Unalalamiika mzee, kwenye bajeti yako si kuna kiwango ambacho unapaswa kujiwekea hata mtu aje wa namna gani isivuke hiyo au unaishi bila kuwa na planed budget ? savings unafanya kweli kama ndo mwendo huo? nimewahi kumdhamini mtu milioni 10 akalala mbele halafu ni ndugu sasa mtu kama huyo unamfanyaje? njia niliyojigundulia ni kuwa na kiwango kama ni 5% au 10% ya pato la mwezi kama kuna dharula ambayo naithibitisha maana hela kuzitumia ni rahisi ila kuzitafuta unatumia masaa mengi - kwa maoni yangu naona bado kuna mengi hujayapitia pitia ila ndo utanyooka tu atakapokupotezea kimya kimya maana umesaidia kwa kutarajia malipo fulani...na imekuuma pengine ni 25% au 50% ya mshahara wako...pole ndugu