Lijue kusudi la wewe kuzaliwa hapa duniani kama binadamu

Lijue kusudi la wewe kuzaliwa hapa duniani kama binadamu

The redemeer

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2025
Posts
4,780
Reaction score
8,155
Wewe hukuzaliwa hapa duniani kama jiwe, mti, mdudu wala mnyama; ulizaliwa kimaalumu kabisa kama binadamu kwa LENGO au KUSUDI maalum; unatakiwa ulijue na ulitimize kabla hujaondoka kwenye uso wa hii dunia kurudi ulikotoka!

Haupo duniani ili mradi hupo tu, la hasha, hupo kwa ajili ya KAZI AU WITO MAALUM kama Yesu na wengi wengineo unaowafahamu!

Kila binadamu ni Masihi (yaani ni Kristo), mpakwa mafuta kwa ajili ya kusudi hili au lile.
Yesu alikuwa Masihi kwa ajili ya kusudi lake, mimi na wewe ni Masihi/ Kristo kwa ajili ya makusudi mengine.
Hakuna mbegu iliyofaulu kutunga mimba na kuzaliwa na mpaka sasa ipo ipo tu ili mradi tu.

Kama wewe ulifaulu kuingia kwenye tumbo la uzazi la mama yako, ukaishi miezi tisa na ukazaliwa mpaka sasa unaishi, wewe ni Kristo, ni Masihi, yaani mpakwa mafuta. Umepakwa mafuta utimize kusudi fulani kama tabibu, mwandishi, kiongozi, fundi ujenzi, mwalimu, askari, mkufunzi wa watu fulani, msanii wa maigizo, muziki nk.

Mimi sio wewe na wewe sio Mimi.
Mimi nilizaliwa kabla yako na wewe ulikuja baada yangu; sote ni Mitume kwa makusudi maalum!

Kabla hatujawa kwenye hii miili tunakuwa raia wa kudumu kwenye ulimwengu mwingine unaitwa ulimwengu wa roho (usioonekana, unaweza ita mbinguni au vyovyote, ili mradi ni ulimwengu usioonekana, wa kiroho)

Huko kuna viongozi wetu wakuu ambao tunafanana nao, walitutangulia kuwepo, tunaweza kuwaita kila aina ya majina kama vile, Miungu, Mabwana, Wazee nk. ili mradi tu kuonesha vyeo vyao vya ukuu kuliko sisi.

Hawa Miungu, Mabwana, Wazee wa Siku (Ancestors) kila mara hukaa Kikao kuhusu nani atumwe aje duniani kwa kusudi maalum.
"Nimtume nani?"
Sauti ya Mzee wa Siku (Ancient of the days) ilisikika kwenye Kikao/ jopo la wazee wenzake.

Kisha ikaendelea, "Ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu?"
Yaani nani mwakilishi atakayekuja huku duniani kwa niaba ya hao wazee wa Siku (Gods and Lords) kwa ajili ya kusudi maalum.

Mmoja wapo kati yetu (au wale ambao hawajazaliwa huku duniani) akajibu "Mimi hapa, nitume Mimi" (Isaya 6:8)

Huyo Mjumbe Mimi au wewe akatumwa kwa kupewa maelekezo maalum... "Nenda kafanye moja mbili tatu ..." (mstari wa 9)

Ukimaliza urudi hapa.

Hivi ndivyo Wazee wetu hufanya kila sekunde, kila dakika, kila saa, kila siku, wanatuma wawakilishi wao.
Mimi nilitumwa tarehe 24/7 miaka zaidi ya 45 iliyopita for a special purpose of teaching, healing the sick, pamoja na mambo mengine, of which naendelea nayo mpaka sasa, tangu nijitambue!

Wewe ulitumwa tarehe ngapi, mwezi wa ngapi na mwaka gani?

Tell me.

Na je, wajua ulitumwa ukafanye kazi gani?

Ndiyo kazi unayoifanya hata sasa au bado unakimbia kimbia tu huku na kule bila kujitambua?

Wakati wako wa kuondoka faili lako litakuwa lina taarifa iliyoshiba au ndo yale mafaili yaliyo wazi, ya Mitume/ Masihi wazembe?

Utawaambia nini wazee wako waliokutuma huku duniani?

Tafakari.

NB: Kuna watu wanaweza kukwazwa na matumizi ya viwakilishi "Wazee, Mabwana, Miungu..." nilivyotumia, lakini hilo lisiwe tatizo, nyie wekeni maneno yenu wenyewe "Bwana Mungu" au "Bwana Yesu" au "YEHOVA" au "Allah" nk ili mradi tukubaliane sote kuwa mmetumwa for special purpose na waliotuma ni Wazee wa zamani sana (Wazee wa Siku) ambao waliwahi kukaa Kikao huko zamani na kusema "Tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa SURA YETU, wakatawale . . ." (Mwanzo 1:26)

Hoja Kuu: Unakubali kwamba wewe umetumwa kwa kusudi maalum?

Fuatana nami katika sehemu ya pili ya Somo hili.
 
LIJUE KUSUDI LA WEWE KUZALIWA HAPA DUNIANI KAMA BINADAMU!

Sehemu ya 2.

Unapokubali utume au wito (calling) wa kuja huku duniani, ulimwengu wa roho unafanya kila linalowezekana uje huku duniani uzaliwe katika mwili wa damu na nyama.
Anakuwa ashachaguliwa mwanamke maalum wa kukupitisha ili upate mwili wako hapa duniani na huanze maisha ya utumishi wako hapa hapa duniani ukiwakilisha Ancestors wako kama tulivyokwisha kubaliana (Rejea kuzaliwa kwa Yesu na kuandaliwa kwa mwanamke Mariam)

Kwa wasio na taarifa, ni kwamba, hata Mungu wa Wayahudi/ Waebrania ni Ancestor, ndio maana ya kuitwa "MZEE WA SIKU" na huko alipo amezungukwa na wazee wenzake 24, wakimsikiliza kila sekunde na kutekeleza maelekezo yake (kwa mujibu wa maandiko ya Kigiriki)

Wewe unawakilisha Wazee, Miungu, Mabwana nk; wanaoishi kwenye Ulimwengu usioonekana au Ulimwengu wa kiroho (ita mbinguni ukipenda)

Umekuja for a special task. You have to know, yaani lazima ujue.
Usipojua na ukafa/ ukaondoka bila report ya uhakika ya wito/ utume wako, my friend, una kesi ya kujibu (nitaongelea hili huko mbeleni)

Ndio maana Wazee (Stars/ Planets), wewe Waite may be malaika, roho, Miungu, mizimu nk, ni sawa tu, ili mradi umefurahi;🤪 kwenye Siku yako ya kuzaliwa wanakuwepo kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa, wakiwa mashuhuda wa wito wako. Wajiridhishe kuwa umeshapata mwili wa damu na nyama wa kuingia ili jukumu lako lianze from that particular day.

Walioangaziwa akili zao (enlightened) huko zamani walihakikisha wanaliishi kusudi lao na waliwasadia watoto wao kuliishi.
Walipolikamilisha waliondoka bila madeni yoyote ya kulipa.

"Kwa maana DAUDI alipokwisha KULITUMIKIA SHAURI LA MUNGU katika kizazi chake, ALILALA, akawekwa pamoja na wazee wake" (Matendo ya Mitume 13:36)

Mimi na wewe tuna SHAURI/ KUSUDI la kutimiza, ambalo tumetumwa KULIKAMILISHA ndipo tufe (kimwili), kiroho turudi home (kwa wazee wetu au kwa Mungu wetu, mbinguni, kwenye Nchi nyingine ya kiroho tulipotoka)

Wewe ulizaliwa uwe mwanamuziki, lakini unafanya biashara; unapoteza muda.
Ulizaliwa uwe mwanasiasa lakini unafundisha, unapoteza muda.
Ulizaliwa uwe Kiongozi wa kisiasa au kijamii lakini hupo jeshini, umejichanganya!

Hata kama unapata hela, hizo hela hazitakupa furaha hata kidogo isipokuwa zinaweza kukuongezea matatizo kwa sababu hazikuja kwa njia sahihi.
Kama unafanya kazi yoyote ambayo inakupa fedha (mshahara) lakini huna raha nayo, hiyo sio kazi yako, umekalia kiti cha mwingine, ondoka utafute kiti chako; la sivyo utaadhibiwa, trust me!

Ulizaliwa makusudi kuanzia March 21 hadi April 20 (kwenye hizo tarehe na huo mwezi) ili ufanye kazi za nguvu!
Wewe ni Punda (Aries) una kichwa kikubwa; umezaliwa kubeba mizigo mizito kama Wanyamwezi🤣

Ukifanya kazi zisizo za nguvu utaugua magonjwa na ufe mapema au hutapata raha. Ndio maana wanajeshi wote waliozaliwa kwenye mwezi March/April (Aries) wana raha na kazi zao, wana kipato na maisha yao ni mazuri sana, tofauti na waliozaliwa miezi mingine.

Ulizaliwa kati ya April 21 na Mei 20?
Wewe ni Ng'ombe (Taurus)
Unatakiwa ujikite kwenye kazi za kilimo. Kodisha au nunua mashamba lima, Fuga utaona raha na fedha za kutosha. Umeitwa kuwa mzalishaji wa chakula, ili wana wa Mungu wale na kushiba. Mtu akifa kwa njaa kwenye mazingira yako, unalo deni nakwambia. Utayakumbuka maneno yangu ukiwa umechelewa, labda unielewe leo na uchukue hatua.

Labda utaniuliza; mbona nafanya kazi fulani na inanipa raha, furaha na amani na napata fedha za kutosha?
Jibu: Fedha hizo ni halali?
Kama ni halali, basi ni sehemu tu ya wito wako, kama kazi yako haihusishi kilimo na mifugo (ardhi), ni ya ziada tu, sio basic!
Taurus nyie ni watu wa ardhi, ingawa pia mmejaaliwa sauti nzuri sana na za kipekee mnaweza kuimba muziki pia mkapata furaha, amani na fedha nyingi.

Wewe Gemini; ulizaliwa kati ya Mei 21 na Juni 20.
Kazi zako ni kuongea my friend.
Pambana uwe msemaji wa Yanga🤣

Kama hupendi soka tafuta kuwa msemaji wa Serikali walau ya eneo lako au ingia kwenye siasa uwe Mweneza sera za chama; achana na udaktari. Madaktari ni wale waliozaliwa kati ya August 23 na Sept 22. Akina Virgo. Hawa wamezaliwa kuwa matabibu au kulima na kufuga, sio kuongea ongea.
Wewe Gemini, my friend, kwenye udaktari huwezi nakwambia, utaishia kutoboa Siri za wagonjwa wako!
Nenda kasomee uandishi wa habari au uanzishe ki-web chako au ki-online TV mbona utaEnjoy sana life na hela itakuja!!!

Cancer unaenda Jeshi?!
Maajabu, utaishia kwenye stress nakwambia. Wewe ni mtu wa kukaa home ukishughulikia mali za ukoo/ familia, ukisoma vitabu na kuchimba historia ya vizazi na vizazi na kazi kama hizo. Wewe utakuwa bora maeneo hayo maana u mtulivu sana rafiki yangu; huna makelele na hupendi makelele kabisa; ni Mzee wa kujichimbia. Unafaa kuwa daktari pia uponye watu.
Ukishindwa kote huko anzisha kijitaasisisi chako cha kusaidia wajane, wazee na watu waishio kwenye mazingira magumu, utapenya sana. Utapiga hela halali na pia utakuwa mtu unayeipenda sana kazi yako.

Ukikutana na mtu hapendi kazi yake, mpatie ushauri maana unaweza kuta hakuja duniani kwa ajili hiyo.

Huko wapi ndugu yangu Mr. Leo? Mzee wa misifa na mikogo!!😃

We jamaa mahali pako ni kwenye Creativity industries.
Wewe ni msanii mzuri wa maigizo, mtunzi wa hadithi, mwandishi wa vitabu, mwimba muziki kama Taurus na kina Libra nk. Wekeza nguvu na muda wako huko. You're born a leader; nenda ukaanzishe kitu maana ninyi mmekuja duniani kubuni vitu, mle raha na muwe matajiri wakubwa. Anzisha vitu, coach watu ndo mahali penu huko, ila kilimo, ufugaji, vibanda vya M-PESA nk. hayo hayawahusu!
Ukimtaka kocha mzuri (good mentor) kwenye mambo yako tafuta hawa kina Leo/ Simba, ni Waalimu kwa asili, watahakikisha jambo lako linafanikiwa, ila usisahau hawatawaliki, nenda nao kwa akili sana; kukuzingua ni chap🤣

Wale wazee wa maono, ndoto, mafunuo, unabii na mambo ya kiroho; enyi Samaki (Pisces)

Nyie mmekuja duniani kuwaletea watu maono ya kimbingu. Mnajua sana kutulia kwenye 'uwepo' (wazee wa meditation) huwa hampendagi makelele kabisa.

Nyie ndo mnatakiwa kuwa viongozi wa dini (kiroho) maana mna connection ya haraka kwenye spiritual realm.

Asiyeamini amtafute Samaki/ Pisces, mtu aliyezaliwa kati ya Feb. 20 na Machi 20, aniambie kama hawa watu wanapendaga makelele!!!
Au kama hawaotagi ndoto za kweli!
Hawa nakwambia wanaona sana maono na kwa kweli hawa watu kama ni dhambi, wanazo kidogo mnooo maana huwa hawapendi hata makundi. Hayo mambo ya magrup wapelekee kina Libra na Aquarius na Gemini, hao ndio kutengeneza marafiki kwao ni simple. Kwenye mabasi ya mikoani, kwenye daladala au mwendokasi za Dar, hawa ndio uwa wanateka mijadala yote!

Somo litaendelea....
 
Wewe hukuzaliwa hapa duniani kama jiwe, mti, mdudu wala mnyama; ulizaliwa kimaalumu kabisa kama binadamu kwa LENGO au KUSUDI maalum; unatakiwa ulijue na ulitimize kabla hujaondoka kwenye uso wa hii dunia kurudi ulikotoka!

Haupo duniani ili mradi hupo tu, la hasha, hupo kwa ajili ya KAZI AU WITO MAALUM kama Yesu na wengi wengineo unaowafahamu!

Kila binadamu ni Masihi (yaani ni Kristo), mpakwa mafuta kwa ajili ya kusudi hili au lile.
Yesu alikuwa Masihi kwa ajili ya kusudi lake, mimi na wewe ni Masihi/ Kristo kwa ajili ya makusudi mengine.
Hakuna mbegu iliyofaulu kutunga mimba na kuzaliwa na mpaka sasa ipo ipo tu ili mradi tu. Kama wewe ulifaulu kuingia kwenye tumbo la uzazi la mama yako, ukaishi miezi tisa na ukazaliwa mpaka sasa unaishi, wewe ni Kristo, ni Masihi, yaani mpakwa mafuta. Umepakwa mafuta utimize kusudi fulani kama tabibu, mwandishi, kiongozi, fundi ujenzi, mwalimu, askari, mkufunzi wa watu fulani, msanii wa maigizo, muziki nk.

Mimi sio wewe na wewe sio Mimi.
Mimi nilizaliwa kabla yako na wewe ulikuja baada yangu; sote ni Mitume kwa makusudi maalum!

Kabla hatujawa kwenye hii miili tunakuwa raia wa kudumu kwenye ulimwengu mwingine unaitwa ulimwengu wa roho (usioonekana, unaweza ita mbinguni au vyovyote, ili mradi ni ulimwengu usioonekana, wa kiroho)

Huko kuna viongozi wetu wakuu ambao tunafanana nao, walitutangulia kuwepo, tunaweza kuwaita kila aina ya majina kama vile, Miungu, Mabwana, Wazee nk. ili mradi tu kuonesha vyeo vyao vya ukuu kuliko sisi.

Hawa Miungu, Mabwana, Wazee wa Siku (Ancestors) kila mara hukaa Kikao kuhusu nani atumwe aje duniani kwa kusudi maalum.
"Nimtume nani?"
Sauti ya Mzee wa Siku (Ancient of the days) ilisikika kwenye Kikao/ jopo la wazee wenzake.

Kisha ikaendelea, "Ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu?"
Yaani nani mwakilishi atakayekuja huku duniani kwa niaba ya hao wazee wa Siku (Gods and Lords) kwa ajili ya kusudi maalum.

Mmoja wapo kati yetu (au wale ambao hawajazaliwa huku duniani) akajibu "Mimi hapa, nitume Mimi" (Isaya 6:8)

Huyo Mjumbe Mimi au wewe akatumwa kwa kupewa maelekezo maalum... "Nenda kafanye moja mbili tatu ..." (mstari wa 9)

Ukimaliza urudi hapa.

Hivi ndivyo Wazee wetu hufanya kila sekunde, kila dakika, kila saa, kila siku, wanatuma wawakilishi wao.
Mimi nilitumwa tarehe 24/7 miaka zaidi ya 45 iliyopita for a special purpose of teaching, healing the sick, pamoja na mambo mengine, of which naendelea nayo mpaka sasa, tangu nijitambue!

Wewe ulitumwa tarehe ngapi, mwezi wa ngapi na mwaka gani?

Tell me.

Na je, wajua ulitumwa ukafanye kazi gani?

Ndiyo kazi unayoifanya hata sasa au bado unakimbia kimbia tu huku na kule bila kujitambua?

Wakati wako wa kuondoka faili lako litakuwa lina taarifa iliyoshiba au ndo yale mafaili yaliyo wazi, ya Mitume/ Masihi wazembe?

Utawaambia nini wazee wako waliokutuma huku duniani?

Tafakari.

NB: Kuna watu wanaweza kukwazwa na matumizi ya viwakilishi "Wazee, Mabwana, Miungu..." nilivyotumia, lakini hilo lisiwe tatizo, nyie wekeni maneno yenu wenyewe "Bwana Mungu" au "Bwana Yesu" au "YEHOVA" au "Allah" nk ili mradi tukubaliane sote kuwa mmetumwa for special purpose na waliotuma ni Wazee wa zamani sana (Wazee wa Siku) ambao waliwahi kukaa Kikao huko zamani na kusema "Tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa SURA YETU, wakatawale . . ." (Mwanzo 1:26)

Hoja Kuu: Unakubali kwamba wewe umetumwa kwa kusudi maalum?

Fuatana nami katika sehemu ya pili ya Somo hili.
Yesu wengine kawaita "shetani, wengine "mbwa" na wengine kondoo.
 
Yesu wengine kawaita "shetani, wengine "mbwa" na wengine kondoo.
Inategemea ujumbe ulilenga nini kwa maana aliongea kwa mifano.
Mfano Petro aliitwa shetani " toka nyuma yangu eeh shetani" pale sio Petro alikuwa shetani
 
mmh sasa kama tuliletwa kwa kusudi fulani kwa nini hilo kusudi liwe siri hata sisi wenyewe hatulijui?? ingefaa tuwe tunazaliwa kukijua lililotuleta. Cancer unazaliwa ukanda wa gaza.. vita kila siku halafu unasema huwezi kuwa mwanajeshi.....

msituchanganyeeeeee
 
mmh sasa kama tuliletwa kwa kusudi fulani kwa nini hilo kusudi liwe siri hata sisi wenyewe hatulijui?? ingefaa tuwe tunazaliwa kukijua lililotuleta. Cancer unazaliwa ukanda wa gaza.. vita kila siku halafu unasema huwezi kuwa mwanajeshi.....

msituchanganyeeeeee
Kujua kusudi ni hadi uijue namba yako ya maisha ni ipi yenyewe imeeleza kila kitu kuhusu wewe umekuja Duniani kufanya nini
 
.
Utumwa wa kweli ni pale mtu anapopoteza maamuzi yake ya ndani kwa kufuata:

  • Mafanikio ya nje yasiyoendana na kusudi lake,
  • Mitazamo ya watu badala ya sauti ya moyo,
  • Vigezo vya jamii badala ya ukweli wake wa ndani.

Uhuru wa kweli huanza pale mtu anapochagua kusikiliza nafsi yake, kufuata mwanga wake, na kuishi maisha ya ndani kwenda nje — si nje kwenda ndani.

Hapo ndipo mtu huwa hai kweli, huru, na mwenye utimilifu. 🌱✨
 
Na walioitwa mbwa wenye biblia unawajuwa?
Aaah usiwape mbwa kilicho kitakatifu.
Mbwa ni mtu yeyeto asiyejua thamani ya maarifa umpayo ni sawa na kupoteza mda wako kumuelimisha mjinga
 
Aaah usiwape mbwa kilicho kitakatifu.
Mbwa ni mtu yeyeto asiyejua thamani ya maarifa umpayo ni sawa na kupoteza mda wako kumuelimisha mjinga
Jikumbshe, unaonesha una fikra zako zaidi ya za Yesu:

22 Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.
23 Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.
24 Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.
25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.
26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

27 Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.
 
Back
Top Bottom