Lipumba awavaa viongozi CHADEMA

Lipumba awavaa viongozi CHADEMA

Nilimuheshimu sana Prof. na kuamini kwamba uprofesa wake haukuwa wa kubumba. Lakini kama sasa hivi kaishiwa mpaka anaanza kuimba sifa za ccm na kuanza kuina cdm kama adui wa cuf, uh, naogopa kama huku ndo kuzeeka, basi bora tufe tukiwa vijana na akili zilizonyooka kuliko kuliko kufikia uzee na kuzeeka vibaya kama Lipumba.

tatzo nyievijana mna matatizo mna mapenzi ya chama co mapenzi na nchi yenu mtu anapotoa tatzo la chama tafakar kwanza ivi kwann azungumze ivo
 
Siasa si uadui wala chuki ndo maana kiongozi fulani anaweza kupondea sana chama fulani lakini keaho akajiunga nacho. Mfano juzi kati tu waziri fulani kamsifia kiongozi fulani wa upinzani kuwa ni mchapa kazi
 
Kwa hiyo inabidi act wachukue nafasi ya CUFCCM???
 
well, Ushauri wngu kwa CHADEMA, msithubutu hata kidogo kujibu hoja za CUF, mkitaka wajione wajinga na wasiojua kitu kaeni Kimya msijaribu kusema anything. Huo ni mtego, CUF inaonekana imekuwa taasisi ya CCM kama zilivyo UVCCM, BAKWATA, etc wao wanafuata kuhimiza yale aliyosema Kikwete.

Ukijibizana na kichaa na wewe utaonekana Kichaa! Please Be careful

Kwani UKAWA IMEISHIA WAPI
 
Yani ukawa ni unafiki tu, lipumba mnafiki,Mnyika mnafiki,Mbowe mnafiki,mbatia ndo mnafiki wa mwisho wanawahadaa watanzania kuwa watawakomboa wote wezi tu,
 
Na Benedict Kaguo, Pangani

MWENYEKITI wa Taifa wa Chama cha Wananchi CUF Profesa Ibrahim Lipumba amesema Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hakina nia thabiti ya kupambana na ufisadi kutokana kuchochea mgawanyiko wa Watanzania.


Alisema chama chochote cha siasa kilichoshindwa kuthamini matakwa ya wananchi wake hakina nia ya dhati ya kuwaletea ukombozi wa kweli wanaouhitaji Watanzania kwa sasa.


Profesa Lipumba alitoa kauli hiyo wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika mji wa Pangani katika mwendelezo wa mikutano ya chama hicho 'kuwazindua Watanzania katika kujenga demokrasia ya kweli hapa nchi'.


Alisema wafanyabiashara wa Chadema hawawezi kuongoza mapambano dhidi ya ufisadi kwa kuwa tayari wako katika mazingira ya kukumbatia rushwa, hivyo ni vigumu wao kuongoza mapambano hayo kama wanavyodai.


“Ndugu zangu wafanyabiashara na wapiga disko wa Chadema wanataka kuwang'oa mapapa ya ufisadi wa CCM ili wao manyangumi ya ufisadi waweze kuingia madarakani, hawana nia thabiti ya kupambana na rushwa,” alisema Profesa Lipumba.


Alisema aliingia kwenye siasa kwa lengo la kuwasaidia Watanzania sio kutafuta sifa kama walivyo baadhi ya wanasiasa wa Chadema.


"Sikuingia kwenye siasa kutafuta sifa, nimeingia kutumia elimu yangu kuwatafutia ukombozi Watanzania wenzangu, sasa hawa Chadema hawawezi kuiondoa CCM kwa kuwa wanachochea mgawanyiko mkubwa ndani ya nchi kwa kuwatukana Wanzanzibari waliokubali Serikali ya Umoja wa Kitaifa,” alisema Profesa Lipumba.


Awali, Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Bw. Julius Mtatiro alisema taifa linaangamia kwa kukosekana uongozi ulio madhubuti sasa ni wakati wa Watanzania kuzinduka ili uchaguzi mkuu ujao waweze kukipa ridhaa chama makini cha CUF.


“Maisha yamekuwa ya kubabaisha huduma za afya hospitalini mama zangu mnatakiwa mwende na nyembe mnapotaka kujifungua, serikali inashindwa kununua wembe lakini wakati wa uchaguzi inaweza kununua kitenge kwa kila mwanamke Tanzania nzima,” alisema Bw. Mtatiro.


Alisema wakati wa mabadiliko ndio huu na wananchi hawana budi kukiunga mkono chama hicho ili kiweze kuongoza mapambano dhidi ya rushwa, matumizi mabaya ya fedha za umma ili kuwakomboa wananchi.

Acha ukuda wewe..hii thread ya mwaka 2011 unaileta leo! Mxxx
 
Na Benedict Kaguo, Pangani

MWENYEKITI wa Taifa wa Chama cha Wananchi CUF Profesa Ibrahim Lipumba amesema Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hakina nia thabiti ya kupambana na ufisadi kutokana kuchochea mgawanyiko wa Watanzania.


Alisema chama chochote cha siasa kilichoshindwa kuthamini matakwa ya wananchi wake hakina nia ya dhati ya kuwaletea ukombozi wa kweli wanaouhitaji Watanzania kwa sasa.


Profesa Lipumba alitoa kauli hiyo wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika mji wa Pangani katika mwendelezo wa mikutano ya chama hicho 'kuwazindua Watanzania katika kujenga demokrasia ya kweli hapa nchi'.


Alisema wafanyabiashara wa Chadema hawawezi kuongoza mapambano dhidi ya ufisadi kwa kuwa tayari wako katika mazingira ya kukumbatia rushwa, hivyo ni vigumu wao kuongoza mapambano hayo kama wanavyodai.


“Ndugu zangu wafanyabiashara na wapiga disko wa Chadema wanataka kuwang'oa mapapa ya ufisadi wa CCM ili wao manyangumi ya ufisadi waweze kuingia madarakani, hawana nia thabiti ya kupambana na rushwa,” alisema Profesa Lipumba.


Alisema aliingia kwenye siasa kwa lengo la kuwasaidia Watanzania sio kutafuta sifa kama walivyo baadhi ya wanasiasa wa Chadema.


"Sikuingia kwenye siasa kutafuta sifa, nimeingia kutumia elimu yangu kuwatafutia ukombozi Watanzania wenzangu, sasa hawa Chadema hawawezi kuiondoa CCM kwa kuwa wanachochea mgawanyiko mkubwa ndani ya nchi kwa kuwatukana Wanzanzibari waliokubali Serikali ya Umoja wa Kitaifa,” alisema Profesa Lipumba.


Awali, Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Bw. Julius Mtatiro alisema taifa linaangamia kwa kukosekana uongozi ulio madhubuti sasa ni wakati wa Watanzania kuzinduka ili uchaguzi mkuu ujao waweze kukipa ridhaa chama makini cha CUF.


“Maisha yamekuwa ya kubabaisha huduma za afya hospitalini mama zangu mnatakiwa mwende na nyembe mnapotaka kujifungua, serikali inashindwa kununua wembe lakini wakati wa uchaguzi inaweza kununua kitenge kwa kila mwanamke Tanzania nzima,” alisema Bw. Mtatiro.


Alisema wakati wa mabadiliko ndio huu na wananchi hawana budi kukiunga mkono chama hicho ili kiweze kuongoza mapambano dhidi ya rushwa, matumizi mabaya ya fedha za umma ili kuwakomboa wananchi.

Nonsense!! Huu ni uongo uliokubuhu CCM kweli mnafanya kila hila kila kona UKAWA uvunjike. Ukawa hauwezi kuvunjika kwa propaganda kama hizi huu ni uongo mtupu kabisa
 
Yani ukawa ni unafiki tu, lipumba mnafiki,Mnyika mnafiki,Mbowe mnafiki,mbatia ndo mnafiki wa mwisho wanawahadaa watanzania kuwa watawakomboa wote wezi tu,


Hii thread ni ya karne 1 nyuma, imefufuliwa hapa kupunguza makali ya UKAWA mbona mara hii msumari umeganda..! ccm hamna mpenyo
 
Siamini prof lipumba anaweza sema hayo maneno. Sijui huyu alieleta hii mada ni nani
 
Mada ni ya 2011 imefufuliwa hata bana KWELI ukawa inawatiiiiiiiiaaaaaaaaaamshawashaaa
 
Stori ya mwaka 2011 ambazo zilisha exp kweli haya majanga
 
Makamanda wenzangu tusipanic hivi ni chanzo gani cha hiyo habari?
Je ni kweli hayo yamesemwa na Prof lipumba? Mimi sitaki kuamini hadi niaminishwe kwanza chanxo cha hii habari! Kwani hii habari ni ya lini?
Isije ikawa ni habari ya enzi hizo wakati ws ujima wakati vyama havijatambua adui yao ni yupi!
Enzi hizi za ukawa hayo hayawezi kuwa maneno ya Lipumba hata kidogo

tukiwaambia viroba hamnazo,mnakuja juu. Ndio maana mkaundiwa Bavicha ( baraza la vichaa chadema) hebu jipime na huo uzi na mchango wako huu
 
Back
Top Bottom