Salaam wapendwa.
Leo nimepokea kwa huzuni habari za kifo cha aunty yangu(ulale pema peponi shangazi)
Allikua anasumbuliwa na saratani ya titi,
As a coincidence ,asubuhi hii pia nimesoma habari which I think some of you might have read,
Ilikua kwenye mtandao wa Yahoo,
Mwanamke ambaye alikua anajua anakufa aliomba wahudumu wa gari la wagonjwa(paramedics) wampeleke beach/ufukweni mwa bahari for one more time,ambapo walikubali kumpeleka.
Kwa kweli hizi habari zimenifanya nifikirie kama na mimi ningekua najua siku zangu za kuishi hapa duniani karibia zinafika ukingoni,ningelichukualiaje na kubalianaje na hili swala ????................
sasa mwana JF ningependa uchukue a minute or two kulifikiria, na wewe ungekua kwenye situation hio,ungefanyaje kukabiliana na hili?
Nimeona mahali kuna sehemu / hospice ambazo ni sehemu za wagonjwa wanaokaribia kufa/siku zao kukaribia ukingoni kukaa huko na specialized doctors and nurses mpaka wanapofariki…………………………..je ungekubali kwenda???...............hii inawapunguzia familia kukuona in pain na hivyo kuwaondolea na wao kuwa traumatized na kifo chako…………
Je tuna hospice ngapi nchini??? Nyingi zinahitajika?if yes, WHY and if no, WHY…….
Usiku saa hizi sijui kama ninaeleweka….
*Again lala pema peponi aunty-a woman should be kind,prayerful and hardworker,is what I have learned in your short but remarkable life*
Pole sana kufiwa na shangazi yako! Apumzike kwa amani! Kuhusu "Hospice" sina uhakika kama Tanzania zipo, na kama zipo basi huduma zake zikoje! Kwa wenzetu "Hospice" zina lengo mahsusi la kuwasaidia wagonjwa wa magonjwa sugu kama kansa kufa kwa amani, bila maumivu, bila mateso na bila mahangaiko! Wanajua kabisa wanakufa, lakini wanapata intensive care ya huduma za kimwili na kiroho hivyo hata ukiwatembelea wanakuwa na amani sana mpaka unaweza kushangaa! Ni msaada mkubwa sana kwa mgonjwa mwenyewe na hata kwa familia yake!