Lipumba usiwe na ubinafsi kama Lowassa

Lipumba usiwe na ubinafsi kama Lowassa

Watanzania wote wanafahamu kuna hila zilifanyika ili kulikata jina la LOWASSA, ila Inshallah mwenyezi Mungu ataamua, what is next!
CCM kwa hila hawajambo,ila jamaa chali kifo cha mende ndembendembe kwisha habari yake.Wapambe wamekula pesa yake sasa hivi wapo na magufuli
 
upo sahihi kabisa
sasa kwanini CDM na UKAWA walishabikia CCM imuingize Lowassa km mgombea URAIS?
huoni walitaka waingie Ikulu kwa kunadi uovu na ufisadi wake
Hushangai leo UKAWA inachanganyikiwa na wao hawamtaki?
Ngoja Mbowe na Mteu watakapomuingiza MuArusha mwenzao
chezea BILLIONI 50 itakayomwagwa?
CCM wote wabovu, Lowassa ni mbovu zaidi. Ilikuwa ni mkakati wa kuwahadaa CCM waweke mgombea mwenye kashfa nyingi ili washinde kirahisi zaidi.
 
Hoja za lipumba ni nne na muhimu:
1. Hatujaachiwa Zanzibar; CUF kabla ya ukawa ilikuwa na uwezo wa kushinda zanzibar.

2. Majimbo ya bara hatupaswi kupewa china ya 100 hii ni dharau. Cuf tunauwezo na mtaji huku bara wakutosha kugawana angalau sawa na chadema. kutupa chini ya mia ukiunganishwa na kutotoa uraisi ni kurudishwa nyuma.

3. Cuf inamgombea aliyebobea kelimu ya sekula. Dr.Slaa hakubaliki kwa waislam wengi na wanakisasi wanasubiri muda tu wakioneshe dhahiri. Dr.Slaa kasomea elimu ya kanisa tu hakubaliki kwa masheikh .

4. Lazima tujue na kukubaliana kuhusu ilani ambayo tutaitekeleza. hatuwezi kushirikiana bila mipaka halisi.


so Hata kama sio mimi then achaguliwe msomi wa NCCR mageuzi.
Hizi ni hoja zinazosukumwa na ubinafsi wake.
 
Ni wakati wa kumuonya Lipumba asiwe kama Lowassa ambaye kwa ubinafsi wake alifikiri Tanzania ni yeye na yeye ndiye Tanzania kana kwamba nchi hii ni mali yake. Lipumba ni wakati wa kusoma alama za nyakati.

Acha kung'ang'ania kugombea urais wakati ukijua hauna ushawishi Tanzania bara.Kura ulizopata ni ushahidi tosha, na wewe kama msomi usifiche kichwa chako kwenye machanga huku mwili wako mzima unaonekana.

Lipumba asilazimishe kupendwa kama Lowassa. Lipumba ukiwa ndani ya UKAWA, waachie CHADEMA wapeperushe bendera ya urais kwa kuwa ni ukweli uliowazi kuwa wanakubalika zaidi Tanzania bara kuliko wewe na chama chako.

Pili CUF tayari imepewa nafasi ndani ya UKAWA kupeperusha bendera ya rais upande wa Zanzibar.

Sasa ubinafsi gani tena huu wa kung'ang'ania kugombea urais kama Lowassa?

Acha hizo Lipumba, toa nafasi kwa UKAWA kumpata rais wa Tanzania kwa kumuunga mkono Dr. Slaa ambaye anauzika kirahisi kuliko wewe.

CUF nao wanataka kuchekesha, yaani wagombee uraisi zanzibar, na huku Bara pia! Kwanza washukuru mbeleko ya Chadema wataongeza viti vya ubunge na madiwani

acheni urofa swala la zanzibar na bara nitofauti kabisa CUF zanzibar inakubalika kote na huku bara CDM inakubalika baadhi ya maeneo.
na kama hoja yenu huyo slaa kuwa anakubalika lakini hana uwezo wa kuongoza hilo mulitambua sio muadilifu kwanza ana kashfa ya kuiba kanisani
 
Hatumtaki Padri Slaa tunamtaka Professa wa Uchumi Lipumba kama vipi tugawane mbao nyie bakini kaskazini nasi tubaki maeneo mengine, wabaguzi wakubwa nyie!
Lipumba hauziki bara. Rejea kura alizopata chaguzi zilizopita
 
acheni urofa swala la zanzibar na bara nitofauti kabisa CUF zanzibar inakubalika kote na huku bara CDM inakubalika baadhi ya maeneo.
na kama hoja yenu huyo slaa kuwa anakubalika lakini hana uwezo wa kuongoza hilo mulitambua sio muadilifu kwanza ana kashfa ya kuiba kanisani
Linganisha kura alizopata Slaa na Lipumba chaguzi zilizopita. Lipumba hauziki bara.
 
CUF nao wanataka kuchekesha, yaani wagombee uraisi zanzibar, na huku Bara pia! Kwanza washukuru mbeleko ya Chadema wataongeza viti vya ubunge na madiwani

Mmeanza matusi hapa kama vp kila chama kivyake CUF ilikuwepo na itaendelea kuwepo huyo slaa alshagombea naye kakosa wote hawana jpya
 
Hatutaki kusema mengi kuhusu huyu Lipumba, ni mbinafsi hakuna. Unakumbuka kampeni zake za mwaka 2010. Kuna CD ilimrekodi anavunja miiko ya umoja wa nchi yetu. Leo hii inajipa umaarufa wa kupandikiza kama Lowassa. Hovyo kabisa Lipumba.

ukweli n kwamba chadema imejkita sana katika christians'populated areas the same to cuf muslims populated areas so kila mmoja hakubaliki pande fulan kosa lolote lkifanyka bila ya mgawo wa madaraka iwapo watapita UKAWA jua wamepoteza hvyo waweke waz iwapo watapta nani rais,makamu na waziri mkuu hakuna mtoto wa kugeukwa baadae hapa la cvyo CCM angalau ina mchanganyiko wa din hizi mbili angalia magufuli na vice wake
 
Hmmm! Ukawa kweli mmekwisha!! Hamna hata viongozi mnaowategemea kuwa raisi! Bado mnamuona kikongwe Slaa ndio rais mtahiki???!!!! Mmekwishaaaaaa
 
Lipumba hauziki Tanzania bara,anatakiwa alijue hili na awaachie CDM ndani ya UKAWA.

Soory charlie !!! mimi sijakuuliza mambo ya biashara

suali lilikuwa

kwani chadema wangaligombea Zanzibar wangalishinda ??
 
Back
Top Bottom