Leseni kwa walevi

Masalu Jacob

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2017
Posts
1,339
Reaction score
1,493
Habari !

Naomba kuuliza,

Hivi ikitokea siku TRA wakawatoza kodi wanywaji wa vileo hapa nchini inaweza kuwa ni wazo zuri, bora na njia nzuri ya kuzuia wimbi kubwa la unywaji wa pombe na vileo kiholela?

Kwamba iwe kwa kila mpenda unywaji pombe au kileo sharti awe na Leseni ya yake ya kugida;
1. Kiwango cha unywaji ( Idadi)
2. Aina za pombe (Ubora)
3. Unywaji wa kimataifa ( Vileo vya nje).

Sijui, watu wataweka wapi sura zao.


Karibu.
 
Ilishafanyagwa hii huko zanzibar kulikuwa na leseni maalum za kunywa pombe.
 
Mbona wanatoza sana tangu kitambo,
Iko hivi kila kinywaji unachonunua tayali washaweka kodi humo, labda kama unaongelea Kodi ya kusachi watu mifukono ,hiyo bado ndio iko jikoni sasa
 
Mbona wanatoza sana tangu kitambo,
Iko hivi kila kinywaji unachonunua tayali washaweka kodi humo, labda kama unaongelea Kodi ya kusachi watu mifukono ,hiyo bado ndio iko jikoni sasa
Sasa unakuwaje mlevi huna leseni ya kuonyesha wewe ni mlevi uliesajiriwa na nchi inatambua mchango wako
 
Kodi inakatwa huko huko viwandani,,lakini ata wanywaji wanakatwa kodi flan inaitwa[kodi usiyoihisi!! aka INDIRECT TAX!!
 
Ukilewa pombe za kienyeji faini iwe ndogo, ukilewa pombe za kisasa faini iwe kubwa🤪
 
Umefikiria na kuhusu wazinzi,wasrngenyaji,wezi/mafisadi na mashoga wafanyweje ili waache au kudhibitiwa tabia zao?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…