Libya: Mapinduzi yatumbukia nyongo!

mpayukaji

JF-Expert Member
Oct 31, 2010
940
349
_60099096_alkeib.jpg

Waziri mkuu wa Libya al Keib pichani.

Habari kuwa ofisi ya waziri mkuu wa Libya Abdurrahim al-Keib imevamia na hajulikani aliko ni pigo kwa serikali mpya NTC. Je tatizo ni nini? Tatizo ni kuchukua madaraka bila kuwa na maandalizi au tamaa ya wale waliokuwa na Muamar Gaddafi wakamgeuka?

Je tatizo ni ukale wa mfumo ulioachwa na Gaddafi au ni umma kuanza kugundua kuwa kumbe wanasiasa si watu wa kuamini kama ilivyotokea Misri ambapo mapinduzi yametekwa na jeshi na mabaki ya Hosni Mubarak sawa na Libya?

Kwa habari kwa kina: BONYEZA HAPA.
 
We unaona inafundisha nini? Kwanza hii si hadithi bali habari.
 
Sure mradi tusiwatoe bila maandalizi ya kutosha kuhakikisha kuwa mapinduzi yetu hayatekwi na mapandikizi watakaohama CCM na kujiunga na upinzani baada ya kuona upepo unabadilika.
 
Sure mradi tusiwatoe bila maandalizi ya kutosha kuhakikisha kuwa mapinduzi yetu hayatekwi na mapandikizi watakaohama CCM na kujiunga na upinzani baada ya kuona upepo unabadilika.
Tanzania si Libya!

Hadithi hii haina uwiano wowote na TZ! Kwa Tanzania, kuna upinzani, kuna utawala wa sheria! Hata ikitokea upinzani ukachukua nchi, itakuwa labda sawa na Zambia, si Libya.

Hii naifananisha na enzi za kutishia wananchi kwa kuwaonyesha mikanda ya vita za Rwanda na Burundi!
 
Tanzania si Libya!

Hadithi hii haina uwiano wowote na TZ! Kwa Tanzania, kuna upinzani, kuna utawala wa sheria! Hata ikitokea upinzani ukachukua nchi, itakuwa labda sawa na Zambia, si Libya.

Hii naifananisha na enzi za kutishia wananchi kwa kuwaonyesha mikanda ya vita za Rwanda na Burundi!
Maandamano na mkesha wa Arusha na silaha alizokutwa nazo kiongozi fulani ambaye hakwenda kulala hotelini huo unauita ni upinzani unaofuata sheria?

Tatizo la Libya unalielewa, ni ukanda na ukabila. Mapinduzi ya kijeshi mara nyingi huwa na visasi na uasi. Hii inatufundisha kuwa ballot boxes ndiyo njia nzuri ya kufanya mabadiliko.
 
_60099096_alkeib.jpg

Waziri mkuu wa Libya al Keib pichani.

Habari kuwa ofisi ya waziri mkuu wa Libya Abdurrahim al-Keib imevamia na hajulikani aliko ni pigo kwa serikali mpya NTC. Je tatizo ni nini? Tatizo ni kuchukua madaraka bila kuwa na maandalizi au tamaa ya wale waliokuwa na Muamar Gaddafi wakamgeuka?

Je tatizo ni ukale wa mfumo ulioachwa na Gaddafi au ni umma kuanza kugundua kuwa kumbe wanasiasa si watu wa kuamini kama ilivyotokea Misri ambapo mapinduzi yametekwa na jeshi na mabaki ya Hosni Mubarak sawa na Libya?

Kwa habari kwa kina: BONYEZA HAPA.

Hilo ndilo jibu. Hao walikuwa opportunist.
 
Tanzania si Libya!

Hadithi hii haina uwiano wowote na TZ! Kwa Tanzania, kuna upinzani, kuna utawala wa sheria! Hata ikitokea upinzani ukachukua nchi, itakuwa labda sawa na Zambia, si Libya.

Hii naifananisha na enzi za kutishia wananchi kwa kuwaonyesha mikanda ya vita za Rwanda na Burundi!

Invi.....not that easy mkuu....ni suala la kuangaliwa kwa ukaribu na thadhari ichukulliwe as well........dhamira za wanasiasa ni sawa na msitu mkuu .................never to be taken for granted ni bora kujua hatari na isitokee kuliko kuachukulia kwa urahisi kama hivi

I beg to differ.......there are lessons in that movemement
 
Inawezekana kabisa wappo kati yetu hawajui kabisa maana ya mapinduzi ya umma (popular revolution). Wengi wanafikiria ni sawasawa na "mapinduzi ya kijeshi". Mapinduzi ya umma yanapotokea hadi kukamilika inaweza ikapita muda kwa sababu changamoto kubwa na ya kwanza kabisa - hasaa kwenye nchi kama Libya - ni kutengeneza mifumo mipya ya utawala ambayo haimzunguki mtu. Hii ni kazi kubwa waliyonayo Walibya and so far they are doing better.

Misri nako ni hivyo hivyo; ila angalau Misri kulikuwa na a strong military institution. Kazi ya Misri ni kutengeneza institutions nyingine za kiraia. Tunisia wao wako vizuri zaidi kwa sababu tayari walikuwa na very strong institutions ambazo hazikutetereka sana baada ya Ben Ali kukimbia. Kwao tatizo lilikuwa la mtu mmoja hasa badala ya system nzima.

Hivyo, ni vizuri kuangalia kesi hizi kila moja kivyake vyake badala ya kujaribu kuangalia zote kwa mkupuo. Mapinduzi hayafanani, na kukamilika kwake hakufanani! Miaka hamsini baadaye bado tunahangaika na mapinduzi ya Zanzibar!!
 
Inawezekana kabisa wappo kati yetu hawajui kabisa maana ya mapinduzi ya umma (popular revolution). Wengi wanafikiria ni sawasawa na "mapinduzi ya kijeshi". Mapinduzi ya umma yanapotokea hadi kukamilika inaweza ikapita muda kwa sababu changamoto kubwa na ya kwanza kabisa - hasaa kwenye nchi kama Libya - ni kutengeneza mifumo mipya ya utawala ambayo haimzunguki mtu. Hii ni kazi kubwa waliyonayo Walibya and so far they are doing better.

Misri nako ni hivyo hivyo; ila angalau Misri kulikuwa na a strong military institution. Kazi ya Misri ni kutengeneza institutions nyingine za kiraia. Tunisia wao wako vizuri zaidi kwa sababu tayari walikuwa na very strong institutions ambazo hazikutetereka sana baada ya Ben Ali kukimbia. Kwao tatizo lilikuwa la mtu mmoja hasa badala ya system nzima.

Hivyo, ni vizuri kuangalia kesi hizi kila moja kivyake vyake badala ya kujaribu kuangalia zote kwa mkupuo. Mapinduzi hayafanani, na kukamilika kwake hakufanani! Miaka hamsini baadaye bado tunahangaika na mapinduzi ya Zanzibar!!
Mzee Mwanakijiji Umesikiliza makongamano wanayofanya Wazanzibar kuhusu kupinga muungano???

Wanadai kuwa Mapinduzi yaliyotokea Znz hawakufanya wao hata kidogo.....Yalipangwa Na Nyerere na John Okello

Na Mapinduzi yalifanyika makusudi ili watawaliwe, na sasa hivi ndio wanadai nchi yao
 
Last edited by a moderator:
Mzee Mwanakijiji Umesikiliza makongamano wanayofanya Wazanzibar kuhusu kupinga muungano???

Wanadai kuwa Mapinduzi yaliyotokea Znz hawakufanya wao hata kidogo.....Yalipangwa Na Nyerere na John Okello

Na Mapinduzi yalifanyika makusudi ili watawaliwe, na sasa hivi ndio wanadai nchi yao

uzuri mmoja wa historia ni kuwa hakuna anayeweza kubadilisha. Unachosikia watu wanakisema ni 'historical revisionism'. Wanajaribu kuandika upya historia ili kuhalalisha matendo yao ya leo! HIvyo, wanaweza kuwavuta wale tu ambao ni wavivu wa kujifunza historia! Hakuna ushahidi wowote kuwa Nyerere alihusika na mapinduzi ya Zanzibar kabla ya kutokea! NONE WHATSOEVER.
 
Back
Top Bottom