Leo na Kesho: CCM izidi kutawala Tanzania

Leo na Kesho: CCM izidi kutawala Tanzania

Masalu Jacob

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2017
Posts
1,440
Reaction score
1,645
Habari Tanzania!

Naomba kushiriki nanyi mawazo mapana na mtazamo usio kikomo. Katika uongozi wa awamu ya tano (5) nimegundua mambo makuu yafuatayo;

1. Nchi hii wapinzani waliopo wote kwa vyama vyote vilivyopo si wema kabisa 100% na hawafai abadani.

2. Rais kujiita mtetezi wa wanyonge ilikuwa fumbo juu ya CCM ya u-mimi na kujuana ( Mtendaji alipenda kujiweka kwa watu wasio nacho huku akiwaadhibu walionacho chamani). Hii ni fikra pana sana.

3. Nchi hii watu wengi sana wapo gizani juu ya elimu, rasilimali na sera maendeleo kutokana na kufungwa sambamba na kupumbazwa kifikra na watu wenye nia ovu kwa nchi yetu.

NB
Nitaisimamia CCM miaka yote na kuamini CCM ndio chama bora na safi kwa maendeleo ya taifa letu. Kiukweli vijana tuamke na tuione kesho ya nchi hii.

CCM ni bora zaidi kuliko kuishi bila chama hapa nchini.

Asante.
 
Upinzani ni muhimu sana mkuu.

Hivi unadhan kusingekuwa na upinzan Tanzania ingefika ilipo?

You have to think.
 
Upinzani ni muhimu sana mkuu.

Hivi unadhan kusingekuwa na upinzan Tanzania ingefika ilipo?

You have to think.
Ndugu,

Wapinzani waliopo hii leo kwa wingi huu tuonao nakuhakikishia hawana wema wowote juu ya taifa letu ukilinganisha na maslai yao binafsi.

Ogopa mtu anayekutetea hadharani; ndani ya chumba anakusengenya. Katika hili wanakosa uhalali kuitwa wema kwa taifa letu.

Asante.
 
Nakuunga Mkono Bwashee. Bila CCM nchi hii Ita yumba Sana. Nikweli tangu Mwaka 1995 kuliibuka Vuguvugu kubwa sana la wananchi kutaka Mabadiliko kupitia Mzee wetu wa Kiraracha na chama chake cha NCCR Mageuzi.

Watu wengi tulimuunga Mkono kutokana na Sera zake zilizokua Zimejaa Maziwa na Asali.

Mwaka 2000 Chama cha Wananchi CUF kilipata Nguvu sana Bara na Visiwani.

Lakini kuanzia Mwaka 2005 chama cha Chadema nacho kilipata Nguvu na kutia fora kabisa hasa Bara.

Lakini kosa walilolifanya chadema baada ya kuvimbishwa kichwa kwa kuungwa mkono na Watanzania wengi ni Kujaza Uhuni kwenye Mambo ya Msingi.

Mimi nilizipenda Sana Sera zao za Kupambana na Ufisadi.

Nikiri wazi kwamba tangu 2010 mpaka Mwaka 2015 sikukipigia kura chama changu cha Mapinduzi.

Niliwapigia Chadema maana Maneno yao yalikua yanamtoa Nyoka pangoni.

Walipewa ulimi wa kuaminika hatakama walichokisema walikua hawana Uwezo wa kukitekeleza.

Walikipaka chama cha Mapinduzi matope kwa wananchi na kukifanya chama cha Mapinduzi kinuke harufu mbaya sana kwa wananchi.

Nakubali kwamba kuna Skendo nyingine chadema walikua wanazitengeneza ilitu CCM ichukiwe na Watanzania na hapa niseme Kwa jinsi Ambavyo Magufuli alikuja na Kutuonyesha namna Bora ya kuongoza nchi ndipo tukaanza kuona upande wa shillingi wa chadema kwamba hawakua na nia Njema na Yale waliokua wanatuhubiria ilikua ni Mbwa mwitu kavaa mwili wa Kondoo.

Ashukuriwe Mwenyezi Mungu. Sijui kama chadema wangekua wamepata Kutawala nchi hii tungejua kwamba Maaragwe ni Mboga.

Tungeuzwa mpaka wajukuu zetu kwa Mabeberu. Nchi ingetafunwa mpaka Inge bakia makapi kabisa.

Wale jamaa walikua ni Kagenge kadogo cha wahuni Ambao walikuja kutulaghai kwa Maneno yao matamu ili wapate madaraka wafanye yao.

Leo wenye Akili zetu tunaona ni wapi walipokimbilia kwa kuganganya Watanzania kwamba hapa kwetu Ali ya kisiasa siyo nzuri.

Nimalizie kwa Kusema. Hata Shetani Hakosi wafuasi hivyo sishangai kuona bado kuna baadhi ya Watanzania wachache wana,shabikia wasichokijua.

Namshukuru Mungu Ndugu yetu Magufuli Amelala na Kura Yangu niliyompigia Oct Mwaka Jana.

Ningejisikia uchungu sana kama Angelala nikiwa sikumpigia Kura yangu.

Utengaji wake. Na Mambo Makubwa Aliyotufanyia nchi hii kwa miaka 5 mambo Ambayo yalishindikana kufanyika tangu tumepata Uhuru Mwaka 61 Yeye kwa miaka 5 Akayafanya, hakika Huyu ataishi mioyoni Mwetu.

Watu hawakujua kwanini watu tulikua tunataka Aongezewe hata miaka 10 Mingine. Tulitaka Atuvushe kabisa kutoka kwenye Nchi za Kudharauliwa na kuwa Super National.

Tanzania bila CCM nchi yetu Hakuna chama chenye kuweza kuongoza nchi yetu uo ndio Ukweli.
 
Ndugu,

Wapinzani waliopo hii leo kwa wingi huu tuonao nakuhakikishia hawana wema wowote juu ya taiga letu ukilinganisha na maslai yao binafsi.

Ogopa mtu anayekutetea hadharani; ndani ya chumba anakusengenya. Katika hili wanakosa uhalali kuitwa wema kwa taifa letu.

Asante.
Kwani mkuu na wewe ni musukuma?.
 
Bandiko lako bila namba muamala utapokeaje sasa?
 
Alichokifanya Marehemu ni kuingiza kundi kubwa la Clueless individuals kutoka Usukumani matokeo yake ndio haya
Wewe utakufa na stress tu! Wasukuma wapo na wataendelea kuwepo milele na milele yote na ndiyo wenye maamuzi nani atawale hapa TZ.
 
Back
Top Bottom