Leo Kubenea Anamshangilia Zitto!!??

Leo Kubenea Anamshangilia Zitto!!??

MABOGOJOHA

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2016
Posts
541
Reaction score
427
Bado nafikicha macho na wala siamini hiki ninachokiona. Naota au ndio ukweli wa hiki ninachokitazama? Hapana, siamini. Leo Kubenea anamshangilia Zitto!!?? Hii ni kali ya karne. Yaani pamoja na magomvi waliyonayo baada ya Kubenea kutumia vilivyo magazeti yake kumnanga Zitto lakini leo pale Bungeni anamshangilia na kumuona kama malaika na kuyashadidisha maudhui ya Zitto kwa bashasha ya makofi. Siamini ni Kubenea huyu huyu au mwingine au kilikuwa kivuli chake pale Bungeni.

Nikikumbuka wawili hao walivyogombana na kuadhiriana tena mbele ya hadhara na maandishi yasiyo ya kiungwana, lakini leo nawaona wamekaa pamoja tena kwa bashasha. Ama kweli hizi siasa zina mambo na vijambo. Tuweke akiba ya maneno!
 
Hahahahhaha daaaa!! Siasa hizi unajua zamani nilikuwa simfahamu Kubenea zaidi ya kusoma habari zake kwenye magazeti yake ya udaku.

Mara ya kwanza kumuona siku ile bungeni anaongelea habari za shanga za wanawake daaah!

Jamaa mmoja anafanyanae kazi akanimbia zile makala alikuwa siyo yeye anayeandika alikuwa anaandikiwa na Dr Slaa.

Yeye alikuwa anaandika tu "Na Said Kubenea" nilikuwa najua kichwa sana huyu jamaa bungeni patakuwa moto kumbe hamna kitu aisee!

Sasa leo Kubenea amekuwa mtu wa kusafiria nyota ya Zitto.

Kubenea bana elimu yake ya hapa na pale.
 
Nafikiri ukitumia falsafa ya Adui wa Adui wako ni Rafiki basi utapata jibu, mara nyingine ni bora kuweka tofauti zenu binafsi ili kufanikisha lengo lenu kubwa.

Ni kama baadhi ya washabiki fulani wanavyomkubali Professa fulani katika kipindi hiki.

Yote hiyo ni sehemu ya siasa.
 
Zitto uwa hana tatizo na mtu wala kumuongelea mtu kwa chuki mara nyingi yeye uwa anakuja na data tu.
Hapo ndipo anapowasulubu wabaya wake. Anajua kupanga hoja na lazima utavutwa na maudhui ya hoja zake
 
Zitto uwa hana tatizo na mtu wala kumuongelea mtu kwa chuki mara nyingi yeye uwa anakuja na data tu.
kwa sababu na yeye aliwahi kuwa mwanaJF
running.png
 
Bado nafikicha macho na wala siamini hiki ninachokiona. Naota au ndio ukweli wa hiki ninachokitazama? Hapana, siamini. Leo Kubenea anamshangilia Zitto!!?? Hii ni kali ya karne. Yaani pamoja na magomvi waliyonayo baada ya Kubenea kutumia vilivyo magazeti yake kumnanga Zitto lakini leo pale Bungeni anamshangilia na kumuona kama malaika na kuyashadidisha maudhui ya Zitto kwa bashasha ya makofi. Siamini ni Kubenea huyu huyu au mwingine au kilikuwa kivuli chake pale Bungeni.
Nikikumbuka wawili hao walivyogombana na kuadhiriana tena mbele ya hadhara na maandishi yasiyo ya kiungwana, lakini leo nawaona wamekaa pamoja tena kwa bashasha. Ama kweli hizi siasa zina mambo na vijambo. Tuweke akiba ya maneno!
http://mwanahalisionline.com/zito-kabwe-kutoka-uzalendo-hadi-usaka-tonge/
Zitto Kabwe Amjibu Kubenea....Asema ni Mgonjwa wa Chuki, Muongo na Kigeugeu | UDAKU SPECIAL BLOG
Kwenye Siasa hakuna adui au rafiki wa Kudumu, so usishangae Tafadhali
 
We furaha yako ni kuona walio na tofauti kwa jambo fulani wanaendeleza kutofautiana hata kwa mambo ambayo wanakubaliana? Jambo linaloitwa reconciliation kwako halina nafasi? Ungependa mbegu ya chuki izidi kushamiri badala ya kuhubiri upendo? Hii tabia ni ya watu wa aina ya Boko Haram, Al Shabaab, ISIS, we uko kundi gani kati ya hayo! Your divide and rule tactics have little time ahead before it stops to operate. Try another way!
 
We furaha yako ni kuona walio na tofauti kwa jambo fulani wanaendeleza kutofautiana hata kwa mambo ambayo wanakubaliana? Jambo linaloitwa reconciliation kwako halina nafasi? Ungependa mbegu ya chuki izidi kushamiri badala ya kuhubiri upendo? Hii tabia ni ya watu wa aina ya Boko Haram, Al Shabaab, ISIS, we uko kundi gani kati ya hayo! Your divide and rule tactics have little time ahead before it stops to operate. Try another way!
 
Back
Top Bottom