umoja wa mashaka huu.... ukiyaomba majina yako ndo utazimia kabisa ,, na ndio utajua pingamizi lina chanzo chake
Chadema wamezingatia kwamba CUF inakubalika zaidi Zanzibar wakawaachia CUF watoe mgombea huko. Ni busara na kwa Lipumba kutambua kuwa hana ushawishi bara na awaachie Chadema wanaokubalika zaidi bara. Halafu, Lipumba azingatie kuwa si busara wao CUF pekee wasimamishe mgombea sehemu zote, bara na visiwani. Hapa napata mashaka makubwa na u-professa wa Lipumba na pia sijui ana agenda gani binafsi iliyojificha.Soory charlie !!! mimi sijakuuliza mambo ya biashara
suali lilikuwa
kwani chadema wangaligombea Zanzibar wangalishinda ??
Huyu bwana nilianza kumtilia shaka wakati UKAWA wanapambana na CCM kuhusu sheria za gesi yeye alikuwa anafanya mikutano ya kulazimisha kupendwa kama Lowassa.Kama haelewi, huenda ni kabaraka basi!
Hii habari ya kuwa CUF watatoa uamuzi tarehe 25 July siyo game ya mapatano bali Lipumba amedhamiria kukwamisha malengo ya UKAWA kwa sababu ya ubinafsi wake.Kauli Ya lipumba kasema ni mambo tu yanamzidi yy hapingi maamuzi Ya UKAWA.
Ni wakati wa kumuonya Lipumba asiwe kama Lowassa ambaye kwa ubinafsi wake alifikiri Tanzania ni yeye na yeye ndiye Tanzania kana kwamba nchi hii ni mali yake. Lipumba ni wakati wa kusoma alama za nyakati.
Acha kung'ang'ania kugombea urais wakati ukijua hauna ushawishi Tanzania bara.Kura ulizopata ni ushahidi tosha, na wewe kama msomi usifiche kichwa chako kwenye machanga huku mwili wako mzima unaonekana.
Lipumba asilazimishe kupendwa kama Lowassa. Lipumba ukiwa ndani ya UKAWA, waachie CHADEMA wapeperushe bendera ya urais kwa kuwa ni ukweli uliowazi kuwa wanakubalika zaidi Tanzania bara kuliko wewe na chama chako.
Pili CUF tayari imepewa nafasi ndani ya UKAWA kupeperusha bendera ya rais upande wa Zanzibar.
Sasa ubinafsi gani tena huu wa kung'ang'ania kugombea urais kama Lowassa?
Acha hizo Lipumba, toa nafasi kwa UKAWA kumpata rais wa Tanzania kwa kumuunga mkono Dr. Slaa ambaye anauzika kirahisi kuliko wewe.
Mimi nawashangaa mnaomtaka lipumba akatae kugombea urais,kuna kitu watu wanakikwepa hapa,
1.cuf kwa mlengo wao wa kisiasa jinsi ilivyo hawawezi kumuunga mkono mkatoliki tena padre,
2.cuf ndio chama ambacho kichinichini kinajinasibu kuwa ndio mtetezi wa waislamu,sasa kitamuungaje mkono mgombea ambae ni mkristo?
NOTE:Muulize ni mtatiro kwanini hayupo kwenye ile nafasi ambayo iko chini ya sakaya kwa sasa!
Una maanisha nini mkuu?
Ona ukweli mkuu. Slaa alipata kura nyingi kiasi kwamba alikaribia kuwa rais. Hata takwimu za urais wa Kikwete haijawahi kuwa wazi na ya kuaminika. Wengi wanaamini Slaa alipata kura za kutosha kuwa rais. Lipumba hana ushawishi bara na kura zake zinaonyesha hivyo kwa mara nne alizogombea urais. Lipumba anatambua kuwa hakubaliki bara ndiyo maana aliamua kumfanyia kampeni Kikwete ilihali na yeye alikuwa anagombea urais. Kikwete alikuwa na hali mbaya kwa Dr. Slaa na hili Lipumba analijua. Lipumba kungangania kugombea urais bara ni mwendeleze uleule wa kutotaka kumuunga mkono Dr. Slaa kwa sababu ya ubinafsi wake kama alivyofanya mwaka 2010.Sio lipumba tu hta dr slaa nae inabidi akae pembeni cz hauziki kwa wananchi wote walishagombea na wakakosa tunahitaji sura mpya ukawa