happiness win
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 2,461
- 1,394
Habari zenu mabibi na mabwana. Napenda kuwajulisha kuwa nimerudi likizo ingawa sikuwaaga.Likizo ina raha jamani, maana unapumzisha mwili, moyo, na akili. Si vibaya nikiwashauri wote muwe mnaenda likizo kwa faida yenu. Msing'ang'anie kuhangaika mwaka mzima bila kupumzika mkidhani ndio mtafanikisha malengo yenu katika utafutaji.
Make sure unapata muda mzuri wa kupumzika. Ikiwezekana jipangie kusafiri kwenda sehemu nyingine kipindi cha kupumzika. Sio lazima uende ulaya, hapa hapa TZ kuna sehemu nyingi za kukufurahisha na kukupumzisha kimwili na kiakili. Hata kama mambo yamebana, basi baki hapo hapo kwako ukijipumzisha.
Wape likizo hata watumishi wako, mke wako au mume wako! na utafurahia utendaji kazi wao/wake baada ya mapumziko.Kumbuka kipindi cha likizo si kipindi cha kuanzisha kazi, au shughuli nyingine, ni kipindi cha kupumzika! Furahia maisha.Usisahau kutenga bajeti ya likizo kila mwaka katika mapato yako!
Make sure unapata muda mzuri wa kupumzika. Ikiwezekana jipangie kusafiri kwenda sehemu nyingine kipindi cha kupumzika. Sio lazima uende ulaya, hapa hapa TZ kuna sehemu nyingi za kukufurahisha na kukupumzisha kimwili na kiakili. Hata kama mambo yamebana, basi baki hapo hapo kwako ukijipumzisha.
Wape likizo hata watumishi wako, mke wako au mume wako! na utafurahia utendaji kazi wao/wake baada ya mapumziko.Kumbuka kipindi cha likizo si kipindi cha kuanzisha kazi, au shughuli nyingine, ni kipindi cha kupumzika! Furahia maisha.Usisahau kutenga bajeti ya likizo kila mwaka katika mapato yako!