Leo Kubenea Anamshangilia Zitto!!??

Leo Kubenea Anamshangilia Zitto!!??

Ningemshangaa asinge-mshangilia kwani ZZK alikuwa anapigania waandishi na vyombo vya habari (of course na walaji wa habari) na Kubenea yote yanamhusu kwa ukaribu zaidi.
Hebu piga picha elimu ya Kubenea halafu ilete kwenye huu Muswada wa Habari ndipo utakajua yale makofi yalimaanisha nini
 
Hahahahhaha daaaa!! Siasa hizi unajua zamani nilikuwa simfahamu Kubenea zaidi ya kusoma habari zake kwenye magazeti yake ya udaku.

Mara ya kwanza kumuona siku ile bungeni anaongelea habari za shanga za wanawake daaah!

Jamaa mmoja anafanyanae kazi akanimbia zile makala alikuwa siyo yeye anayeandika alikuwa anaandikiwa na Dr Slaa.

Yeye alikuwa anaandika tu "Na Said Kubenea" nilikuwa najua kichwa sana huyu jamaa bungeni patakuwa moto kumbe hamna kitu aisee!

Sasa leo Kubenea amekuwa mtu wa kusafiria nyota ya Zitto.

Kubenea bana elimu yake ya hapa na pale.

Kubenea Elimu yake ni la saba B
 
Hii inafanana na pale mwenyekiti wa ccm alipomkumbatia mgana msindahi kwenye sherehe ya kukabidhiwa uenyekiti.
 
Nakushangaa wewe maana it was not personal but for national interest.Hiyo ndio siasa iliyokomaa.
 
Kwani kakosea wapi huyo S.Kubenea kanogewa na uwasilishaji wa Mzalendo Zzk kampa haki yake, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni
 
Bado nafikicha macho na wala siamini hiki ninachokiona. Naota au ndio ukweli wa hiki ninachokitazama? Hapana, siamini. Leo Kubenea anamshangilia Zitto!!?? Hii ni kali ya karne. Yaani pamoja na magomvi waliyonayo baada ya Kubenea kutumia vilivyo magazeti yake kumnanga Zitto lakini leo pale Bungeni anamshangilia na kumuona kama malaika na kuyashadidisha maudhui ya Zitto kwa bashasha ya makofi. Siamini ni Kubenea huyu huyu au mwingine au kilikuwa kivuli chake pale Bungeni.
Nikikumbuka wawili hao walivyogombana na kuadhiriana tena mbele ya hadhara na maandishi yasiyo ya kiungwana, lakini leo nawaona wamekaa pamoja tena kwa bashasha. Ama kweli hizi siasa zina mambo na vijambo. Tuweke akiba ya maneno!
http://mwanahalisionline.com/zito-kabwe-kutoka-uzalendo-hadi-usaka-tonge/
Zitto Kabwe Amjibu Kubenea....Asema ni Mgonjwa wa Chuki, Muongo na Kigeugeu | UDAKU SPECIAL BLOG
Usiwaamini wanasiasa by Zitto Kabwe
 
Hujamshangaa wakatiwakati ule anamshambulia lowada wakati was Richmond na vichwa vyake vya habari halafu baadae anamsifia kwa kifupi no MTU asiye na misimamo
 
Katika Siasa una dill watu wakinyakuana katika maslahi hununiana
Lakini wanapootea huwa pamoja na hushangiliana kwahili la muswaada wa harari waliramba pamoja
 
Visasi na nongwa wanazo watu wa ccm. Kwao wakikuchukia hata ufanye jema kwao ni baya tuu
Ndio maana hata JK alisema hawaaminiani hata maji ya kunywa akiyaacha mezani akitoka akirudi hayanywi
 
Hahahahhaha daaaa!! Siasa hizi unajua zamani nilikuwa simfahamu Kubenea zaidi ya kusoma habari zake kwenye magazeti yake ya udaku.

Mara ya kwanza kumuona siku ile bungeni anaongelea habari za shanga za wanawake daaah!

Jamaa mmoja anafanyanae kazi akanimbia zile makala alikuwa siyo yeye anayeandika alikuwa anaandikiwa na Dr Slaa.

Yeye alikuwa anaandika tu "Na Said Kubenea" nilikuwa najua kichwa sana huyu jamaa bungeni patakuwa moto kumbe hamna kitu aisee!

Sasa leo Kubenea amekuwa mtu wa kusafiria nyota ya Zitto.

Kubenea bana elimu yake ya hapa na pale.
Ndio madhara ya Elimu ya Hapa na Pale
 
Kweli siasa ni usanii. Kuna watu waliimba ukumbini "TUNA IMANI NA...".Lakini watu haoihao leo hii wnamshangilia MTUKUFU
 
Back
Top Bottom