba na Mapalala unapata jibu.
 
Kulinda usalama wa raia na mali zao yakiwemo maandamano na mikutano ya hadhara
 
Kimsingi CUF ilianzishwa bara...


Hivi leo unadhani CUF ikivunjika upande upi utaumia? Bara au visiwani?

BTW CUF bara kuna mamluki wengi..afadhali Zanzibar wanaonekana wako serious...CUF Zanzibar wanamaanisha business sio ma puppet kina lipumba
 
 
Pasco maoni na ushauri wako si sahihi. Lipumba is not desperate to that level. Lipumba ni kiongozi wa TANU Youth League - enzi Kikwete akiwa mwenyekiti (UDSM 1973). Lipumba alitokea Tabora Boys (PCM) akiwa na akina Mukandala na Kaberuka. Hao wote walipata div.I F.6 PCM lakini hakuna aliyeslma Engeneering. Hiyo haikuwa accident either; Mukandala alisoma political science na Lipumba na Kaberuka walisoma Arts -Economics. Wote walikuwa recruited tangu wakiwa Tabora boys. Lipumba yuko kazini. Hints:
1. Kutoka ushauri wa Rais (TZ), kwenda ushauri wa Rais (Uganda) halafu kujiunga na kugombea upinzani (chama kilichokuwa kikipigiwa kelele kuwa ni chama cha waislam).

2. Sababu ya kifo cha Hayati Prof. Kighoma Ali Malima vis-a-vis kuongoza chama cha upinzani kilichodhaniwa kuwa cha waislam (NAREA).

3. Vituko vyake wakati wa kutafuta mgombea urais wa UKAWA (2015), kumkaribisha Lowasa na baadaye kujikata 'ki aina' (actually hiyo ilikuwa plan B baada plan ya awali kukwama kutokana na Lowasa kujiunga UKAWA).

Lipumba will always be there doing this and that so long as it gives vent to his principal, basi.
 
 
Mwanzoni nilimchukia LI-pumba lkn sasa namhurumia. Mungu aniepushie mwisho huu mbaya.
 
Wanaompa maagizo
huoni alikuwa analindwa na polisi?
jiulize polisi wanawezaje kumlinda mtu bila 'amri kutoka mamlaka ya juu'?
Sasa'apo unasemaje ka-blackmailiwa badala ya kusema yeye ndiye aliyeki-blackmail Cuf! Usahihi ni upi?
 
Dhambi ya usaliti ndio inayomtesa
Nasikia hata kuamua kujiuzuru si nia yake kwa mapenzi yake,alishinikizwa kama wazaramo wanavyoshinikizwa kuhama makwao, katikati ya Dar. Mtu anafukuzwa kwa dau! "Chukua mil.50,kesho uhame nisikuone hapa" Ndivyo alivyoshinikizwa kuachia ngazi.
Ivi wewe hiyo "dilemma" yake ya sitakinataka,inaweza kufanywa na msomi ngazi ya professor?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…