Libya yazima Mohammed Enterprises

Kuwa na urafiki na Libya ni sawa swa kuwa na urafiki na mamba. Huyu Gadafi kaleta machafuko mengi sana hapa Africa. Kamuuwa Tolbert , na sankara Tom. Kumyenyekea gadafi msilaumu Kikwete. hata Nyerere amlinyenyekea sana gadafi. Kumbuka wakati ule alipoingilia vita vyetu na Uganda mwaka 1978 na kututia hasara nyingi. Watanzania karibia wote tulimlaani sana Gadafi kasoro Nyerere tuu. Maana Nyerere alienda mkutanoni wa OAU Libya na kumpigia debe gadafi achaguliwe kuwa mwenyekiti wa OAU huku akijua wazi kuwa wanachi wake wengi na mataifa mengi ya Africa,wamemkasirikia Gadafi. Sasa msimlaumu kikwete kama Nyerere nae aliingia mtegoni humo.
 
Unajua ndugu yangu humu kuna watu wenye nia ya kuongeza idadi ya post zao bila kujali kile wanachochangia kina mchango gani kwa taifa au jamii. Halafu hili tatizo la udini linaelekea kuwatia upofu watu kiasi cha kushindwa kufanya tathmini ya mambo kwa macho mawili. Katika historia ya nchi hii serikali haijawahi kukopa kulipia masuala ya kiimani, lakini kwa bahati mbaya kwa sababu watu walidhani ni deni lilitokana na uongozi wa rais wanayemchukia kwa sababu zao basi wakadhani huu ni wakati wa kumtia 'hatiani' kumbe maskini ni deni linaloihusu awamu inayoheshimika sana, tena kwa masuala ya kimaendeleo kwa nchi yetu! What a shame for these irresponsible people.

Na baada ya ukweli kufahamika wameikimbia thread, hutawaona tena wakichangia
 
Naomba tu tunapojadili masuala muhimu ya nchi tuwe serious na tuachane na upotofu na dhihaka. Tangu lini Libya, Iran au hata Saudi Arabia zikajenga misikiti kwa deni? Au katika suala hili pia wataka utie udini wako wa kunuka?Sikulaumu wewe, nalaumu elimu mbovu uliyopata, au kama umesoma at all.
ukweli, kusoma na kuelewa ni vitu vitatu ambavyo aghalabu hulandana viwiliwapo ama husharabina baadhi, tambua ukijengewa msikiti hata kama hukulipa shekeli, kwa nadharia umekopeshwa!!! naam! umekopeshwa imani. kwa vitendo utalipa kwamba mwarabu kuwa mungumtu, kama unabisha mtaje mwislam mmatumbi (mwafrika) mmoja aliyethubutu kumbishia mwarabu kwa kadri ya ufaham wako. usiwatishie watu ufaham, nakwambia hivii ufaham hauna mmiliki bali watu hupewa na mungu, utaamua mwenyewe kama mungu wa wabantu au utaamua kujitosa kulipa deni.
 
Jamani,kama deni hili ni la mwaka 1983 ni sawa,manake zama hizo ukweli matumizi yake hayakuchakachuliwa.Na kwa upeo wa Mwalimu JK,uwezo wake wa kumtumia yule ambae wengi wamemuona kama adui [IF YOU CANT DEFEAT THEM JOIN THEM],Nyerere aliweza kuishi na kuongoza Taifa liloheshimika kwa kutochaguliwa nini cha kufanya.Libya na mafuta yake ilikua ni kitu muhimu sana kuishi nao kwa umakini sana wa KIDPLOMASIA na pamoja tofauti zote za kumsaida Idd Amini kutupiga.

Bado Mwalimu aliyahitaji mafuta yake Ghadaf kuendeshea maisha yetu watanzania.Ndio maana ilifikia hatua yeye binafsi akapokea pesa kuwasaidia Watyama wenzake wenye imani ya Kiislamu kujenga msikiti pale Butiama,kwa nia njema ya undugu na si kwa nia mbaya kama ambazo zama hizi watu wanajalibu kutuonyesha sasa.

Hivyo hakika kama deni hilo ni la mwaka huo tajwa basi ni kweli.Hongera yangu ni kwa ubalozi wa LIBYA,kwa kuzuia dili hilo la kuchakachua kumature na kuongeza mzigo wa kilio cha umaskini wa watanzania.Ndio maana kidplomasia Tanzania imekaa kimya sana kwenye swala la LIBYA na siasa zake zinazoendelea kimataifa na NATO kusimamia mchakato mzima wa kumuondoa Ghadaf baada ya matendo yake ya gadhabu ya Walibya kupambana nae kumtoa yeye Ghadaf madarakani.

Kwa kuwa ndani ya mchakato huo wa kumuondoa Ghadf kuna Mheshimiwa [Nchi] nae kwa maswala ya Interest yuko makini na kwa kuwa nasi tuna interest zetu pia kama Nchi basi tumechuna kulaumu mateso wanayopata raia wa libya kwa kuwa mtendaji wa hayo ni swahiba wetu kimaslahi japo hatupendezwi na aliyoyatenda basi tutakaa kimya.

Ila usanii kutuibia kwa kusingizia kesi hizo nashukuru walibya kwa kushituka huko,vinginevyo wasingeshituka wao jamani watu wangechakachua pesa ya kula bata na kuandaa mazingira ya kumtafuta mkuu wa kusimamia missiontown na si kiongozi wa TAIFA.

Jamani hawa watu awaamini kuwa watu wameshashituka jamani,wanafuatilia kila dili wanalofanya.Haijalishi wewe ni nani,una madaraka gani siku watu wakiamua kuwachana patakua hapatoshi.Walibya wamesema mfumo wao wa kudeal na maswala Serikali kama Nchi uwa ni Nchi na Nchi.Mfumo wa kudeal na Mtu na Nchi ni wa Watanzania pekee.

Issue hizi za kisanii jamani tuishi hivi kwa usanii wa matendo dhamila zetu zinatwambia nini ndani ya mioyo yetu,Watawala wetu wanataka kuaachive nini?Na kama wanaimani,Imani yao inatofauti gani dhidi ya imani za watanzania wengine kupitia madhehebu yao.Manake matendo hayo wakati mwingine ni tofauti na ubinadamu.

Hakika watendaji wa michongo hiyo wanajiona ni wajanja sana kuzidi watanzania wengine na kuwa wanamaarifa ya kutafuta fedha zaidi kuliko watanzania wengine.

Sawa wakati mwingine nikitafakali sana uwa naumia ukiwakuta watanzania walio mitaani haswa wenye ufahamu mdogo kulingana na uwezo wa elimu yao,wanatabia ya kuwasifia wafanyabiashara wakubwa hapa Nchini utasikia fulani anafedha kuzidi fulani laiti kama wangeambiwa ukweli japo robo sifa hizo wangeamishia kuwasifia mama zao wanaouza genge mtaani kwao.

Ni vyema pia serikali ikaasisi mfumo wa kutupatia taarifa Wafanyabiahara wetu wa kitanzania wanathamani kiasi gani ya utajiri wao na kutuonyesha shughuri zao zote halali kwa faida ya kutathimini na kuwapongeza hata kwa kuwapa nishani kwa mchango wao wa ujenzi wa Taifa kwa kutoa ajira na kuinua pato la Taifa.

Serikali ilishajitoa kuwa HAIFANYI BIASHARA,hivyo basi mapato ya serikali yanategemea kodi na vyanzo vingine,hivyo wafanyabiashara hawa ambao ni walipa kodi tuambiwe kwa mfano kwa mwaka huu Kampuni fulani inayomilkiwa na fulani mwaka huu imelipa kodi kiasi kutaokana na shughuri kadha wa kadha.Kujitoa kufanya biashara basi tushindwe kusimamia biashara na michakato ya hawa waliochiwa kufanya biashara hizo.

Mfano deni hilo la walibya hatujui lilinunuliwa na MeTL kwa bei gani?Mambo yawekwe wazi.manake sikuwatanzania watakapo yaweka wazi wenyewe basi sipati picha yatakuaje.
 
na baada ya ukweli kufahamika wameikimbia thread, hutawaona tena wakichangia

yaani chuki zingine hazina msingi,,badala ya kuchangia thread kwa mawazo huru mtu anakuwa biased na itikadi ya dini yake kaazi kweli kweli but siku moja tutafika tu wanakotaka.......tufike
 
jamani deni mmeambiwa limeanza 83 baada ya vita na idi amin sasa mbona mwalihusisha na kikwete?? Huu ujinga kutumia matashi chuki tamaa na kuacha hoja mantiki na ukweli tubadilike
 
naomba tu tunapojadili masuala muhimu ya nchi tuwe serious na tuachane na upotofu na dhihaka. Tangu lini libya, iran au hata saudi arabia zikajenga misikiti kwa deni? Au katika suala hili pia wataka utie udini wako wa kunuka?
Sikulaumu wewe, nalaumu elimu mbovu uliyopata, au kama umesoma at all.

waache waropoke wasiyoyajua,,,af baadae wakiona tumepost post hapa inayothibitisha ni deni la tokea awamu ya kwanza wote watakimbia na kubaki midomo wazi,,kama humpendi jk basi unatakiwa utoe tuhuma sahihi sio kila pumba unamhusisha nazo yeye.....
 
Tatizo si deni na si haki kulaumu utawala wa sasa wa JK kwa lawama hii ya kuwepo kwa deni hili,Ingawa lawama kwao nitazitoa pindi tukijua MeTL alilinua deni hili zama za utwala wa nani JK au zama za Mwalimu JK au waliofuata baada ya Mwalimu. ningependa kuona mjadala ni namna gani hawa walionunua deni hili.Manake kuwa tajiri sio dhambi,dhambi ni mbinu au mikakati iliyotumika kutafuta utajili huo.

Sisi kuwa na deni la Walibya sio dhambi, dhambi itakuwa ni jinsi tunavyo deal kulilipa deni hilo la Walibya.Manake hapo ndipo tunapoona sarakasi na maigizo.
 
Mimi nafurahi kwamba mjadala sasa umehama kutoka kujadili mtu au imani ya mtu na kwenda kwenye hoja. Na hoja hapa ni jinsi deni hilo linalogombewa lilivyofikia kuwa ni mali ya MeTL au MEISS na hili la suala la ushahidi na ufahamu wa ubalozi wa Libya. Hapa watu ni lazima waelewe kwamba kazi ya kuuza deni hilo haikuwa ya serikali ya Tanzania na wala haikuhusika. Uhusika wa serikali uko katika mikataba ya namna ya kulipa deni hilo na si vinginevyo. Kwa hiyo it doesnt matter deni hilo liliuzwa katika awamu gani ya uongozi, as long as uuzwaji huo haukufanywa na serikali ya Tanzania. Ni vizuri sasa kuelewa kwamba lawama dhidi ya JK na serikali yake katika suala la madeni haya ni misplaced na ni vizuri ikaeleweka kwamba siasa haipaswi kupewa nafasi katika hili.
 
Hivi hawa Libya si kuna wakati walipewa hotel moja iliyopo baharini (sina uhakika na jina) kama malipo ya deni hilo?

Sasa mbona mnaotetea hamlisemi hilo? Hivi sambamba na kupewa hiyo hotel, walilipwa nini zaidi?

Anyway, wanaoleta dini na wanaotetea deni, nafikiri tusubiri kidogo maana ukweli utaanikwa tu wazi.

Sasa hivi sidhani kama kuna anayejua ukweli wa ndani ni nini........

Deni la mwaka 1983......./Ujenzi wa misikiti......... vyote vyaweza kuwa na ukweli. Time will tell......
 
Hivi hawa Libya si kuna wakati walipewa hotel moja iliyopo baharini (sina uhakika na jina) kama malipo ya deni hilo?

Sasa mbona mnaotetea hamlisemi hilo? Hivi sambamba na kupewa hiyo hotel, walilipwa nini zaidi?

Anyway, wanaoleta dini na wanaotetea deni, nafikiri tusubiri kidogo maana ukweli utaanikwa tu wazi.

Sasa hivi sidhani kama kuna anayejua ukweli wa ndani ni nini........

Deni la mwaka 1983......./Ujenzi wa misikiti......... vyote vyaweza kuwa na ukweli. Time will tell......

Nadhani unazungumzia Bahari Beach Hotel ambayo inamilikiwa na kampuni ya Libya. Lakini hakuna popote ambapo imewahi kunukuliwa kwamba hoteli hiyo ilipewa kampuni ya Libya kama fidia ya deni hilo. In any case, hakuna uwezekano wa hoteli ile iliyokuwa imechoka ikawa ni fidia ya deni la dola milioni 42 achilia mbali jumla kuu ya deni ambalo lilifika dola 202 milioni.

Baadhi ya wachangiaji humu wanashangaza kwa fikra hasi kwa kitu ambacho hawana uhakika nacho. Hivi deni la milioni 42 ni sawa na gharama za misikiti mingapi kwa kiwango cha wakati huo. Nadhani kila mtaa nchi nzima ungekuwa na msikiti. Je, Nyerere au kiongozi yeyote angeweza kufanya hivyo i.e. kukopa hela za kujengea nyumba za ibada? Hivi kuna msikiti au kanisa nchi hii vimejengwa kwa fedha au udhamini wa serikali? Tuache kuzua mambo kwa nia ya kufanikisha lengo la kuhitimisha chuki kwa rais. Kama nilivyosema awali, uhusika wa serikali katika kujua nani apewe deni gani haupo. Choice ni ya walibya wenyewe.
 
Kikwete hakupigana Vita vya Uganda akiwa Jeshini? haoni kuwa Ghadaffi kwa kumsaidia Amin Uchumi wa Tanzania Ulidhoofika sababu ya kununua silaha kwa third party? Tanzania kabla ya vita hatukuwa na Deni IMF; Nchi ilikuwa na Foreign Currency Reservers; after War everything went Wrong

Sasa tunamkumbatia Ghadaffi na kutupa misaada ya kujenga Misikiti kwa Mkopo; we have to pay them later? what is this?

Sijakuelewa hapa. Mbona unachanganya habari wewe? Ni wapi imesemwa kuwa kuna mikopo ya misikiti?
 
Kuwa na urafiki na Libya ni sawa swa kuwa na urafiki na mamba. Huyu Gadafi kaleta machafuko mengi sana hapa Africa. Kamuuwa Tolbert , na sankara Tom. Kumyenyekea gadafi msilaumu Kikwete. hata Nyerere amlinyenyekea sana gadafi. Kumbuka wakati ule alipoingilia vita vyetu na Uganda mwaka 1978 na kututia hasara nyingi. Watanzania karibia wote tulimlaani sana Gadafi kasoro Nyerere tuu. Maana Nyerere alienda mkutanoni wa OAU Libya na kumpigia debe gadafi achaguliwe kuwa mwenyekiti wa OAU huku akijua wazi kuwa wanachi wake wengi na mataifa mengi ya Africa,wamemkasirikia Gadafi. Sasa msimlaumu kikwete kama Nyerere nae aliingia mtegoni humo.

Kwa matendo hayo ya Gaddafi ndio yanaharalisha uwizi wa Mohamed Dewji na baba yake?
 
Hivi Kikwete hakupigana Vita vya Uganda? Kwanini bado tuna Ubalozi wa Libya? hakuona Maumivu wakati wa hivyo vita; Ilitushushia GDP na pia tulilazimishwa kununua silaha kwa bei kali through a third party... Tanzania kabla ya VITA tulikuwa na enough foreign currency reserves hatukuwa na deni IMF after the war kila kitu kikaanguka...

Sasa Kikwete anamkumbatia Ghadaffi anatupa pesa za kujenga Misikiti kwa Mkopo tuna Madeni nao -- Is it shame on US? Kweli Tanzania soon we will see the results of AZIMIO LA ZANZIBAR

Kikwete anamkumbatia vipi Gaddafi?
 
Kesi hii imekwishaamuliwa leo asubuhi na Mohamed Dewji, Baba yake mzee Gullamabbas na mama yake mzazi, Bi. Zubeida wameonywa kuacha uongo na uwizi. Mahakama imeamuru pia kampuni iliyoomba pesa hizo kwa Serikali ya Libya ipewe hela zote ilizoomba ndani ya masaa 24.
 
Swali, je makampuni yanayonunua madeni ya serikali yanapata manufaa gani?

Mimi nielewavyo ktk nchi zilizoendelea kuna makampuni kazi yake kununua madeni sugu kwa bei pungufu kutoka kwa mdai na kisha kampuni nunuzi ya madeni kuchukua mzigo wa kuhakikisha inalipwa pesa zote toka kwa mdaiwa ( hapa Mohammed Enterprise na kina-MMN watailipa Libya pesa pungufu halafu kuikomalia serikali ya Tanzania ilipe deni lote).

Sasa basi kama ndivyo ilivyo, je serikali ya Tanzania ina uwezo wa kuilipa Moh'd ent. au MMN kiasi gani na serikali ya Tanzania itapata unafuu gani kudaiwa na Moh'd Ent/ MMN deni hili litakalouziwa na serikali ya Libya kwa makampuni ya ki-Tanzania? Je serikali ya Tanzania italipa hawa watarajiwa wa ununuzi wa deni kwa pesa za Shillingi za Tanzania au kwa pesa za kigeni? au watapewa migodi au madini n.k kama malipo ya deni hili lililoshindikana? Jambo hili linahitaji kufafanuliwa kwa undani jinsi Moh'd ent au MMN watakavyolipwa na serikali hii iliyofilisika ya Tanzania na walipa kodi watabebeshwa zigo gani?.
 
Baada ya kumalizika kwa kesi hii, sasa akina Mohamed Dewji wasubiri kesi ya jinai kwa kujipatia fedha za Serikali kwa njia ya udanganyifu
 
Nadhani unazungumzia Bahari Beach Hotel ambayo inamilikiwa na kampuni ya Libya. Lakini hakuna popote ambapo imewahi kunukuliwa kwamba hoteli hiyo ilipewa kampuni ya Libya kama fidia ya deni hilo. In any case, hakuna uwezekano wa hoteli ile iliyokuwa imechoka ikawa ni fidia ya deni la dola milioni 42 achilia mbali jumla kuu ya deni ambalo lilifika dola 202 milioni.

?

Baadhi ya wachangiaji humu wanashangaza kwa fikra hasi kwa kitu ambacho hawana uhakika nacho. Hivi deni la milioni 42 ni sawa na gharama za misikiti mingapi kwa kiwango cha wakati huo. Nadhani kila mtaa nchi nzima ungekuwa na msikiti. Je, Nyerere au kiongozi yeyote angeweza kufanya hivyo i.e. kukopa hela za kujengea nyumba za ibada? Hivi kuna msikiti au kanisa nchi hii vimejengwa kwa fedha au udhamini wa serikali? Tuache kuzua mambo kwa nia ya kufanikisha lengo la kuhitimisha chuki kwa rais. Kama nilivyosema awali, uhusika wa serikali katika kujua nani apewe deni gani haupo. Choice ni ya walibya wenyewe.

Inaonekana kuna watu humu ndani wamelipwa kupotosha ukweli wa kilicholetwa kama taarifa. Suala hapa ni kesi iliyokuwa mahakamani inayohusu fedha za Libya ambazo Serikali ya Tanzania ilikopa mafuta miaka ya themanini. Suala la misikiti linatoka wapi
 
Back
Top Bottom