Leo Kubenea Anamshangilia Zitto!!??

Leo Kubenea Anamshangilia Zitto!!??

Yule aliyekataa kupokea mkono wa salamu kwenye msiba kwa sababu za sababu za kisiasa alionekana yupo sahihi na Leo Kubenea anaonekana pia yupo sahihi.

Tuacheni unafiki.
 
We furaha yako ni kuona walio na tofauti kwa jambo fulani wanaendeleza kutofautiana hata kwa mambo ambayo wanakubaliana? Jambo linaloitwa reconciliation kwako halina nafasi? Ungependa mbegu ya chuki izidi kushamiri badala ya kuhubiri upendo? Hii tabia ni ya watu wa aina ya Boko Haram, Al Shabaab, ISIS, we uko kundi gani kati ya hayo! Your divide and rule tactics have little time ahead before it stops to operate. Try another way!
Mbona unanipeleka kushabikia vitu nisivyovitaka katika maisha yangu? Tunahubiri upendo na ndio maana ya huu uzi. Lengo ni kuwaonyesha watu kwamba uadui hauna mashiko katika maisha yetu ya kila siku.
 
Bado nafikicha macho na wala siamini hiki ninachokiona. Naota au ndio ukweli wa hiki ninachokitazama? Hapana, siamini. Leo Kubenea anamshangilia Zitto!!?? Hii ni kali ya karne. Yaani pamoja na magomvi waliyonayo baada ya Kubenea kutumia vilivyo magazeti yake kumnanga Zitto lakini leo pale Bungeni anamshangilia na kumuona kama malaika na kuyashadidisha maudhui ya Zitto kwa bashasha ya makofi. Siamini ni Kubenea huyu huyu au mwingine au kilikuwa kivuli chake pale Bungeni.
Nikikumbuka wawili hao walivyogombana na kuadhiriana tena mbele ya hadhara na maandishi yasiyo ya kiungwana, lakini leo nawaona wamekaa pamoja tena kwa bashasha. Ama kweli hizi siasa zina mambo na vijambo. Tuweke akiba ya maneno!
http://mwanahalisionline.com/zito-kabwe-kutoka-uzalendo-hadi-usaka-tonge/
Zitto Kabwe Amjibu Kubenea....Asema ni Mgonjwa wa Chuki, Muongo na Kigeugeu | UDAKU SPECIAL BLOG
Kwani lipi la ajabu hapo?
 
Yule aliyekataa kupokea mkono wa salamu kwenye msiba kwa sababu za sababu za kisiasa alionekana yupo sahihi na Leo Kubenea anaonekana pia yupo sahihi.

Tuacheni unafiki.
Kila aliyekiona kile kituko cha kutopeana mikono alikerwa sana. Lilikuwa ni tukio lisilo na uungwana hata kidogo
 
Mbona unanipeleka kushabikia vitu nisivyovitaka katika maisha yangu? Tunahubiri upendo na ndio maana ya huu uzi. Lengo ni kuwaonyesha watu kwamba uadui hauna mashiko katika maisha yetu ya kila siku.
Basi mpongeze Kubenea kumshangilia Zitto, usimshangae maana suala la kukosana na kusameheana ni la kijasiri.
 
Kwani lipi la ajabu hapo?
Pole sana kwa kushindwa kuiona ajabu. Yawezekana fikra na macho zipo tofauti ndio maana mwenzetu kwako sio ajabu. Ila rejea matamshi wawili hao kabla ya tukio la leo.
 
Basi mpongeze Kubenea kumshangilia Zitto, usimshangae maana suala la kukosana na kusameheana ni la kijasiri.
Hilo ni jambo kuu, na kwa kweli nampongeza kwa kuonyesha ujasiri wa hali ya juu.
 
Nafikiri ukitumia falsafa ya Adui wa Adui wako ni Rafiki basi utapata jibu, mara nyingine ni bora kuweka tofauti zenu binafsi ili kufanikisha lengo lenu kubwa.

Ni kama baadhi ya washabiki fulani wanavyomkubali Professa fulani katika kipindi hiki.

Yote hiyo ni sehemu ya siasa.
Point of correction....professor fulani= bwana yule
 
Bado nafikicha macho na wala siamini hiki ninachokiona. Naota au ndio ukweli wa hiki ninachokitazama? Hapana, siamini. Leo Kubenea anamshangilia Zitto!!?? Hii ni kali ya karne. Yaani pamoja na magomvi waliyonayo baada ya Kubenea kutumia vilivyo magazeti yake kumnanga Zitto lakini leo pale Bungeni anamshangilia na kumuona kama malaika na kuyashadidisha maudhui ya Zitto kwa bashasha ya makofi. Siamini ni Kubenea huyu huyu au mwingine au kilikuwa kivuli chake pale Bungeni.
Nikikumbuka wawili hao walivyogombana na kuadhiriana tena mbele ya hadhara na maandishi yasiyo ya kiungwana, lakini leo nawaona wamekaa pamoja tena kwa bashasha. Ama kweli hizi siasa zina mambo na vijambo. Tuweke akiba ya maneno!
http://mwanahalisionline.com/zito-kabwe-kutoka-uzalendo-hadi-usaka-tonge/
Zitto Kabwe Amjibu Kubenea....Asema ni Mgonjwa wa Chuki, Muongo na Kigeugeu | UDAKU SPECIAL BLOG
Wewe endelea kufikicha macho mkuu, mikono ikichoka tumwite scorpion ayatoe kabisa.
 
Wewe endelea kufikicha macho mkuu, mikono ikichoka tumwite scorpion ayatoe kabisa.
Pole sana. Hivi wewe unamuogopa Scorpion? Haifai kuwa muoga kiasi hicho, yeye Scorpion ndio inapaswa akuogope
 
Nafikiri ujafikiria vzri au umesahau kikwete alisema siasa ni siasa watu wanatukanana nje ya bunge wanashikana mikono vzri sasa punguza kufksha macho
 
Sasa ulitaka iwe vp! Ugonvi wao nn hadi uone mambo ya kushangaza, kama ingekuwa hivyo basi ninaimani kimaudhi upinzani na ccm hata salamu zisingekuwepo wao walikuwa na tofauti za kisiasa tu lakini wao ni wabunge ni kama ndugu, wacha uchonganishi, na kama wangekuwa na ugonvi basi ingekuwa ww na chama chako milivyobaka matokeo kuleeee unakokujua!
 
Ningemshangaa asinge-mshangilia kwani ZZK alikuwa anapigania waandishi na vyombo vya habari (of course na walaji wa habari) na Kubenea yote yanamhusu kwa ukaribu zaidi.
 
Sasa ulitaka iwe vp! Ugonvi wao nn hadi uone mambo ya kushangaza, kama ingekuwa hivyo basi ninaimani kimaudhi upinzani na ccm hata salamu zisingekuwepo wao walikuwa na tofauti za kisiasa tu lakini wao ni wabunge ni kama ndugu, wacha uchonganishi, na kama wangekuwa na ugonvi basi ingekuwa ww na chama chako milivyobaka matokeo kuleeee unakokujua!
Sijakuelewa ulichokusudia. Hebu weka vizuri mawazo yako ili ueleweke
 
Back
Top Bottom