Sabayi
JF-Expert Member
- Dec 4, 2010
- 2,310
- 1,003
Ni kweli familia si jambo la siri, lakini ukumbuke kipindi cha yesu mpaka kifo chake alikuwa "NO BODY" amekuja kupata umaarufu miaka mingi baada ya kifo chake. Kama watu mashuhuri wakina Kaizari koo zao zilifutika kitambo, ni kitu gani kinakufanya uamini kuwa ukoo wa yesu ungeprevail? Hata ukoo wa Yosefu babaake yesu ulishafutika with no single trace!
Hahahahaaa eti Yesu hadi kifo chake aliuwa NOBODY alipata umaarufu miaka mingi sana baada ya Kifo chake maneno kama haya ndio yanayo onyesha uhafifu na udhaifu wa hoja ya kuwa Yesu alimuoa Maria Magdalena kwasababu hamumjui huyo Yesu hata Kidogo sasa kama yeye mwenyewe tu hamumjui mnajifanyaje kuijua familia yake? hebu anzeni kumjua yeye basi japokidogo tu kabla hamjaanza kuzusha hivyo vitu vingine nakupa facts chache kwanini Yesu alikuwa maarufu sana tu wakati bado yupo hai na baada ya Kifo na ufufuko wake
1. Yesu alikimbilia Africa (Misri) akiwa na miaka miwili kwasababu alikuwa anatafutwa na Herode auwawe kwa kuwa alipewa taarifa kuwa Mfalme amezaliwa kwasababu ya Yesu watoto wote wa kiume kuanzia Miaka miwili kushuka chini waliuwawa kwa lengo la kumuu Yesu - Kwa hivyo unaona Yesu alikuwa Maarufu tangu anazaliwa achilia mbali miaka mingi baada ya yeye kufa na hadi leo bado ni maarufu sana na ndo anawafuasi wengi kulimko yoyote yule
2.Aliwalisha watu elfu tano (bila kuhesabu wanawake na watoto) kwenye mkutano wake - kwa population ya wakati huo kukusanya watu elf tano (bila kuhesabu wanawake na watoto) haikuwa kazi rahisi na lazima uwe mtu maarufu sana - Unaona umaarufu wa Yesu mkuuuu!!!
3. Wayahudi waliamua aachiwe Baraba na Yesu afe kwasababu amejiita mfalme wa Wayahudi na pale msalabani waliandika huyu ni mfalme wa Wayahudi - hii ni wazi kuwa alijulikana na wayahudi wote rejea wakati anaingia Yerusalemu umati ulivyompokea na kumwita Mfalme wa Wayahudi - Na hiyo ndio sababu kubwa Pilato alimuhukumu Yesu japokuwa ilishaandikwa hivyo
4.Alivyofufuka Watawala walijitahidi sana kuficha habari zake wakasema wawaambie watu kuwa wanafunzi wake wamemuiba -Kwanini wafiche habari za ufufuo wake if he was nobody?
Ukihitaji mifano zaidi niambie