Leo nilivyokwenda kupima UKIMWI!

Leo nilivyokwenda kupima UKIMWI!

Duu mkuu acha hizo unaaibisha wanaume bila shaka wewe ni mwanaume wa Dar
Kwanza ningependa kuwapa hongera watu wote walioamua kwenda kupima bila kujali majibu yalikuwaje. Kwa kweli kitendo cha kuamua kwenda kupima ni ujasiri wa hali. Mimi sikuwahi kuupata ujasiri huo mpaka mama alipotishia kuwa kama tusingeende kupima basi angesitisha huduma.

Sikua na jinsi ya kufanya, siku mbili hizi nimekuwa nawaza sana. Sasa leo nikasema ngoja nijipeleke mwenyewe kwanza. Ili nijue afya yangu kabla mamaa hajanipeleka kwa nguvu atakapogomea kutoa huduma.

Nikaenda hospitali. Nilipofika nikamwambia yule mhudumu. Nimekuja kupima kwa utashi na hiyari yangu mwenyewe. Najua kuna majibu ya aina mbili. Sitaki maelezo yoyote mengine naomba nipime. Jamaa akanielewa akanitoba akatoa damu. Sio siri nilitetemeka wakati nasubiri majibu. Nikasikia harufu ya kikwapa wakati asubuhi nilipaka deodorant. Dakika tano hizi nilikuwa kwenye hali ngumu sana.

Niliwaza mademu wote niliowahi kukutana nao. Baadae nikajipa moyo mbona kuna watu wanaishi na maambukizi. Mimi sitakuwa wa kwanza. Mhudumu akanistua. "Huko tayari kwa majibu yako". Hapo ndipo nilisikia harufu zaidi ya kikwapa. Midomo ikakauka. Nikajikamua. Nikamjibu "Ndio maana nimekuja kupima".

"Hauna HIV. HAUNA UKIMWI". Nikamuangalia. Nikashusha pumzi kwa nguvu. Nikamjibu. Asante sana. Nimetoka hapo nikajipongeza kwa Mirinda ya baridiiii.

Sasa nikirudi home. Nitamwambia wife, achague twende tupime wapi. Aseme mwenyewe. Nitajifanya sijapima. I hope na yeye atakuwa poa. Pengine amekwisha pima ndio maana kaanza figisu figusu. Nitawapa mrejesho.
 

Attachments

  • IMG_20181210_170317.jpg
    IMG_20181210_170317.jpg
    374.8 KB · Views: 31
Hakuna kitu ninachopenda kama kupima HIV, yaani kula nikiumwa nikienda hospital lazima nipime HIV na wingi wa damu,

Najiamini 100% niwe na wacwac wann
Kama unajiamini unapima kutafuta nini, kupima tafsiri yake ni kuondoa uatata juu ya whether you are +Veor -ve HIV status,

Usiseme unajiamini, kuna siku utapata suprise unayoitafuta.
 
Wajameni ninapenda kutumia Sana hivi ata kupima mizigo ya dharura ili ata rubber ikipasuka kusiwe na makando kando mengi je vina usahihi uliyo fikia 60%
IMG_20181210_172119.jpg

kama unajiamini unapima kutafuta nini, kupima tafsiri yake ni kuondoa uatata juu ya whether you are +Veor -ve HIV status,

Usiseme unajiamini, kuna siku utapata suprise unayoitafuta.
 
Wajameni ninapenda kutumia Sana hivi ata kupima mizigo ya dharura ili ata rubber ikipasuka kusiwe na makando kando mengi je vina usahihi uliyo fikia 60%
View attachment 963269
Kuna kitu kinaitwa window period. Mtu anakuwa na virusi ana uwezo wa kuambukiza lakini bado maambukizi hayaonekani katika vipimo isipokuwa PCR. Jihadhari sana
 
Kwanza ningependa kuwapa hongera watu wote walioamua kwenda kupima bila kujali majibu yalikuwaje. Kwa kweli kitendo cha kuamua kwenda kupima ni ujasiri wa hali. Mimi sikuwahi kuupata ujasiri huo mpaka mama alipotishia kuwa kama tusingeende kupima basi angesitisha huduma.

Sikua na jinsi ya kufanya, siku mbili hizi nimekuwa nawaza sana. Sasa leo nikasema ngoja nijipeleke mwenyewe kwanza. Ili nijue afya yangu kabla mamaa hajanipeleka kwa nguvu atakapogomea kutoa huduma.

Nikaenda hospitali. Nilipofika nikamwambia yule mhudumu. Nimekuja kupima kwa utashi na hiyari yangu mwenyewe. Najua kuna majibu ya aina mbili. Sitaki maelezo yoyote mengine naomba nipime. Jamaa akanielewa akanitoba akatoa damu. Sio siri nilitetemeka wakati nasubiri majibu. Nikasikia harufu ya kikwapa wakati asubuhi nilipaka deodorant. Dakika tano hizi nilikuwa kwenye hali ngumu sana.

Niliwaza mademu wote niliowahi kukutana nao. Baadae nikajipa moyo mbona kuna watu wanaishi na maambukizi. Mimi sitakuwa wa kwanza. Mhudumu akanistua. "Huko tayari kwa majibu yako". Hapo ndipo nilisikia harufu zaidi ya kikwapa. Midomo ikakauka. Nikajikamua. Nikamjibu "Ndio maana nimekuja kupima".

"Hauna HIV. HAUNA UKIMWI". Nikamuangalia. Nikashusha pumzi kwa nguvu. Nikamjibu. Asante sana. Nimetoka hapo nikajipongeza kwa Mirinda ya baridiiii.

Sasa nikirudi home. Nitamwambia wife, achague twende tupime wapi. Aseme mwenyewe. Nitajifanya sijapima. I hope na yeye atakuwa poa. Pengine amekwisha pima ndio maana kaanza figisu figusu. Nitawapa mrejesho.
HATA NINGEKUA MIMI NDIO NIMEKUPIMA lazima ningekuambia HUNA UKIMWI.Ya nini unifie ofisini kwangu kibwege kwa mi rayvdiamond yako!!!
 
Mkuuu sio lazima iwe dakika 15-20 inategemeana na kipimo mkuu,
Sio kila kipimo kinatoa majibu kwa muda huo kuna baadi ya vipimo huchukua hadi masaa kadhaa
Muhimu nikujua ni aina gani ya kipimo kilitumika baasi
Mfano aliyepima miaka ya nyuma atakuambia inakuchukua siku tatu hadi tano kupata majibu, so inategemeana na kipimo
kuna vipimo vidogo na vikubwa
Unaweza kuchukuliwa damu sehemu mbili
Kwenye mshipa moja kwa moja ama kwenye kidole kama kipimo cha maleria vile
So ukichukuliwa damu katika mshipa jua utapimwa kwa kutumia kipimo kikubwa na ndio kizuri zaidi wakitoboa kidolen ni kipimo kidogo dakika chache kabisa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom